Nchi Kavu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 4,271
- 2,401
Tunakoelekea mambo yatakuwa moto kama Rais ataamua kusimamia yale anayoyaamini kuwa ni sahihi kwa taifa. habari za mitandao huko zinasema kuwa ziko harakati za kumkwamisha katika utekelezaji wake wa majukumu ya kila siku. Na ugumu zaidi ataupata kwenye chama chake CCM ambapo wanadai kuwa mwanamama hataweza kuhimili mikiki mikiki ya siasa za bongo kama Rais, na zaidi kama mwenyekiti wa chama.
Taifa linaisubiri kwa hamu hotuba yake ya kesho (22/04/2021) hapo Bungeni Dodoma. Hakika itakuwa ni kama ile hotuba ya Rev MLK - I have a dream. Kuanzia hapo ndio taifa litajua ni upi mwelekeo sahihi wa taifa hili kwa kipindi cha miaka minne iliyobakia. Mama kasema kuwa yeye na hayati ni kitu kimoja lakini kiuhalisia si kweli. Ni kauli za kisiasa tu zile. Yeye ni Samia. Mtazamo wake na wa hayati hauwezi kuwa sawa hata kwa asilimia 70. Hizo 30 ndizo wadau wanazisikilizia, na ndizo zenye kila kitu ambacho watanzania pengine wanataka.
Sasa katika kuenenda huko ndipo yanatokea mambo kadha ambayo kwa namna moja au nyingine yanaweza kumkwamisha Rais katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku, hasa wale wanazi wa chama tawala. Ukizingatia pia keshagusia suala la urais ifikapo 2025 ni wazi anajua kuna figisu nyingi zinaendelea huku chini. Jambo la heri ni kwamba, na sisi tumesikia ni kuwa CDF yuko nae.
Jambo lingine la kupendeza ni kwamba CHADEMA kwa wingi wao wameonyesha nia ya wazi ya kumkubali Rais wa sasa katika kutekeleza majukumu yake. Hii ni fursa njema sana kwa pande zote mbili (CDM na Rais). Pia tumesikia katika hotuba ya M'kiti Mbowe kuwa wameshamuandikia Rais barua ya kuhitaji kuonana nae ili kuona kwa pamoja tunasonga vipi mbele kama taifa hasa baada ya kipindi cha mpito cha miaka minne nyuma.
Maandishi haya yananirudisha nyuma kidogo kwa aliyekuwa Rais wa Malawi (Joyce Banda 2012 - 2014) baada ya kifo cha aliyekuwa Rais (Mutharika). Joyce aliingia madarakani kama alivyoingia Samia. Alikutana na hali ngumu ya kiuchumi hadi kuibuka kwa kashfa maarufu iliyoitwa Cash gate. Ulikuwa ni upigaji wa maana ulliofanyika kwenye serikali ambayo yeye alikuwa ni Makamu wa Rais. Hata alipokuwa akijitetea kwa wananchi baada ya kipindi cha urais kuisha, wakati wa kampeni, alikuwa akijitetea kuwa aliibua ufisadi wa kutisha Malawi. Wapinzani walidai kuwa ufisadi wote huo ulifanyika wakati yeye akiwa ni makamu wa Rais, na pengine alifaidika nao, hivyo mwisho hata uchaguzi alishindwa.
Hivyo Rais ana machaguo mawili; kuhakikisha hii ari mpya waliyo nayo watanzania inadumu hasa katika awamu yake hii na baada, au kudemka midundo ya wanazi wa chama chake.
Rais anayo backup ya kutosha toka kwa watanzania bila kujali vyama. Hata kama ndani ya chama chake kutatokea mizengwe, hana haja ya kuunda chama kingine. CDM ipo na ninaamini itampokea ikiona inafaa. Kadhalika Rais anao uwezo wa kubakia ndani ya chama chake akakubaliana na matakwa ya wanazi na hatimaye muda wake ukiisha, aidha urais ubakie huko CCM lakini kwa m-ccm mwingine, au urais uhamie upinzani, hasa tukichukulia mfano wa Malawi.
