Kuna wanaopanga maandamano ya nchi nzima kushinikiza kusiwe na uchaguzi 2020 na Magufuli aendelee kuwa Rais

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,266
Maandamano yatakayofanyika nchi nzima yanakuja. Najua ndugu mtanzania umetega sikio kutaka kufahamu ni maandamano ya nini.
Ndugu zangu watanzania maandamano yajayo ni maandamano ya kushinikiza kutofanyika uchaguzi kwani lengo ni kuendeleza maendeleo kwa gharama kubwa ya hela zitakazotumika kufanya uchaguzi ambao kimsingi hauna maana kwani hautabadili matokeo yaliyopo sasa pili kwenye maandamano hayohayo tutakuwa na lengo la kumuomba Rais magufuli akubali ombi la wananchi kuendelea kutuongoza hata baada ya miaka 10 kuisha tutaandamana hadi kieleweke maandamano yatafanyika tanzania nzima naamanisha kila mkoa ccm oyee magufuli oyee.

+254752679213

1569837492345.jpeg
 
Naunga mkono hoja, ila uchaguzi ambao usifanyike ni uchaguzi wa rais tuu, Magufuli aendelee. Lakini kwa wabunge na madiwani, uchaguzi uendelee tuu kama kawaida kama nilivyoshauri hapa

Na kwenye huo uchaguzi wa wabunge na madiwani, kwa heshima ya utendaji uliotukaka wa rais Magufuli na serikali yake ya awamu ya tano, katika uchaguzi wa wabunge na madiwani, Watanzania katika umoja wetu tutapaza sauti zetu na kuongea kwa sauti moja kupitia sanduku la kura kuwa tumemwelewa Magufuli na tunajua anataja kutupeleka wapi hivyo siku ya Uchaguzi Watanzania wote kazi ni moja tuu, "unachukua, unaweka, ..."
Malizia mwenyewe.
P
 
Subutu!!!!!

Subiri aone jeshi linaanza mazoezi ya vifaru na ndege vita na usafi mitaani siku 2 kabla ya maandamano.

Subiri aone matamko ya makamanda wa polisi wa mikoa kutahadhalisha vipigo vya mbwa mwitu na koko.

Subiri aone wakuu wa mikoa watakavyotahadhalisha hakuna muda wa maandamano kuna muda wa kazi za maendeleo tu

Nawaza kwa sauti tu wakuu.
 
Naunga mkono hoja, ila uchaguzi ambao usifanyike ni uchaguzi wa rais tuu, Magufuli aendelee. Lakini kwa wabunge na madiwani, uchaguzi uendelee tuu kama kawaida kama nilivyoshauri hapa

Na kwenye huo uchaguzi wa wabunge na madiwani, kwa heshima ya utendaji uliotukaka wa rais Magufuli na serikali yake ya awamu ya tano, katika uchaguzi wa wabunge na madiwani, Watanzania katika umoja wetu tutapaza sauti zetu na kuongea kwa sauti moja kupitia sanduku la kura kuwa tumemwelewa Magufuli na tunajua anataja kutupeleka wapi hivyo siku ya Uchaguzi Watanzania wote kazi ni moja tuu, "unachukua, unaweka, ..."
Malizia mwenyewe.
P

Paskali umelewa na mvinyo gani?
 
Waruhusu na waandamanaji watakaotaka rais atoke.
Siku wakiingia tu hao barabarani, wapinzani waanze kampeni ya kuandamana kumwambia ondoke waombe na vibali.
Hata wakikataliwa tunaweka kukmbukumbu sawa wasije wakasema wengine hawajaomba kibali.
 
Back
Top Bottom