MeinKempf
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 11,094
- 7,218
Kutokana na kauli za kuchefua, kifedhuri, na kuudhi za viongozi wa magamba kama Makinda, Lukuvi na wengineo juu ya tukio lilotokea Arusha, mimi naona kuwa huu ni muda mwafaka kwa sisi watanzania kuwachangia pesa japo kwa njia ya mtandao (m-pesa, tigo pesa, airtel mone, sasatel money, )viongozi wa magamba ili waende maeneo kama lebanon, darful, syria, yemen, palestina , ukanda wa gaza, ukingo wa magharibi, maeneo ya jordan yatawafaa zaidi na kisha watapokuwa huko wawe mstari wa mbele ( frontline) japo kwa asiku tatu tu, na kisha wakati wa kurudi wamtembelee Hosni mbarak, Laurent Bagbo, na wengineo kwani zitawatosha kurudi na somo halisi. Msafara utaongozwa na Lukuvi na Wasira , wakisaidiwa na ndugai na makinda. naomba Nawasilisha.