Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,782
Nilikuwa macho toka saa nane usiku na kuna mtu nikaongea naye kwa simu kama dakika kumi hivi. Kufika saa tisa hivi nikasikia kama kitu kinanyata nje ya nyumba. Nilidhani ni mbwa. Hivyo nikafunua pazia kidogo nikachungulia nje. Lahaulah grill la jikoni lilikuwa wazi. Lakini mlango ulikuwa umefungwa nikajua wa mwisho kuingia alipitiwa.
Dakika 20 hivi baadae dogo kanigongea mlango kuwa kuna mtu kafungua dirisha na alikuwa anamulika na tochi. Kuja kuchunguza nyumba yote. Jumla ya madirisha mane haya ya aluminum yalikuwa yamefunguliwa yote.
Kilichosaidia ni ma grill, TUMENUSURIKA KUIBIWA. Mungu ni mwema wakati wote.
Baada ya hapo nikaingia JF na kukutana na hii habari ya folk aliyesema atafariki baada ya miezi minne kutokana na kansa ya kongosho.
Ni kupitia uzi nikakumbuka masahibu mengi wanayopitia wa JF wengine muda huu lakini kamwe hawajayaandika hapa. Naomba nisimulie machache bila kuathiri privacy zao. Kwa njia hii tunaweza kuona magumu mazito wanayopitia wenzetu hawa. Na pengine hata wewe uyakayesoma hii mada kuna mazito magumu unapitia. Basi mada hii ikawe faraja, kupeana moyo, kupeana pole na ikiwezekana kupeana ufumbuzi. Unakaribishwa nawe kuweka kisa chako. Kwa kusimulia tu unaweza kupata faraja ya ajabu na huenda ikawa mwanzo wa kupata ufumbuzi.
Watu wamekamatwa katika magonjwa makubwa yasiyotibika. Watu wamefungwa kwenye vifungo na laana za ukoo. Watu hapa wamedhulumiwa mali, fedha, mahusiano, kazi nknk
Watu hapa wamegombanishwa na wenza wao, familia, koo, marafiki, kazi. Watu hapa wamefungwa kwenye uchawi na ushirikina na kufanyiwa mambo machafu mno.
Jamii Forums kwa weledi wake ina nafasi ya kuokoa roho nyingi na kuponya maumivu mengi.
Niandikapo mada hii kuna mwanaJF mwenzetu yuko kwenye maumivu makubwa kitandani akisubiri kukatwa mguu wake muda wowote wiki hii. Bado ni kijana lakini ndio hivyo tena. Anaenda kuwa mlemavu. Hujafa hujaumbika. Lakini ulemavu ni wa kimwili tu. Bado ana nafasi ya kusimama na kusonga mbele baada ya kupona. Tumuombee sana
Tuna wana JF wenzetu hapa kwao ajira imekuwa ni jinamizi linalotisha sana. Pamoja na kisomo kizuri na CV nzuri lakini kila walipopita wameishia kuahidiwa ahadi tasa. Wengine wanafamilia na wanategemewa na wazazi. Wanapitia kipindi kigumu mno. Wanahitaji faraja yetu.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanapitia kipindi kigumu mno kwenye ndoa na mahusiano yao. Inawezekana hata wewe ni mmojawapo.
Mume mlevi, malaya, mke si mwaminifu, wengine wameishia kutendwa na kudhulumiwa. Mmechuma wote mkaishi kwa dhiki lakini unakuja kugundua kumbe mwenza wako hakuwa na mapenzi ya kweli kwako.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanapitia kipindi kigumu mno cha mafarakano kwenye ukoo. Kuoneana wivu na kijicho. Kufanyiana fitina, kurogana, kudhulumiwa na mambo mengine mabaya sana.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wamechafuliwa nyota zao na kujikuta hawana kinga za kiroho tena. Roho la kukataliwa limetamalaki kwao. Hakuna wanachoshika kikasimama. Mambo hayaendi na wanajikuta ni watu wa kuharibu na kuchukiwa bila sababu.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanaumwa lakini wakifika kwenye hospital za kizungu hakuna ugonjwa unaoonekana na katika harakati za kusaka tiba wanajikuta wanaangukia Kwa matapeli ambao wengine tunao humu na wanasoma hii mada.
Ni maumivu juu ya maumivu
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanapitia kipindi kigumu mno cha madeni yasiyolipka mpaka wanaziogopa simu zao na nyumba zao. Wanaishi kama digidigi. Hawana amani hawana furaha
Kwakweli list ni ndefu na waliovurugiwa ramani za maisha si haba
Wapo wasaka mafanikio
Wapo wasaka ndoa
Wapo wasaka umaarufu
Wapo wasaka utajiri nk..
Wote hawa ni sehemu yetu ndani ya Jamii Forums. Natambua una magumu na changamoto unapitia. Lakini inawezekana lako lina nafuu kuliko la mwenzako. Sema neno la faraja sasa. JF ina impact kubwa sana. Ni kisemeo cha kuaminika cha jamii.
Neno lako moja linaweza kuwa tiba kubwa kwa wengi.
Dakika 20 hivi baadae dogo kanigongea mlango kuwa kuna mtu kafungua dirisha na alikuwa anamulika na tochi. Kuja kuchunguza nyumba yote. Jumla ya madirisha mane haya ya aluminum yalikuwa yamefunguliwa yote.
