Kuna wakati huwa tunalishwa matango pori na mjamaa

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,606
696,713
Ziara ya Mwanza ilikuwa tofauti kabisa na ya Bukoba ya Mwanza tumeona yatokanayo.

Mama mjane aliyedhulumiwa kiwanja na wakili maarufu na kisha kupewa kibunda cha pesa pale pale uwanjani na mkulu... Niliona camera zilivyokuwa zinamzunguka yule mama wakati akiangua kilio cha shukrani na kumshukuru 'rais wa wanyonge'... MWANZA HAKUKUWA NA UTUMBUAJI.

Ziara iliyofuatia ni ya Bukoba, tumeona yaliyotokea. Udhalilishwaji wa kiwango chake na kukiuka miiko ya uongozi bora heshima na kuthamini utu wa mtu.

Kuna kitu kilizungumzwa kwa msisitizo sana pale na ikawa kama ndio sababu ya uhakiki usioisha na ushindi mkubwa wa hayo mazoezi.

Ni watumishi watatu waliobainika kudai malimbikizo ya mishahara na marupurupu.

Mmoja BILIONI SABA, mwingine BILIONI MBILI na wa mwisho million mia moja.

Sitaki kutetea sana kama hili lilikuwa ni uzembe ama lilifanyika kwa dhamira maalum.

Lakini tukirudi kwenye uhalisia hizi pesa zisingelipika.. Yaani hizi BILIONI 7 na BILIONI 2. Hao walipwaji sijui hata wangezibebaje hizo pesa huko kwenye akaunti zao.

Hapa ni wazi kuna makosa makubwa yalifanyika.

Makosa kama hayo ni ya kawaida kwenye taasisi za serikali, uzembe umetamalaki, watu wanafanya kazi kwa mazoea na uwajibikaji hakuna
Hili si la wafanyakazi wa kawaida tu bali mpaka wa ngazi za juu na kwenye mambo sensitive ya nchi.

Hivi karibuni kuna proffesa aliyeamika kupewa mikataba aisome na kujiridhisha kama kilichoandikwa ni sahihi na kina maslahi kwa nchi.

Yeye hakufanya hivyo badala yake alisaini bila kusoma na kwenye utetezi wake akadai kuwa aliwaamini wasaidizi wake. HAKUCHUKULIWA HATUA YOYOTE.

Hawa wanaoitwa wasaidizi ni watu wa hovyo kabisa, nao huwa sio watendaji kabisa.

Kwa sehemu kubwa kazi kama hizo hufanywa na matarishi na makatibu muhtasi hawa ndio watu wanaomenyeka hasa.

Hawa wakushamaliza kuchapa kazi husika hupelekewa msaidizi wa mkuu naye huuuliza umeangalia iko vizuri hujibiwa kwa unyenyekevu NDIO BOSS...!

Na yeye bila kujiridhisha husaini na kumpelekea mkuu wake wa kazi ambaye naye bila kujiridhisha huuuliza swali lilelile UMEIPITIA IKO SAWA? msaidizi bila kusita hujibu NDIO MKUU.. anasaini na kutoa maamuzi.

Mikataba mingi imerigharimu taifa kwenye mambo ya kizembe na uvivu wa kusoma kama haya.

Tunawaamini matarishi na wapicha chapa kwa asilimia mia moja wakati wengi elimu zao si za kiwango cha juu.

Hawa wana sehemu yao kuchapa basi... Kuangalia na kupitia usahihi wa kilichochapishwa sio wao wengi tunajua viingereza na hata viswahili vyao ni vile vya Facebook.

Ishu ya BILIONI 7 na BILIONI 2 kuna mtu aliona shida ilipo na akarepoti... Imeagizwa wahusika wachukuliwe hatua stahiki za kisheria.

Nimejiuliza tu hata yule prof naye atachukuliwa hatua za kisheria kwa kusaini mkataba mbovu kiasi kile na kukiri mwenyewe kuwa hakuusoma?

Kuna siku zitasainiwa nyaraka za kuuza nchi na utetezi uwe kama huu. Hakuna kuoneana aibu au kutoa maamuzi kwa macho ya makengeza.

Wote waliohusika na kusaini malipo ya BILIONI 7 wawajibishwe lakini pia Prof na watendaji wake nao wasiachwe.

Kuleta mizania ya haki kwenye utawala bora nao wachukuliwe hatua stahiki kwa makosa waliyofanya.
 
"Kuna siku zitasainiwa nyaraka za kuuza nchi na utetezi uwe kama huu"

We unadhani nchi inauzwaje??! nchi inauzwa kwa mikataba mibovu, ukisikia mkataba mbovu umesainiwa ujue tayari tumeuzwa, kama unadhan nchi inauzwa kama shamba au gari ambapo utabadir jina la mmiliki sio hivo.
 
Ziara ya Mwanza ilikuwa tofauti kabisa na ya Bukoba... Ya Mwanza tumeona yatokanayo... Mama mjane aliyedhulumiwa kiwanja na wakili maarufu na kisha kupewa kibunda cha pesa pale pale uwanjani na mkulu... Niliona camera zilivyokuwa zinamzunguka yule mama wakati akiangua kilio cha shukrani na kumshukuru 'rais wa wanyonge'... MWANZA HAKUKUWA NA UTUMBUAJI....
Ziara iliyofuatia ni ya Bukoba, tumeona yaliyotokea... Udhalilishwaji wa kiwango chake na kukiuka miiko ya uongozi bora heshima na kuthamini utu wa mtu
Kuna kitu kilizungumzwa kwa msisitizo sana pale na ikawa kama ndio sababu ya uhakiki usioisha na ushindi mkubwa wa hayo mazoezi
Ni watumishi watatu waliobainika kudai malimbikizo ya mishahara na marupurupu.. Mmoja BILIONI SABA, mwingine BILIONI MBILI na wa mwisho million mia moja
Sitaki kutetea sana kama hili lilikuwa ni uzembe ama lilifanyika kwa dhamira maalum... Lakini tukirudi kwenye uhalisia hizi pesa zisingelipika.. Yaani hizi BILIONI 7 na BILIONI 2... Hao walipwaji sijui hata wangezibebaje hizo pesa huko kwenye akaunti zao... Hapa ni wazi kuna makosa makubwa yalifanyika
Makosa kama hayo ni ya kawaida kwenye taasisi za serikali, uzembe umetamalaki, watu wanafanya kazi kwa mazoea na uwajibikaji hakuna
Hili si la wafanyakazi wa kawaida tu bali mpaka wa ngazi za juu na kwenye mambo sensitive ya nchi... Hivi karibuni kuna proffesa aliyeamika kupewa mikataba aisome na kujiridhisha kama kilichoandikwa ni sahihi na kina maslahi kwa nchi... Yeye hakufanya hivyo badala yake alisaini bila kusoma na kwenye utetezi wake akadai kuwa aliwaamini wasaidizi wake... HAKUCHUKULIWA HATUA YOYOTE
Hawa wanaoitwa wasaidizi ni watu wa hovyo kabisa, nao huwa sio watendaji kabisa... Kwa sehemu kubwa kazi kama hizo hufanywa na matarishi na makatibu muhtasi hawa ndio watu wanaomenyeka hasa.... Hawa wakushamaliza kuchapa kazi husika hupelekewa msaidizi wa mkuu naye huuuliza umeangalia iko vizuri hujibiwa kwa unyenyekevu NDIO BOSS...! Na yeye bila kujiridhisha husaini na kumpelekea mkuu wake wa kazi ambaye naye bila kujiridhisha huuuliza swali lilelile UMEIPITIA IKO SAWA? msaidizi bila kusita hujibu NDIO MKUU.. anasaini na kutoa maamuzi
Mikataba mingi imerigharimu taifa kwenye mambo ya kizembe na uvivu wa kusoma kama haya... Tunawaamini matarishi na wapicha chapa kwa asilimia mia moja wakati wengi elimu zao si za kiwango cha juu... Hawa wana sehemu yao kuchapa basi... Kuangalia na kupitia usahihi wa kilichochapishwa sio wao. . wengi tunajua viingereza na hata viswahili vyao ni vile vya Facebook...
Ishu ya BILIONI 7 na BILIONI 2 kuna mtu aliona shida ilipo na akarepoti... Imeagizwa wahusika wachukuliwe hatua stahiki za kisheria.. Nimejiuliza tu hata yule prof naye atachukuliwa hatua za kisheria kwa kusaini mkataba mbovu kiasi kile na kukiri mwenyewe kuwa hakuusoma?
Kuna siku zitasainiwa nyaraka za kuuza nchi na utetezi uwe kama huu.... Hakuna kuoneana aibu au kutoa maamuzi kwa macho ya makengeza... Wote waliohusika na kusaini malipo ya BILIONI 7 wawajibishwe lakini pia Prof na watendaji wake nao wasiachwe... Kuleta mizania ya haki kwenye utawala bora nao wachukuliwe hatua stahiki kwa makosa waliyofanya


Hebu format paragraph vizuri boss. Na hamu yakuisoma lakini ikiwa hivi, inakatisha tamaa hata kuanza.
 
483abcdfd3875f50094cbefbdbe36e41.jpg
 
Pale katerero ilikuwa sound tu
Kwani hamjui Joni ni MTU wa puropagander sana na hakumbuki asemacho awali.

Amesema kwa Leo nawasamehe wale madedi kisha baadae wasikia ametungua ndolo.
Joni Joni Joni Joni Chonde Chonde
You can fool some people some time but you can't fool all people all the time.
 
18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom