Kuna ubaya gani Zanzibar ikajitenga na kuwa huru kama Zamani?

Kama hivyo ndivyo ilivyo basi tambua haya:

  1. Muungao haukuletwa na Chama cha Mapinduzi au Kijani kibichi as on your words (1964 ASP ndiyo iliridhia huko visiwani kwa kuona manufaa ya Kuunganisha nchi.
  2. ASP imekuwepo Visiwani kama chama Tawala, Chini ya Serikali huru ya Mapinduzi ya Zaanzibar mpaka 1977 iliporidhia tena kuungana na TANU kwa bara ili kupata Chama kimoja ambacho kwa heshima ya kuendelea kuyaenzi kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi kwa huko Zanzibar chama mpaka hivi sasa kinaitwa "CHAMA CHA MAPINDUZI"
  3. Muungano haujaiondolea Zanzibar maamuzi ya kiserikali na utawala na wala hakuna popote hilo katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Labda tuseme imeondoa mamlaka ya kuwa na Serikali ya Tanganyika na Taifa la Tangayika).
  4. Yale ambayo yanatajwa kwenye "Artcles of Union" na Katiba ya Jamhuri ya Muungano kuwa ni mambo ya Muungano ni yale ambayo ASP iliyaona yanastahili kuwa hivyo na kuyaweka chini ya mashirikinao ya pamoja ya Serikali ya Jamhuri (hakukuwa na shinikizo lolote).
  5. Uzanzibar upo na utaendelea kuwepo Kikatiba kwa maana ya kuwepo kwa Mkoa huru na Serikali huru ya Mapinduzi ya Zanzibar. Hata hivyo, kwa kuwa Uzanzibar kama ulivyo "Uchaga", Unyamwezi, nk sio "Urai" kwa mujibu wa "Mambo ya Muungano, huwezi kutambulika hivyo kimataifa kuwa "WEWE NI MZANZIBARI" bali ni "MTANZANIA MWENYE ASILI YA ZANZIBARI"....

Btw hizo the so called ARTICLES of UNION mmezificha wapi?

nakumbuka kuna jamaa walienda Mahakamani kuzidai halafu JIIIIIII!!!!!
 
Swali la Zanzibar kujitenga naona halina mantiki/tija yeyote, sana sana nahofia itakuza instability characterizing small island nations-Mfano Haiti,Ngazija.Malagasy etc.

Mbona unataja mifano kidogo au ndio unakimbia hoja?...New Zealand,Jamaica,Seashells etc etc...hoja yako haina mshiko kuwa visiwa vyote vilivyokuwa ni mataifa kamili basi vinakuwa na instability...very very poor point.

Probably solution ya kumanage diversity na vi difference vidogogo ni some form of federation kati ya Tanganyika na Zanzibar au with the wider East Africa Region.Tuache mitazamo finyu na self deafeating attitudes/We must be students of philosophy of optimism /i.e everything is for the best in this best of all posssible worlds.We only need to improve on what we got.
Watu wote wenye muda na resources za kudumisha muungano wako na hali nzuri kiuchumi na maendeleo.Na nimejibu hii hoja vizuri tuu katika post iliyopita, kuwa Tanganyika na Zanzibar ni nchi miongozi mwa nchi fukara au masikini duniani.

Sasa unapokuwa na limitation ya resources inabidi ufanye priority kipi ni muhimu kuliko chengine.Matatizo na complexity ya kuunganisha nchi si jambo lenye high priority (japokuwa ni jambo muhimu)...inabidi JK adili na jinsi ya kupata chakula kwanza tusije kufa njaa, au unataka adili na matatizo ya muungano halafu tunakumbwa na ukame?:rolleyes:
 
Kwenye hili namkumbuka Mwl Nyerere. Alisema Zanzibar ikijitenga (kwa uroho wa madaraka wa viongozi wake), haitakaa salama. Baada ya kujitenga wazanzibari hawatajiona wazanzibari tene kutekuwa na 'wazanzibari' na 'wazanzibara'. Vivyo hivyo kwa 'Tanganyika' (wakijitenga watagundua kuwa wao siyop wamoja bali kuna makabila mabalimbali). Kwa mujibu wa Mwl, kujitenga ni 'dhambi' aliyoilinganisha kama kula nyama ya mtu.

Lakini mimi binafsi ningependela zaidi suala hili litatuliwe kwa referendum. Waulizwe wa zanzibari wote na wabara wote kama wanataka muungano ama la. Kama wanataka muungano, je ni aina gani ya muungano wanayoitaka (serikali moja, mbili, tatu ama 'nne'!)? Ili kupata uamuzi wa pamoja, ni lazima uamuzi uwe popular pande zote mbili.
 
Optimistic inakuja tu pale inapokuwa we are at the same level of understanding. Ishu inakuja vipi zanzibar whenever someone ask the identity of zanzibar kuna mtu anakuja na negative views za eti haiwezekani wao kujitawala kwasababu eti watabaguana (to me this is a narrow view) cha msingi kwanza watoe demokrasia kwa zanzibar ipatikane serikali iliyochaguliwa na wananchi (na sio CCM Butiama au CCM dodoma). Pili ikishachaguliwa serikali ya wananchi mawazo ya wananchi yatawakilishwa na waliowachagua na hapo ndipo tutapata solution ya muungano. Otherwise mie nadhani wazanzibari wana haki ya kudai nchi yao na sie tukabakia na Tanganyika yetu.
well said bro. humu watu huwa wanaongelea sana historia lakini wanasahau kwamba katika historia zanzibar iliendelea bila ya tanganyika na kinyume chake ilirudi nyuma baada ya kuungana na tanganyika, hususan baada ya kuunganisha vyama.
 
Kama hivyo ndivyo ilivyo basi tambua haya:

  1. Muungano wa Srertikali ya Jamhuri ya Watu wa Tanganyika na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar haukuletwa na Chama cha Mapinduzi au Kijani kibichi as on your words. Mwaka 1964, Chama kilichofanya mapinduzi kwa Upande wa Zaanzibar (ASP) ndiyo kilichoridhia kuungana na Tanzanyika kwa kuona manufaa ya Kuunganisha nchi.

  1. ASP imekuwepo Visiwani kama chama Tawala, chini ya Serikali huru ya Mapinduzi ya Zanzibar mpaka 1977 iliporidhia tena kuungana na TANU kwa upande wa bara ili kupata Chama kimoja ambacho kwa heshima kubwa ya kuendelea kuyaenzi Mapinduzi yaliyoletea uhuru kwa wa Zanzibar, chama hicho kikaitwa "CHAMA CHA MAPINDUZI" . Ikumbukwe kuwa Bara hakukuwa na Mapinduzi, hivyo hata jina la chama lingewezwa kupingwa na waasisi wa chama hicho.
  2. Muungano haujaiondolea Zanzibar maamuzi ya kiserikali na utawala na wala hakuna popote hilo katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Labda tuseme imeondoa mamlaka ya kuwa na Serikali ya Tanganyika na Taifa la Tanganyika).
  3. Yale ambayo yanatajwa kwenye "Artcles of Union" na Katiba ya Jamhuri ya Muungano kuwa ni mambo ya Muungano ni yale ambayo ASP iliyaona yanastahili kuwa hivyo na kuyaweka chini ya mashirikinao ya pamoja ya Serikali ya Jamhuri (hakukuwa na shinikizo lolote).
  4. Uzanzibar upo na utaendelea kuwepo Kikatiba kwa maana ya kuwepo kwa Mkoa huru na Serikali huru ya Mapinduzi ya Zanzibar. Hata hivyo, kwa kuwa Uzanzibar kama ulivyo "Uchaga", Unyamwezi, nk sio "Urai" kwa mujibu wa "Mambo ya Muungano, huwezi kutambulika hivyo kimataifa kuwa "WEWE NI MZANZIBARI" bali ni "MTANZANIA MWENYE ASILI YA ZANZIBARI"....

