MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Inasikitisha sana kwamba kuna Waislam bendera-fuata-upepo waliopotoka, ambao walishawishiwa na ule ujumbe uliokuwa ukisambazwa kwamba Kikwete anapaswa kupigiwa kura na Waislam KWA KUWA ni Muislam, na kwamba Dk. Slaa asipigiwe kura kwa kuwa ni ADUI wa WAISLAM!
Hii nimeipata baada ya kukutana na binti mdogo, tena AISHIYE Ughaibuni (Dubai), aliyenitusi kwa kuniita mpumbavu na Mkristo nisiyejielewa, kila Jumapili niko kanisani "kumuimbia bwana" na kusali, sijielewi, ati!
Inashangaza, Ijumaa kabla ya uchaguzi mkuu nilienda (kutimiza wajibu) masjid, pale BAKWATA, Kinondoni, na Jakaya Kikwete - Muislam Mwenzetu - alikuwapo. Tulimwombea dua, kama Muislam Mwenzetu, na si kwa misingi ya chama chake. Tulimtakia kheri.
LAKINI SIKUMPIGIA KURA!
Waislam sasa wajifunze kutofautisha kati ya MAFUNDISHO ya KIDINI na SIASA. Vitu hivi viwili HAVICHANGANYIKI, ni kama MAJI na MAFUTA. Ukiweka mafuta ndani ya ndoo ya maji, yataelea juu, kwa kuwa hayana DENSITY ya kutosha.
Huyu mwenzetu KWELI KAPOTEA, na inashangaza, kama binti mdogo kama huyu amepotoka, je, waliomzidi umri?
Ukweli ni kwamba, asilimia 90 ya Waislam HAWAIJUI DINI, huku wakidhani wanaijua. Hii ni kwa mujibu wa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, aliyetoa hotuba siku ya Ijumaa, tarehe 29 Oktoba 2010, akiwataka Waislam KUJIFUNZA DINI!
Huyu binti, licha ya kujifanya anaijua sana dini, alikiri kwamba HAKUISOMEA madrassat!
Inasikitisha, lakini, kwetu sisi tunaodai kwamba dini yetu ndiye ya HAKI na UKWELI, matendo yetu YANATUTOFAUTISHA na mafundisho ya Uislam, ambao maana yake halisi ni AMANI!
Amani kwako, amani kwetu wote!
Tukubaliane kutofautiana KISIASA, tuziweke dini zetu pembeni!
-> Mwana wa Haki
P.S. Sijui nilie au nicheke? Ati nimeritadi kwa kumchagua Slaa? Duh!
Hii nimeipata baada ya kukutana na binti mdogo, tena AISHIYE Ughaibuni (Dubai), aliyenitusi kwa kuniita mpumbavu na Mkristo nisiyejielewa, kila Jumapili niko kanisani "kumuimbia bwana" na kusali, sijielewi, ati!
Inashangaza, Ijumaa kabla ya uchaguzi mkuu nilienda (kutimiza wajibu) masjid, pale BAKWATA, Kinondoni, na Jakaya Kikwete - Muislam Mwenzetu - alikuwapo. Tulimwombea dua, kama Muislam Mwenzetu, na si kwa misingi ya chama chake. Tulimtakia kheri.
LAKINI SIKUMPIGIA KURA!
Waislam sasa wajifunze kutofautisha kati ya MAFUNDISHO ya KIDINI na SIASA. Vitu hivi viwili HAVICHANGANYIKI, ni kama MAJI na MAFUTA. Ukiweka mafuta ndani ya ndoo ya maji, yataelea juu, kwa kuwa hayana DENSITY ya kutosha.
Huyu mwenzetu KWELI KAPOTEA, na inashangaza, kama binti mdogo kama huyu amepotoka, je, waliomzidi umri?
Ukweli ni kwamba, asilimia 90 ya Waislam HAWAIJUI DINI, huku wakidhani wanaijua. Hii ni kwa mujibu wa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, aliyetoa hotuba siku ya Ijumaa, tarehe 29 Oktoba 2010, akiwataka Waislam KUJIFUNZA DINI!
Huyu binti, licha ya kujifanya anaijua sana dini, alikiri kwamba HAKUISOMEA madrassat!
Inasikitisha, lakini, kwetu sisi tunaodai kwamba dini yetu ndiye ya HAKI na UKWELI, matendo yetu YANATUTOFAUTISHA na mafundisho ya Uislam, ambao maana yake halisi ni AMANI!
Amani kwako, amani kwetu wote!
Tukubaliane kutofautiana KISIASA, tuziweke dini zetu pembeni!
-> Mwana wa Haki
P.S. Sijui nilie au nicheke? Ati nimeritadi kwa kumchagua Slaa? Duh!