Yote kwa yote tunamwombea Rais ulinzi kwa Mungu na ulinzi toka taasisi imara na zenye uadilifu. Afanye kazi zake kwa weledi akishirikisha washauri wake pamoja na mawazo ya watanzania pale anapoona inafaa.
Taifa linaisubiri kwa hamu hotuba yake ya kesho (22/04/2021) hapo Bungeni Dodoma. Hakika itakuwa ni kama ile hotuba ya Rev MLK - I have a dream. Kuanzia hapo ndio taifa litajua ni upi mwelekeo sahihi wa taifa hili kwa kipindi cha miaka minne iliyobakia. Mama kasema kuwa yeye na hayati ni kitu kimoja lakini kiuhalisia si kweli. Ni kauli za kisiasa tu zile. Yeye ni Samia. Mtazamo wake na wa hayati hauwezi kuwa sawa hata kwa asilimia 70. Hizo 30 ndizo wadau wanazisikilizia, na ndizo zenye kila kitu ambacho watanzania pengine wanataka.
Sasa katika kuenenda huko ndipo yanatokea mambo kadha ambayo kwa namna moja au nyingine yanaweza kumkwamisha Rais katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku, hasa wale wanazi wa chama tawala. Ukizingatia pia keshagusia suala la urais ifikapo 2025 ni wazi anajua kuna figisu nyingi zinaendelea huku chini. Jambo la heri ni kwamba, na sisi tumesikia ni kuwa CDF yuko nae.
Jambo lingine la kupendeza ni kwamba CHADEMA kwa wingi wao wameonyesha nia ya wazi ya kumkubali Rais wa sasa katika kutekeleza majukumu yake. Hii ni fursa njema sana kwa pande zote mbili (CDM na Rais). Pia tumesikia katika hotuba ya M'kiti Mbowe kuwa wameshamuandikia Rais barua ya kuhitaji kuonana nae ili kuona kwa pamoja tunasonga vipi mbele kama taifa hasa baada ya kipindi cha mpito cha miaka minne nyuma.
Maandishi haya yananirudisha nyuma kidogo kwa aliyekuwa Rais wa Malawi (Joyce Banda 2012 - 2014) baada ya kifo cha aliyekuwa Rais (Mutharika). Joyce aliingia madarakani kama alivyoingia Samia. Alikutana na hali ngumu ya kiuchumi hadi kuibuka kwa kashfa maarufu iliyoitwa Cash gate. Ulikuwa ni upigaji wa maana ulliofanyika kwenye serikali ambayo yeye alikuwa ni Makamu wa Rais. Hata alipokuwa akijitetea kwa wananchi baada ya kipindi cha urais kuisha, wakati wa kampeni, alikuwa akijitetea kuwa aliibua ufisadi wa kutisha Malawi. Wapinzani walidai kuwa ufisadi wote huo ulifanyika wakati yeye akiwa ni makamu wa Rais, na pengine alifaidika nao, hivyo mwisho hata uchaguzi alishindwa.
Hivyo Rais ana machaguo mawili; kuhakikisha hii ari mpya waliyo nayo watanzania inadumu hasa katika awamu yake hii na baada, au kudemka midundo ya wanazi wa chama chake.
Rais anayo backup ya kutosha toka kwa watanzania bila kujali vyama. Hata kama ndani ya chama chake kutatokea mizengwe, hana haja ya kuunda chama kingine. CDM ipo na ninaamini itampokea ikiona inafaa. Kadhalika Rais anao uwezo wa kubakia ndani ya chama chake akakubaliana na matakwa ya wanazi na hatimaye muda wake ukiisha, aidha urais ubakie huko CCM lakini kwa m-ccm mwingine, au urais uhamie upinzani, hasa tukichukulia mfano wa Malawi.
Yote kwa yote tunamwombea Rais ulinzi kwa Mungu na ulinzi toka taasisi imara na zenye uadilifu. Afanye kazi zake kwa weledi akishirikisha washauri wake pamoja na mawazo ya watanzania pale anapoona inafaa.