Kuna Uwezekano Mwanaume kuacha kumpenda Mwanamke baada ya kugundua Amekeketwa?

sirluta

JF-Expert Member
Nov 28, 2012
6,325
2,486
Kama tujuavyo ni rahisi sana kupenda na kuingia katika mahusiano, ila ni ngumu pia kutoka katika Upendo hata kama ni wa siku moja. Nafsi ikipenda, asikuambie mtu. Tumeshuhudia KE/ME wakipenda hata wenye magonjwa mazito bila kujali.

Kuna wanaume huko kanda ya Ziwa Mkoa wa Mara Wilaya ya Tarime wameshawishiana kutowapenda wanawake waliokeketwa ili kukomesha mila hizo za ukeketaji. Nimebaki na maswali kichwani, je hilo zoezi linaweza kufanikiwa? Kuizuia nafsi isipende kwasababu ya ukeketaji! Mimi binafsi siwezi kuizuia nafsi yangu kupenda, sijui wengine.
 
Sio rahisi kuiambia nafsi mpende huyu, mchukie huyu.love is never about propaganda.
ila hivi karibuni nilikuwa naongea na kaka mmoja ambae ni mzawa wa kanda ya ziwa, akasema kuwa wadada waliokeketwa hawana shida yeyote, wanafurahia mapenzi vizuri tuu na kwamba issue ya kuzaa kwa shida ni propaganda ya Wazungu tuu.
Kuna ukweli wowote hapa?
 
Wakurya tupeni ukweli Tarime one. Mmewezaje kushawishiana msiwapende waliokeketwa? Je wakija huku twn kwetu pia tusiwapende?
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom