Kuna uhusiano gani wa mtu kutema Mate pale pua yake inapo kutana na harufu mbaya ya mavi/ mzoga n.k

Swizzy

JF-Expert Member
Nov 4, 2016
773
511
habari wana Jf!!!

Kumekuwepo na hii tabia ya watu kutema mate pale pua zao zinapo kutana na harufu mbaya yoyote ile iwe ya mzoga, gogo (mavi/kinyesi cha mtu mwingine), unapo kunya/ kukojoa, uchochoro ambao una nuka kwasababu ya mikojo n.k.

Tangu zamani huwa najiuliza kuna uhusiano gani wa mtu kutema mate (saliva), pale tu pua yake inapo kutana na harufu mbaya/ kuona mzoga wenye harufu kali, mavi, choo kichafu, mtu mchafu (anaye nuka).

Kwanini tuna tema mate? kuna uhusiano gani wa kutema mate na hizo harufu? Kwani usipo tema utakufa? au utaumwa? au kuna lolote linaweza kukupata usipo fanya hivyo?

Najua kitendo hichi wengi wetu tunakifanya. Sasa basi njooni tujuzane KWANINI TUNA TEMA MATE? Je kuna uhusiano wowote na sayansi ya mwili hapo?

......NJOONI TUJUZANE HAPA...
 
Tujibu kwanza ww kwamba kuna uhusiano gan wa kumeza mate na harufu nzur mfano ya pila nzur ilioungwa na binzar na kila k2!!!
Halafu jibu lake ni inversely proportiona na la swal lako
 
Tujibu kwanza ww kwamba kuna uhusiano gan wa kumeza mate na harufu nzur mfano ya pila nzur ilioungwa na binzar na kila k2!!!
Halafu jibu lake ni inversely proportiona na la swal lako
tuanze na hilo la kutema mate kwanza, hilo lako litafuata baadaye
 
Ni suala la kibaiolojia hili mkuu, usipotema mate hauumwi wala kufa

Nadhani ile harufu mtu akiinusa inaleta mchafuko ndani ya mwili na automatically mate ndio yanatoka... Tofauti na ukinusa harufu ya pilau lazima umezee mate huwezi kutema
 
Ni psychological factor.. Na inajengeka kwa watu fulani fulani mfano kuna watu wakiingia chooni kabla hajajisaidia lazima ateme mate.. Mm hyo tabia sina.. So ni tabia zaidi
 
Anakuwa na mimba
Naomba nikushauri kitu Mkuu!

Next time, kama huna la kujibu ni bora ukawa msomaji tu na si kujitoa ufahamu kwa ku-comment majibu ya hovyo.

Nilishauriwa na mtu mmoja kuwa "Kuliko utoe ushauri, majibu, maoni nk ya hovyo ni bora ukae kimya na kumuacha mlengwa katika hali ya sintofahamu kuliko kumpa jibu bovu"

Unaishusha hadhi Jamii Forums.
 
hyo sio kibaiolojia bhana mbona mm hata nikutane na harufu mbaya kias gani huwa sitemi mate, hii ni tabia ya MTU tuu
 
Naomba nikushauri kitu Mkuu!

Next time, kama huna la kujibu ni bora ukawa msomaji tu na si kujitoa ufahamu kwa ku-comment majibu ya hovyo.

Nilishauriwa na mtu mmoja kuwa "Kuliko utoe ushauri, majibu, maoni nk ya hovyo ni bora ukae kimya na kumuacha mlengwa katika hali ya sintofahamu kuliko kumpa jibu bovu"

Unaishusha hadhi Jamii Forums.
ahsante kwa kumwambia ukweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom