Nandinii
JF-Expert Member
- Jun 19, 2019
- 2,573
- 2,808
Habari zenu wana MMU ,nimekuwa msomaji mzuri wa thread za watu lakini leo naona na mie nilete duku duku langu ambalo linanitatiza kila uchwao.
Mwaka 2017 baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wangu, niliamua kubaki peke yangu na kuielekeza akili yangu sehemu zenye maana zaidi katika maisha. Mwaka 2019 umekuwa ni mwaka ambao nimekuwa makini sana katika kuanzisha mahusiano na nikajikita zaidi katika dini na kuwa mkristo mzuri tu, nikaimarika zaidi.
Mwaka jana nimefuatwa na wanaume wengi tu wakitaka kuanzisha mahusiano na mie, nilikuwa naangalia sifa alizonazo na je ana hofu ya Mungu? Na kama ni muelewa? Wanapatikana lakini changamoto kubwa ni wanataka sex kabla ya mambo yote, ukizingatia mie sharti langu la kwanza hakuna kufanya mapenzi mpaka kwa kipindi fulani ambacho tutajipangia, wengi wa wanaume wanaokuja tunaishia njiani kwani wao wanakuwa hawawezi kukaa bila kufanya mapenzi. Na mie sikubali basi tunaishia kuachana tu, mpaka sasa nimechoka kuwa katika mahusiano tena.
Wanaume kwani kama umempenda mtu na una malengo naye kuna haja gani ya kufanya mapenzi kwanza? Au ndo nyie ambao mnataka kuonja then mtathimini kama linafaa au halifai? Halafu, kama kweli mnakuwa wakweli kwanini mtu anapokataa kutoa penzi kwa muda wa miez 3 na zaidi mnaondoka kimya kimya? Tena wengine wanajifanya wana hofu ya Mungu kabisa na wanaijua dini lakini ndiyo wa kwanza wanaendekeza ngono, badala ya kuangalia vigezo vingine vya mke sahihi.
Sasa sijajua huu msimamo wangu utanikosesha mume au la, maana mie msimamo wangu ndiyo huo. Ukinifuata hakuna sex mpaka nijihakikishie na tumeelewana hata kwa miezi 6. Yakikushinda basi unaweza kwenda, na wanaondoka kimya kimya.
Je, wakuu ninachofanya nakosea; kukataa kutoa penzi mpaka kwa wakati maalum? Au ndiyo mtu ukubali kutoa ale then asepe, aje mwingine ale asepe?
Mwaka 2017 baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wangu, niliamua kubaki peke yangu na kuielekeza akili yangu sehemu zenye maana zaidi katika maisha. Mwaka 2019 umekuwa ni mwaka ambao nimekuwa makini sana katika kuanzisha mahusiano na nikajikita zaidi katika dini na kuwa mkristo mzuri tu, nikaimarika zaidi.
Mwaka jana nimefuatwa na wanaume wengi tu wakitaka kuanzisha mahusiano na mie, nilikuwa naangalia sifa alizonazo na je ana hofu ya Mungu? Na kama ni muelewa? Wanapatikana lakini changamoto kubwa ni wanataka sex kabla ya mambo yote, ukizingatia mie sharti langu la kwanza hakuna kufanya mapenzi mpaka kwa kipindi fulani ambacho tutajipangia, wengi wa wanaume wanaokuja tunaishia njiani kwani wao wanakuwa hawawezi kukaa bila kufanya mapenzi. Na mie sikubali basi tunaishia kuachana tu, mpaka sasa nimechoka kuwa katika mahusiano tena.
Wanaume kwani kama umempenda mtu na una malengo naye kuna haja gani ya kufanya mapenzi kwanza? Au ndo nyie ambao mnataka kuonja then mtathimini kama linafaa au halifai? Halafu, kama kweli mnakuwa wakweli kwanini mtu anapokataa kutoa penzi kwa muda wa miez 3 na zaidi mnaondoka kimya kimya? Tena wengine wanajifanya wana hofu ya Mungu kabisa na wanaijua dini lakini ndiyo wa kwanza wanaendekeza ngono, badala ya kuangalia vigezo vingine vya mke sahihi.
Sasa sijajua huu msimamo wangu utanikosesha mume au la, maana mie msimamo wangu ndiyo huo. Ukinifuata hakuna sex mpaka nijihakikishie na tumeelewana hata kwa miezi 6. Yakikushinda basi unaweza kwenda, na wanaondoka kimya kimya.
Je, wakuu ninachofanya nakosea; kukataa kutoa penzi mpaka kwa wakati maalum? Au ndiyo mtu ukubali kutoa ale then asepe, aje mwingine ale asepe?