Kilichosaidia ni ma grill, TUMENUSURIKA KUIBIWA. Mungu ni mwema wakati wote.
Baada ya hapo nikaingia JF na kukutana na hii habari ya folk aliyesema atafariki baada ya miezi minne kutokana na kansa ya kongosho.
Nimeambiwa nitafariki baada ya miezi 4 kutokana na kansa ya kongosho (pancreatic cancer stage 4)
Ripoti ya daktari inasema baada ya miezi 4 nitakufa kutokana na kansa ya kongosho (pancreatic cancer stage 4.) Kwa hiyo miezi minne ijayo nitaweza kuona kile marehemu wanachoona sijui kufa kunaumaje? Juzi nimepita kando ya makaburi nikaishia kutabasamu tu nilipogundua next 4 month nitafukiwa...
www.jamiiforums.com
Ni kupitia uzi nikakumbuka masahibu mengi wanayopitia wa JF wengine muda huu lakini kamwe hawajayaandika hapa. Naomba nisimulie machache bila kuathiri privacy zao. Kwa njia hii tunaweza kuona magumu mazito wanayopitia wenzetu hawa. Na pengine hata wewe uyakayesoma hii mada kuna mazito magumu unapitia. Basi mada hii ikawe faraja, kupeana moyo, kupeana pole na ikiwezekana kupeana ufumbuzi. Unakaribishwa nawe kuweka kisa chako. Kwa kusimulia tu unaweza kupata faraja ya ajabu na huenda ikawa mwanzo wa kupata ufumbuzi.
Watu wamekamatwa katika magonjwa makubwa yasiyotibika. Watu wamefungwa kwenye vifungo na laana za ukoo. Watu hapa wamedhulumiwa mali, fedha, mahusiano, kazi nknk
Watu hapa wamegombanishwa na wenza wao, familia, koo, marafiki, kazi. Watu hapa wamefungwa kwenye uchawi na ushirikina na kufanyiwa mambo machafu mno.
Jamii Forums kwa weledi wake ina nafasi ya kuokoa roho nyingi na kuponya maumivu mengi.
Niandikapo mada hii kuna mwanaJF mwenzetu yuko kwenye maumivu makubwa kitandani akisubiri kukatwa mguu wake muda wowote wiki hii. Bado ni kijana lakini ndio hivyo tena. Anaenda kuwa mlemavu. Hujafa hujaumbika. Lakini ulemavu ni wa kimwili tu. Bado ana nafasi ya kusimama na kusonga mbele baada ya kupona. Tumuombee sana
Tuna wana JF wenzetu hapa kwao ajira imekuwa ni jinamizi linalotisha sana. Pamoja na kisomo kizuri na CV nzuri lakini kila walipopita wameishia kuahidiwa ahadi tasa. Wengine wanafamilia na wanategemewa na wazazi. Wanapitia kipindi kigumu mno. Wanahitaji faraja yetu.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanapitia kipindi kigumu mno kwenye ndoa na mahusiano yao. Inawezekana hata wewe ni mmojawapo.
Mume mlevi, malaya, mke si mwaminifu, wengine wameishia kutendwa na kudhulumiwa. Mmechuma wote mkaishi kwa dhiki lakini unakuja kugundua kumbe mwenza wako hakuwa na mapenzi ya kweli kwako.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanapitia kipindi kigumu mno cha mafarakano kwenye ukoo. Kuoneana wivu na kijicho. Kufanyiana fitina, kurogana, kudhulumiwa na mambo mengine mabaya sana.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wamechafuliwa nyota zao na kujikuta hawana kinga za kiroho tena. Roho la kukataliwa limetamalaki kwao. Hakuna wanachoshika kikasimama. Mambo hayaendi na wanajikuta ni watu wa kuharibu na kuchukiwa bila sababu.
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanaumwa lakini wakifika kwenye hospital za kizungu hakuna ugonjwa unaoonekana na katika harakati za kusaka tiba wanajikuta wanaangukia Kwa matapeli ambao wengine tunao humu na wanasoma hii mada.
Ni maumivu juu ya maumivu
Kuna wanaJF wenzetu hapa wanapitia kipindi kigumu mno cha madeni yasiyolipka mpaka wanaziogopa simu zao na nyumba zao. Wanaishi kama digidigi. Hawana amani hawana furaha
Kwakweli list ni ndefu na waliovurugiwa ramani za maisha si haba
Wapo wasaka mafanikio
Wapo wasaka ndoa
Wapo wasaka umaarufu
Wapo wasaka utajiri nk..
Wote hawa ni sehemu yetu ndani ya Jamii Forums. Natambua una magumu na changamoto unapitia. Lakini inawezekana lako lina nafuu kuliko la mwenzako. Sema neno la faraja sasa. JF ina impact kubwa sana. Ni kisemeo cha kuaminika cha jamii.
Neno lako moja linaweza kuwa tiba kubwa kwa wengi.
Miaka ya neema, miaka ya uharibifu
Nimeamua kuandika hii mada kama nilivyoahidi baada ya kusoma hapa JF kuwa Lulu binti aliyepitia mitihani mingi katika maisha yake ya usichana anakaribia kuolewa! Nikasema inawezekana miaka ya uharibifu imekwisha! Kuna neno linasema.... Natazama kutakuwako miaka saba ya neema na miaka saba ya...
www.jamiiforums.com