Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
 
My dear Sky Eclat

Ndio maana siku zote wazazi huwa wanashauriwa kuwa wanakula meza moja na watoto wao ili wawafundishe TABLE MANNERS ikiwamo kuwafikiria wengine na hata namna ya kutafuna chakula.

Inawezekana hao wageni ndio wale waliopelekwa boarding wakiwa bado wadogo sana (darasa la tatu) wakakosa muda wa kufundishwa tabia njema na wazazi/walezi wao.
 
My dear,

Ndio maana siku zote wazazi huwa wanashauriwa kuwa wanakula meza moja na watoto wao ili wawafundishe TABLE MANNERS ikiwamo kuwafikiria wengine na hata namna ya kutafuna chakula..
Sikuhizi baba anakula kwenye sofa huku anaangalia Man United inacheza, mama yuko Instagram na simu yake. Watoto anaachiwa dada apambambane nao mezani.
 
Noted. Ila mimi sipendi kabisa kula kwa watu. Na ikitokea basi huwa napakuwa chakula kiwango kidogo kadiri nitakavyoweza. Ni bora nisishibe ugenini, nitaenda kujazia mbele ya safari (nyumbani).
Binadamu ni social mammals, kula pamoja ni sehemu ya utamaduni wetu tangu enzi za mababu zetu. Tena kula pamoja ni kama tiba maana mtaongea na kucheka na wenzako.

Kitu cha kuzingatia ni ustaarabu tu mkiwa mnakula pamoja. Wengine wanaona ni kawaida ku fart saa ya kula kisa wamezoea kula wenyewe.
 
Kweli wazazi huwa baadhi wanafeli katika malezi.

Mtoto anafanya jambo la aibu unamuangalia tu hukemei unasahau kuwa yeye atachukulia sawa na tabia atakuwa nayo hadi utu uzima.
Kuna sherehe tulienda jirani akabeba wanae wote akaenda nap sasa mle ukumbini mezani zikaletwa sambusa acha waanze kugombania wakati zimeletwa idadi sawa na watu waliomo mezani na mama hakemei anaona tu kawaida.

Mwingine aliwekewa chakula akamfuata mama yake analia chakula kidogo mama akamjibu kula haraka ukarudie awamu nyingine.
Sasa watoto kama hao wakikua watakuwa na tabia gani kama sio za ajabu na wala haoni tatizo.

Mtoto usipomfunza na kumkemea anaweza kukutia aibu.
 
Kweli wazazi huwa baadhi wanafeli katika malezi.
Wakati wa likizo huu unapokea watoto wamekuja likizo. Asubuhi umezoea kuwakaangia watoto wako mayai manne lakini wenyewe umewafundisha kuwa ni lazima kila mtu apate.

Wanakuja watoto wageni wanamaliza mayai yote wanao wanabaki wanaangalia. Kama wangefundishwa wote wangegawana na wote wangepata hata kipande kidogo.
 
Sijui ni ulafi au Uzungu, wewe kama umepika wachache si shida ni yako? kwanini usiweke kwenye sahani na mkashea hasa kwenye upande wa mboga? Hivyo vipande vitatu ni vya gram ngapi kila kimoja? Chakula cha manung'uniko bhana mwisho mtu anigwe na mfupa kisa jicho la usuda la kuchukua samaki mmoja (tena kagawanywa vipande vitatu) mwenye gram 400.

Kwani haufahamu siku hizi chakula ni mboga, YAANI MBOGA INAKUWA KUBWA ZAIDI YA WALI/UGALI?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom