Kuna ukweli kiasi gani Tanzania hakuna uhuru na haki

mwengeso

JF-Expert Member
Nov 27, 2014
9,219
6,650
Lengo kuu lililo kwenye Ilani ya CHADEMA ya Uchaguzi Mkuu, 2020 ni UHURU, HAKI NA MAENDELEO YA WATU.

Suala la tafsiri sahihi na ya kiuhalisia ya maendeleo imezungumzwa sana. Hivyo, basi najikita kwenye Uhuru na Haki.

Kwenye Ilani hiyo ya CHADEMA, naamini msingi wa kuwa na lengo la Uhuru na Haki, ni kama lilivyoainishwa, nanukuu: Leo Tanzania inashuhudia, hususani katika Serikali ya Awamu ya Tano, vitendo vya watawala vinavyolenga kuwapunguzia wananchi “uwezo wao wa kuamua mambo yao wenyewe na
kutawala maisha yao wenyewe” na hivyo kujikuta wakilazimika kuwa sehemu ya vuguvugu la ukombozi awamu ya pili.


Kulingana na yaliyomo kwenye hiyo Ilani, na jinsi lengo hilo linavyositizwa kwenye kampeni za wagombea wao, hasa na mgombea Urais, ni wazi ukombozi awamu ya pili, siyo ukombozi wa kiuchumi. Swali, je Tanzania bado watu wake hawako huru na hawana haki? Huyu Mtanzania anakombolewa kutoka kwa nani na nani anamnyima uhuru na haki?

Ili kujibu swali la msingi la kama ni kweli Tanzania hakuna Uhuru na Haki, ni vyema kurejea kwenye Katiba ya JMT (1977). Uhuru na Haki vimeanishwa kwenye Sehemu ya Tatu ya Katiba: HAKI NA WAJIBU MUHIMU. Sehemu hii ya Katiba ina Ibara nyingi tu kuhusu:
√ Haki ya Usawa;
√ Haki ya Kuishi;
√ Haki ya Uhuru wa Mawazo;
√ Haki ya Kufanya Kazi; na
√ Masharti ya Jumla.

Kwa muktadha huo, je, ni sahihi kudai kuwa Watanzania wanahitaji ukombozi mwingine wa kudai Uhuru na Haki, au nyuma ya pazia kuna agenda zilizofichwa? Labda ni kwa sababu Rais Magufuli alipoingia madarakani alipiga marufuku siasa za majukwaani ili nguvu za Watanzania zielekezwe kwenye shughuli za maendeleo?

Jibu lolote katika maswali hayo inabidi lizingatie mahitaji ya Katiba, Ibara ya 29(1) Kila mtu katika Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kufaidi haki za msingi za binadamu, na matokeo ya kila mtu kutekeleza wajibu wake kwa jamii, kama zilivyofafanuliwa katika
ibara ya 12 hadi ya 28 za sehemu hii ya Sura hii ya Katiba
;

na

Ibara ya 30(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja
kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa
kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.


Yawezekana Ibara hizo zina mapungufu km kuminya uhuru na haki ya watu wanaotaka Uhuru usio na mipaka au Haki bila kuwajibika. Ama sivyo CHADEMA wanaimba ngonjera isiyoeleweka kwani, hata kikifanikiwa kuwa chama tawala, hakitapenda hali ya uhuru na haki katika misingi wanayodai.

Kamwe mtu maskini hatajisikia huru na haki zake mara nyingi zitabanwa na walio nacho (matajiri). Sauti ya maskini dunia kote haiwezi kusikika. Hivyo kwa sasa tunahitaji ukombozi wa kiuchumi ili kila Mtanzania aone fahari ya kuishi katika nchi hii. Ndipo hapo tu sauti ya kila Mtanzania itasikika na si vingenevyo.
 
TBC television ya taifa muda wote kumpigia kampeni jpm, na Hussein mwinyi.wapinzani hawarushwi kamwe.hii si haki
 
TBC television ya taifa muda wote kumpigia kampeni jpm, na Hussein mwinyi.wapinzani hawarushwi kamwe.hii si haki
Je, hilo ni suala la Kisera au utekelezaji? Au umesahau ni hao hao wanaohubiri Uhuru na Haki ndio waliowafukuza TBC bila aibu?
 
Uhuru na haki vitoke wapi wakati mtu anatishia wapiga kura kuwa msipompa kura mgombea wa chama changu mtajuta hamtapata maendeleo.

Mtu anaamua kutumia fedha za umma kama zake na ukijaribu kuhoji unaweza kutekwa na hata kuuwawa.

Vyombo vya habari vyote vimefungwa midomo vinatakiwa kumsifia tu Magufuli vinginevyo ni kufungiwa. Tanzania kwa sasa imekidhi vigezo vyote vya kuitwa nchi inayotawaliwa kiimla.
 
Kuwepo vipengele vinavyoongelea haki na uhuru ni kitu kimoja na Utekelezaji wake ni kitu kingine.
 
Kuwepo vipengele vinavyoongelea haki na uhuru ni kitu kimoja na Utekelezaji wake ni kitu kingine.
Ni kweli uliyoyasema. Ila tujiulize ni mazingira yapi yanaimarisha au kudumisha Uhuru/Haki ilivyo kwenye Katiba ya JMT (1977).
√ Je, ni kwa sababu ya uelewa mdogo wa jamii kuhusu Uhuru/Haki zao?
√ Je, ni ufukara wa kifikra jinsi ya kutumia fursa zilizopo za Uhuru/Haki?
√ Labda umaskini wa kipato kushindana na nguvu ya pesa ya waliyo nayo?
√ Yawezekana ni utegemezi wa mahitaji muhimu kukimu/kumudu maisha?
√ Je, iwapo kila mwananchi akiwezeshwa kiuchumi ataweza kutafsiri kwa vitendo Uhuru/Haki zake, badala ya kuhubiriwa Uhuru/Haki, ambavyo kimsingi vimeainishwa kwenye Katiba ya JMT, Sheria, Kanuni na Taratibu, ikiwa ni pamoja na Katiba za vyama mbalimbali, na kanuni za Taasisi na Mashirika?
√ Ikiwa ni hivyo ni mazingira gani ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, na kiteknolojia mwananchi awezeshwe kiuchumi?
 
Lengo kuu lililo kwenye Ilani ya CHADEMA ya Uchaguzi Mkuu, 2020 ni UHURU, HAKI NA MAENDELEO YA WATU.

Suala la tafsiri sahihi na ya kiuhalisia ya maendeleo imezungumzwa sana. Hivyo, basi najikita kwenye Uhuru na Haki.

Kwenye Ilani hiyo ya CHADEMA, naamini msingi wa kuwa na lengo la Uhuru na Haki, ni kama lilivyoainishwa, nanukuu: Leo Tanzania inashuhudia, hususani katika Serikali ya Awamu ya Tano, vitendo vya watawala vinavyolenga kuwapunguzia wananchi “uwezo wao wa kuamua mambo yao wenyewe na
kutawala maisha yao wenyewe” na hivyo kujikuta wakilazimika kuwa sehemu ya vuguvugu la ukombozi awamu ya pili.


Kulingana na yaliyomo kwenye hiyo Ilani, na jinsi lengo hilo linavyositizwa kwenye kampeni za wagombea wao, hasa na mgombea Urais, ni wazi ukombozi awamu ya pili, siyo ukombozi wa kiuchumi. Swali, je Tanzania bado watu wake hawako huru na hawana haki? Huyu Mtanzania anakombolewa kutoka kwa nani na nani anamnyima uhuru na haki?

Ili kujibu swali la msingi la kama ni kweli Tanzania hakuna Uhuru na Haki, ni vyema kurejea kwenye Katiba ya JMT (1977). Uhuru na Haki vimeanishwa kwenye Sehemu ya Tatu ya Katiba: HAKI NA WAJIBU MUHIMU. Sehemu hii ya Katiba ina Ibara nyingi tu kuhusu:
√ Haki ya Usawa;
√ Haki ya Kuishi;
√ Haki ya Uhuru wa Mawazo;
√ Haki ya Kufanya Kazi; na
√ Masharti ya Jumla.

Kwa muktadha huo, je, ni sahihi kudai kuwa Watanzania wanahitaji ukombozi mwingine wa kudai Uhuru na Haki, au nyuma ya pazia kuna agenda zilizofichwa? Labda ni kwa sababu Rais Magufuli alipoingia madarakani alipiga marufuku siasa za majukwaani ili nguvu za Watanzania zielekezwe kwenye shughuli za maendeleo?

Jibu lolote katika maswali hayo inabidi lizingatie mahitaji ya Katiba, Ibara ya 29(1) Kila mtu katika Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kufaidi haki za msingi za binadamu, na matokeo ya kila mtu kutekeleza wajibu wake kwa jamii, kama zilivyofafanuliwa katika
ibara ya 12 hadi ya 28 za sehemu hii ya Sura hii ya Katiba
;

na

Ibara ya 30(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja
kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa
kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.


Yawezekana Ibara hizo zina mapungufu km kuminya uhuru na haki ya watu wanaotaka Uhuru usio na mipaka au Haki bila kuwajibika. Ama sivyo CHADEMA wanaimba ngonjera isiyoeleweka kwani, hata kikifanikiwa kuwa chama tawala, hakitapenda hali ya uhuru na haki katika misingi wanayodai.

Kamwe mtu maskini hatajisikia huru na haki zake mara nyingi zitabanwa na walio nacho (matajiri). Sauti ya maskini dunia kote haiwezi kusikika. Hivyo kwa sasa tunahitaji ukombozi wa kiuchumi ili kila Mtanzania aone fahari ya kuishi katika nchi hii. Ndipo hapo tu sauti ya kila Mtanzania itasikika na si vingenevyo.
mwengeso unajitahidi sana kupigania chama chako. Kama unalipwa buku 7 kwa kweli unastahili. Siyo sawa na Elitwege yeye kazi kuandika "CHADEMA watapinga" eti na yeye anapewa buku 7 hapo Lumumba. Big up sana japo mambo unayoandika hayana maana kwetu ambao huu utawala umetutenda
 
mwengeso unajitahidi sana kupigania chama chako. Kama unalipwa buku 7 kwa kweli unastahili. Siyo sawa na Elitwege yeye kazi kuandika "CHADEMA watapinga" eti na yeye anapewa buku 7 hapo Lumumba. Big up sana japo mambo unayoandika hayana maana kwetu ambao huu utawala umetutenda

Asante kwa hiyo Big up lakini mimi sijawahi na sintokuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Vyama vya siasa vimejaa viongozi waotumia siasa kama ajira, wenye uchu wa madaraka na mbaya zaidi ni wajasiriamali wa kisiasa.

Kama unafuatilia michango yangu, au mada zangu, sijadili matukio au watu. Nasakama kundi la wafuasi wa upinzani, humu JF, ambao bandiko/mijadala yao ni vioja badala ya hoja. Ni kwa sababu hiyo, ni wachache wenye uwezo wa kuchangia hoja zangu.

Mfano mzuri ni hii mada ya Uhuru/Haki ambayo hata wewe ukichoweza ni kunipongeza ukimalizia na sentensi ya kukata tamaa, nanukuu unayoandika hayana maana kwetu ambao huu utawala umetutenda. Kama ungejua utawala wa sasa unaweka mazingira rafiki na ya uhakika kwa kila Mtanzania kupiga vita umaskini.

Nitatoa mfano wa mkulima. Ubora wa miundo mbinu ya usafirishaji inahamasisha kuongeza tija kwenye kilimo, na kadharika na kadharika. Lakini, badala ya wanasiasa kuhubiri fursa za maendeleo zitokanazo na ubora wa maendeleo ya vitu, wanabaki kupiga siasa za madai ya Katiba mpya, Uhuru/Haki kwa lengo la kuongeza fursa za wao kupata madaraka!!
 
kwa mfano hapa kuna uhuru gani kwenye tume ya uchaguzi?
JamiiForums2000245234.jpg
 
'Msipochagua mbunge wa CCM sileti maendeleo hapa....'

Hii ni haki kweli?.
 
Wananchi kuwa na uwezo wa kuchagua wakurugenzi, wakuu wa wilaya na mikoa.
Ni kweli uliyoyasema. Ila tujiulize ni mazingira yapi yanaimarisha au kudumisha Uhuru/Haki ilivyo kwenye Katiba ya JMT (1977).
√ Je, ni kwa sababu ya uelewa mdogo wa jamii kuhusu Uhuru/Haki zao?
√ Je, ni ufukara wa kifikra jinsi ya kutumia fursa zilizopo za Uhuru/Haki?
√ Labda umaskini wa kipato kushindana na nguvu ya pesa ya waliyo nayo?
√ Yawezekana ni utegemezi wa mahitaji muhimu kukimu/kumudu maisha?
√ Je, iwapo kila mwananchi akiwezeshwa kiuchumi ataweza kutafsiri kwa vitendo Uhuru/Haki zake, badala ya kuhubiriwa Uhuru/Haki, ambavyo kimsingi vimeainishwa kwenye Katiba ya JMT, Sheria, Kanuni na Taratibu, ikiwa ni pamoja na Katiba za vyama mbalimbali, na kanuni za Taasisi na Mashirika?
√ Ikiwa ni hivyo ni mazingira gani ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, na kiteknolojia mwananchi awezeshwe kiuchumi?
 
Wananchi kuwa na uwezo wa kuchagua wakurugenzi, wakuu wa wilaya na mikoa.
Ungefafanua zaidi mwananchi kuchagua watendaji na wakuu wa wilaya na wakati huo achague wawakilishi, inamwongezeaje uhuru/haki zake? Au mfumo wa sasa hivi una mapungufu gani hadi kuongezea mwananchi majukumu kuchagua watendaji wa shughuli za kila ambazo kimsingi ni za kitaalamu?
 
Kina Nusrat Henje waliimba "Mungu ibariki Chadema ....",wako mahabusu mpaka leo bmna kunyimwa dhamana zaidi ya miezi 3 sasa!

UVCCM waliimba "Mungu mmbariki Magufuli....",wako uraiani na hawajachukuliwa hatua yoyote!

Hapa unaweza kuona uhuru na haki nchi hii ni kulingana na matakwa ya serikali!
Ukiwa na mawazo tofauti au itikadi tofauti basi unakuwa targeted!
Mambo ya kubambikizia kesi yameshamiri sana awamu hii!

Its a shame!
 
Mfano alioutoa yesu juu ya kondoo aliepotea unaujua? Wewe haikuumi damu isiyo na hatia?
We utaokoa kondoo mmoja haraf uache mia wapotee

Hv ukiwa unaendesha basi lenye abiria 60 barabara ambay pemben kuna mashimo ghafla jamaa akajichanganya barabarani utamkwep uingie shimon uue 60 au utaua 1 sitini wapone
 
Wakuu wa wilaya ambao hawajachaguliwa na wananchi wanaweza kukuweka ndani muda wowote bila kuhofia kupoteza nafasi zao,wabunge hawana mamlaka hayo na hata wangekuwa nayo wangejiupusha kufanya hivyo.Pia Watendaji na wakuu wa wilaya wasioachaguliwa na wananchi wasipotekeleza majukumu yao yoyote ipasavyo wananchi wa eneo hilo hawana haki ya kuwaondoa.
Ungefafanua zaidi mwananchi kuchagua watendaji na wakuu wa wilaya na wakati huo achague wawakilishi, inamwongezeaje uhuru/haki zake? Au mfumo wa sasa hivi una mapungufu gani hadi kuongezea mwananchi majukumu kuchagua watendaji wa shughuli za kila ambazo kimsingi ni za kitaalamu?
 
We utaokoa kondoo mmoja haraf uache mia wapotee

Hv ukiwa unaendesha basi lenye abiria 60 barabara ambay pemben kuna mashimo ghafla jamaa akajichanganya barabarani utamkwep uingie shimon uue 60 au utaua 1 sitini wapone
nikosa gani alilofanya Ben mpaka imempasa kuuawa?
 
Back
Top Bottom