Ndugu zangu.,
Ndio, kuna walioamua kutetea uvivu wao kwa kusingizia Freemasons.
Nimepata kusoma kitabu cha Sir Andy Chande kiitwacho ' Knight In Africa'. Huko nyuma nilimsikia tu mtu anayeitwa Andy Chande, lakini, kupitia kitabu chake nikamfahamu zaidi alikotokea.
Kupitia simulizi ya maisha yake unaona jinsi alivyo mchapakazi. Anatoa mifano mingi ya kazi alizofanya; kwenye biashara na hata utumishi wa taifa hili.
Na jioni moja nilipomwona pale kwenye reception nyumbani kwa Balozi wa Sweden nikashawishika kuongea naye. Ucheshi niliouona kwenye maandiko yake upo pia kwa Andy unapozungumza naye. Kitabu chake kinasimulia pia historia ya nchi yetu. Kinatusaidia kuelewa tulikotoka, tulipo sasa na kuweza kufikiri juu ya wapi tuendako.
Andy alikuwa pia rafiki wa Julius Nyerere tangu enzi za kudai uhuru wa nchi hii. Andy aliwahi kumkatalia Julius alipoombwa akagombee Ubunge Tabora kwenye uchaguzi wa kura tatu. Akatamaka; " I would save better as a business man rather than a politician".
Famlia yake, kuanzia babu yake ni ya wafanyabiashara. Pale Bukene, Shinyanga, walianza na biashara ya kuuza magunia. Wakafanya pia biashara ya vinu vya kusaga na kukoboa. Baadae Andy na familia yake wakahamia Dar. Mbele ya Stesheni Kuu ya Tazara iliko sasa kampuni ya Azam ndipo kilipokuwa kiunga cha akina Chande. Walianza kwa kufyeka mapori. Hapo wakaweka vinu vya kukoboa na kusaga.
Asubuhi moja enzi za Azimio la Arusha, mwaka 1967, Andy anasimulia kwenye kitabu chake, kuwa aliamka asubuhi moja kwenda kiwandani kwao. Yeye alikuwa meneja wa kiwanda hicho. Getini akawakuta askari wa FFU. Akaambiwa kuwa kuanzia siku hiyo kiwanda kimetaifishwa. Kikaitwa National Milling Cooperation. Aakaingizwa ofisini kwake akabidhi ofisi kwa Meneja mpya ambaye hakuwahi hata kukutana naye mitaani.
Alipomaliza kufanya shughuli ya kukabidhi, Andy akumuuliza Meneja Mpya kama angependa aongozane naye akamtambulishe kwa wafanyakazi wengine. Andy akaambiwa imetosha, aende zake tu.
Siku hiyo hiyo Andy akaitwa na rafiki yake Julius aende Ikulu. Hata alipoingia Ikulu, Andy alimwona Julius mwingine. Hakuwa mcheshi kama ilivyokuwa kawaida yake. Julius akamwambia Andy akae kitako na hapo hapo akamfahamisha maamuzi ya kutaifisha kiwanda chao na kuwa Shirika la Umma.
Na cha ajabu, Julius akamwomba Andy awe Mwenyekiti wa Kwanza wa Bodi ya National Milling Cooperation!
Andy akakubali! Na akaifanya kazi ile kwa nguvu zake zote.
Inasikitisha kuona leo Andy anaanikwa kwenye magazeti ya udaku na kutolewa taswira hasi. Tena ni Andy huyu huyu ambaye aliwahi kuwa mmoja wa wajunbe wa Tume iliyokuwa ikipitia filamu zote zinazoingizwa Tanzania kuziangalia kabla umma haujaonyeshwa. Lengo lilikuwa kuhakikisha kuwa filamu hizo za kigeni haziathiri maadili, mila na utamaduni wetu.
Leo Andy amekuwa mhanga wa baadhi ya vyombo vya habari vinavyokiuka maadili, mila na utamaduni wetu, kwa kumuanika hadharani, tena kwa kuweka picha zake, bila ridhaa yake, kuwa ni mwanachama wa jumuiya ya Freemasons, jumuiya ambayo, kwa kupotosha umma, media inadai wanachama wake wanaamudu mashetani!
Naam, kuna waliamua kutetea uvivu wao kwa kusingizia Freemasons! Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
Ndio, kuna walioamua kutetea uvivu wao kwa kusingizia Freemasons.
Nimepata kusoma kitabu cha Sir Andy Chande kiitwacho ' Knight In Africa'. Huko nyuma nilimsikia tu mtu anayeitwa Andy Chande, lakini, kupitia kitabu chake nikamfahamu zaidi alikotokea.
Kupitia simulizi ya maisha yake unaona jinsi alivyo mchapakazi. Anatoa mifano mingi ya kazi alizofanya; kwenye biashara na hata utumishi wa taifa hili.
Na jioni moja nilipomwona pale kwenye reception nyumbani kwa Balozi wa Sweden nikashawishika kuongea naye. Ucheshi niliouona kwenye maandiko yake upo pia kwa Andy unapozungumza naye. Kitabu chake kinasimulia pia historia ya nchi yetu. Kinatusaidia kuelewa tulikotoka, tulipo sasa na kuweza kufikiri juu ya wapi tuendako.
Andy alikuwa pia rafiki wa Julius Nyerere tangu enzi za kudai uhuru wa nchi hii. Andy aliwahi kumkatalia Julius alipoombwa akagombee Ubunge Tabora kwenye uchaguzi wa kura tatu. Akatamaka; " I would save better as a business man rather than a politician".
Famlia yake, kuanzia babu yake ni ya wafanyabiashara. Pale Bukene, Shinyanga, walianza na biashara ya kuuza magunia. Wakafanya pia biashara ya vinu vya kusaga na kukoboa. Baadae Andy na familia yake wakahamia Dar. Mbele ya Stesheni Kuu ya Tazara iliko sasa kampuni ya Azam ndipo kilipokuwa kiunga cha akina Chande. Walianza kwa kufyeka mapori. Hapo wakaweka vinu vya kukoboa na kusaga.
Asubuhi moja enzi za Azimio la Arusha, mwaka 1967, Andy anasimulia kwenye kitabu chake, kuwa aliamka asubuhi moja kwenda kiwandani kwao. Yeye alikuwa meneja wa kiwanda hicho. Getini akawakuta askari wa FFU. Akaambiwa kuwa kuanzia siku hiyo kiwanda kimetaifishwa. Kikaitwa National Milling Cooperation. Aakaingizwa ofisini kwake akabidhi ofisi kwa Meneja mpya ambaye hakuwahi hata kukutana naye mitaani.
Alipomaliza kufanya shughuli ya kukabidhi, Andy akumuuliza Meneja Mpya kama angependa aongozane naye akamtambulishe kwa wafanyakazi wengine. Andy akaambiwa imetosha, aende zake tu.
Siku hiyo hiyo Andy akaitwa na rafiki yake Julius aende Ikulu. Hata alipoingia Ikulu, Andy alimwona Julius mwingine. Hakuwa mcheshi kama ilivyokuwa kawaida yake. Julius akamwambia Andy akae kitako na hapo hapo akamfahamisha maamuzi ya kutaifisha kiwanda chao na kuwa Shirika la Umma.
Na cha ajabu, Julius akamwomba Andy awe Mwenyekiti wa Kwanza wa Bodi ya National Milling Cooperation!
Andy akakubali! Na akaifanya kazi ile kwa nguvu zake zote.
Inasikitisha kuona leo Andy anaanikwa kwenye magazeti ya udaku na kutolewa taswira hasi. Tena ni Andy huyu huyu ambaye aliwahi kuwa mmoja wa wajunbe wa Tume iliyokuwa ikipitia filamu zote zinazoingizwa Tanzania kuziangalia kabla umma haujaonyeshwa. Lengo lilikuwa kuhakikisha kuwa filamu hizo za kigeni haziathiri maadili, mila na utamaduni wetu.
Leo Andy amekuwa mhanga wa baadhi ya vyombo vya habari vinavyokiuka maadili, mila na utamaduni wetu, kwa kumuanika hadharani, tena kwa kuweka picha zake, bila ridhaa yake, kuwa ni mwanachama wa jumuiya ya Freemasons, jumuiya ambayo, kwa kupotosha umma, media inadai wanachama wake wanaamudu mashetani!
Naam, kuna waliamua kutetea uvivu wao kwa kusingizia Freemasons! Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam