Kuna umuhimu wa kuelimishana maana halisi ya haya maneno: Uzalendo, Ubeberu, Unyonge, Vita vya Kiuchumi na Maendeleo

mr mkiki

JF-Expert Member
Sep 22, 2016
5,583
11,659
Mtu anachangia 30% ya mshahara wake kama kodi. Zingine anawakopesha ziingie mfuko wa jamii. Anachangia mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) na tozo ya maendeleo ya ujuzi (SDL). Kama haitoshi, anachangia REA ya umeme vijijini kupitia LUKU na tozo ya mshikamano ya miamala ya simu

Huyu mtu anaambiwa ajifunze kuwa mzalendo kidogo aache ubinafsi maana hospitali, barabara na umeme vijijini vinahitajika. Hapo anachangia misiba, kuuguza na elimu kwenye jamii yake.Uzalendo kwenye nchi ngumu ni changamoto. Unaweza kutoa roho yako na bado ukaombwa uongeze uzalendo!

Kuna umuhimu wa kuelimishana maana halisi ya haya maneno:

1. Uzalendo
2. Ubeberu
3. Unyonge
4. Vita ya kiuchumi
5. Maendeleo
 
Nakumbuka Mwalimu wangu wa kiswahili alinifundisha kuwa hiyo misimu ilizuka kipindi Cha kupigania uhuru na baada ya uhuru.

Ghafla nikaanza kuisikia kipindi Cha Mwendazake!

Sasa hivi nikiisikia naanza kui-associate na maisha magumu
 
Mtu anachangia 30% ya mshahara wake kama kodi. Zingine anawakopesha ziingie mfuko wa jamii. Anachangia mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) na tozo ya maendeleo ya ujuzi (SDL). Kama haitoshi, anachangia REA ya umeme vijijini kupitia LUKU na tozo ya mshikamano ya miamala ya simu

Huyu mtu anaambiwa ajifunze kuwa mzalendo kidogo aache ubinafsi maana hospitali, barabara na umeme vijijini vinahitajika. Hapo anachangia misiba, kuuguza na elimu kwenye jamii yake.Uzalendo kwenye nchi ngumu ni changamoto. Unaweza kutoa roho yako na bado ukaombwa uongeze uzalendo!

Kuna umuhimu wa kuelimishana maana halisi ya haya maneno:

1. Uzalendo
2. Ubeberu
3. Unyonge
4. Vita ya kiuchumi
5. Maendeleo
Hayo ni maneno yaliyoondoka na Utawala wa wagagagigikoko. Sasa hivi tunadeal na kalamu tu mama amesema mambo ya kukaripiana na watu wazima hayawezi.

Mzungu akizingua ni maandishi tu, mbongo ukizingua ni maandishi tu, mambo ya kuzurura mtu mzima kama mwalimu wa zamu hatutaki mtu unakula mahindi barabarani hatutaki kabisa no mwendo wa kula kiyoyozi na mambo yanasonga.
 
Nakumbuka Mwalimu wangu wa kiswahili alinifundisha kuwa hiyo misimu ilizuka kipindi Cha kupigania uhuru na baada ya uhuru.

Ghafla nikaanza kuisikia kipindi Cha Mwendazake!

Sasa hivi nikiisikia naanza kui-associate na maisha magumu
yule ni tapeli,sijui mwendazake
 
Back
Top Bottom