sirluta
JF-Expert Member
- Nov 28, 2012
- 6,325
- 2,486
Kama tujuavyo ni rahisi sana kupenda na kuingia katika mahusiano, ila ni ngumu pia kutoka katika Upendo hata kama ni wa siku moja. Nafsi ikipenda, asikuambie mtu. Tumeshuhudia KE/ME wakipenda hata wenye magonjwa mazito bila kujali.
Kuna wanaume huko kanda ya Ziwa Mkoa wa Mara Wilaya ya Tarime wameshawishiana kutowapenda wanawake waliokeketwa ili kukomesha mila hizo za ukeketaji. Nimebaki na maswali kichwani, je hilo zoezi linaweza kufanikiwa? Kuizuia nafsi isipende kwasababu ya ukeketaji! Mimi binafsi siwezi kuizuia nafsi yangu kupenda, sijui wengine.
Kuna wanaume huko kanda ya Ziwa Mkoa wa Mara Wilaya ya Tarime wameshawishiana kutowapenda wanawake waliokeketwa ili kukomesha mila hizo za ukeketaji. Nimebaki na maswali kichwani, je hilo zoezi linaweza kufanikiwa? Kuizuia nafsi isipende kwasababu ya ukeketaji! Mimi binafsi siwezi kuizuia nafsi yangu kupenda, sijui wengine.