Ni nani asiejua kama ASP haikuwa na 100% support visiwani Zanzibar?...tatizo lako unafananisha TANU na ASP.TANU ni chama kilichokubalika Tanganyika yote...kwa Zanzibar ASP haikukubalika, ni chama kilichokuwa na wafuasi 54% kwa mujibu wa kura ya 1963....jee ASP inawakilisha matakwa ya wazanzibari, wakati kilishindwa kuwapatia wazanzibari uhuru kutoka kwa wakoloni na kulazimika kutumia mgongo wa Bara kuingia madarakani kwa chinja-chinja i.e Mapinduzi?

Sasa hoja yako ya ASP kuridhia Muungano haiwezi kuwa valid na wala haina mashikilio.
 
Bila ya mgongo wa Bara ASP isingeingia madarakani na ndio hivyo hivyo ilivyo sasa kwa CCM kuweza kuongoza Zanzibar ni lazima upatikane mgongo au mkono wa Dodoma/Butiama na kusaidiwa kidogo na JWTZ.

Ukiondoa hivyo maamuzi ya wazanzibari utayaona kwa macho yako bila ya kutumia tochi :D
 
Kwenye hili namkumbuka Mwl Nyerere. Alisema Zanzibar ikijitenga (kwa uroho wa madaraka wa viongozi wake), haitakaa salama. Baada ya kujitenga wazanzibari hawatajiona wazanzibari tene kutekuwa na 'wazanzibari' na 'wazanzibara'. Vivyo hivyo kwa 'Tanganyika' (wakijitenga watagundua kuwa wao siyop wamoja bali kuna makabila mabalimbali). Kwa mujibu wa Mwl, kujitenga ni 'dhambi' aliyoilinganisha kama kula nyama ya mtu.

Lakini mimi binafsi ningependela zaidi suala hili litatuliwe kwa referendum. Waulizwe wa zanzibari wote na wabara wote kama wanataka muungano ama la. Kama wanataka muungano, je ni aina gani ya muungano wanayoitaka (serikali moja, mbili, tatu ama 'nne'!)? Ili kupata uamuzi wa pamoja, ni lazima uamuzi uwe popular pande zote mbili.
hizi siasa za woga alizotunywesha nyerere ndio mpaka leo zinazotudhuru.Rwanda wanayakabili mambo na wanatuacha nyuma ,sisi ndo kwanza tunamhubiri nyerere.Hivi wadanganyika ni lini mtaondoa woga katika kukabili hali halisi?, no wonder CCM haitokuwa na upinzani maisha tanzania bara. watu hata kuwapigia kura wapinzani wanaogopa kwasababu nyerere alikuwa CCM.
 
hizi siasa za woga alizotunywesha nyerere ndio mpaka leo zinazotudhuru.

Lakini, hudhani alichosema Mwl kuhusu possibility ya Zanzibar kugawanyika (Unguja, Pemba!) endapo itajitenga na bara kina mantiki? Maana nje ya muungano hakutakuwa na 'wazanzibari', probably kutakuwa na 'waunguja' na 'wapemba'! Naona kuna mantiki kwa kiasi fulani hapa.
 
Mimi ni mzanzibari na wala moyoni kwangu sijawahi kujitambulisha kama mtanzania....:D


Be specific, wewe ni mpemba au Muunguja because outside the union there is so such thing as Zanzibar, there is Pemba and Unguja period. The only thing that unite Wazanzibari momentarily is their hatred towards mainlanders. Once they achieve to dismantle the union , Wazanzibari are not going to stop there !
 
Be specific, wewe ni mpemba au Muunguja because outside the union there is so such thing as Zanzibar, there is Pemba and Unguja period. The only thing that unite Wazanzibari momentarily is their hatred towards mainlanders. Once they achieve to dismantle the union , Wazanzibari are not going to stop there !

Hizi ni story zisizo na mshiko...pengine jiulize taifa la watu wa Zanzibar lilikuwepo kwa muda gani au limezaliwa lini?

Zanzibar kama jamhuri ni moja ya mataifa makongwe barani Afrika...na lipo kwa karne nyingi sana, kongwe zaidi hata hilo taifa la Tanganyika.

Sasa unaposema kuwa Zanzibar haiwezi kuwepo watabaguana....mimi sikufahamu.

Aidha kwa suali lako kama unataka mimi niwe specific kama ni muunguja au mpemba basi formation ya damu ni kama ifuatavyo (50% black/Unguja + 25% Oman + 25% black/Pemba).Yaani wazee wangu wawili mmoja anatoka Unguja (pure black)....na mwengine anatoka kisiwani Pemba akiwa 50-50 na muarabu wa Oman.

Sasa mie mwenyewe nashindwa kuwa specific naomba msaada kutoka kwako :D
 
Lakini, hudhani alichosema Mwl kuhusu possibility ya Zanzibar kugawanyika (Unguja, Pemba!) endapo itajitenga na bara kina mantiki? Maana nje ya muungano hakutakuwa na 'wazanzibari', probably kutakuwa na 'waunguja' na 'wapemba'! Naona kuna mantiki kwa kiasi fulani hapa.
nimefurahi kwamba umeiita hiyo ni "possibility" lakini pia usisahau kwamba possibility ni neno la two sided coin, what kama nikienda against na nyerere na nikasema kuna possibility wazanzibari wakawa more united nje ya muungano? will i be wrong?, umefika wakati tuamue kile tunachohisi ni right bila kujali nani kasema nini!, kama mtu ni mbaguzi hata tukiliunganisha bara zima la afrika basi atabaki kuwa mbaguzi tu, ubaguzi umo ndani ya damu ya mtu na sio ndani au nje ya muungano.
 
Ni nani asiejua kama ASP haikuwa na 100% support visiwani Zanzibar?...tatizo lako unafananisha TANU na ASP.TANU ni chama kilichokubalika Tanganyika yote...kwa Zanzibar ASP haikukubalika, ni chama kilichokuwa na wafuasi 54% kwa mujibu wa kura ya 1963....jee ASP inawakilisha matakwa ya wazanzibari, wakati kilishindwa kuwapatia wazanzibari uhuru kutoka kwa wakoloni na kulazimika kutumia mgongo wa Bara kuingia madarakani kwa chinja-chinja i.e Mapinduzi?

Sasa hoja yako ya ASP kuridhia Muungano haiwezi kuwa valid na wala haina mashikilio.

MrFroasty,

Napata Kigugumizi hapa, Watanganyika wanajua mpaka kesho kuwa ASP ni chama cha kizalendo kwa huko visiwani na ndicho kilicholeta mapinduzi. ASP imekuwepo tokea mapinduzi mpaka ilipoungana na TANU 1977 na kufanya CCM. Hapa unataka kusema mpaka kipindi hicho ilikuwa haikubaliki Zanzibar? na nani alikuwa haikubali?

Unaweza kuona tofauti hapa, Muungano wa Tanganyika na Zaanzaibar una sura mbili, ya Kishaeria (Makubalinao ya Muungano au "Article of Union) ambayo badae yaliwekwewa Katiba (Katiba za Mpito na ile ya 1977) na pia Kuna muungano wa Vyama (TANU na ASP) ambayo kwa mujibu wa mfumo wa Utawala, chama ndio Serikali,

Unaweza kuona tofauti kubwa tena hapa, Kisiasa, Raisi wa Zanzibar ni Makamu Mwenyekiti Mwenza wa Chama Tawala (CCM) lakini Kiserikali ni Mtawala Mkuu wa Serikali ya Zanzibar Mwenye maamuzi Makubwa kwani analindwa na Katiba (Katiba ya Jamhuri ya Muungano, 1977 na Katiba ya Zanzibar, 1984). Ukichukulia majadilinao yaliyokuwa yanafanyika/kuendelea kuhusu muafaka ambayo yana athari pia kwenye Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano kuhusu Muundo wa Serikali, unastaajabu kuona Seif Sharif ambae ni Katibu Mkuu wa CUF (Bara na Visiwani) ndie amekuwa akijadiliana na Dr. A.A Karume (Makamu Mwenyekiti wa Chama tawala ) kuhusu muundo wa Serikali na mausala mengineyo na sio Dr. Lipumba (M/Kiti wa CUF (bara na Visiwani) wala Dr. J.K.Kikwete Mwenyekiti wa CCM au Kapt. Yusufu Makamba Katibu wa CCM (bara na Visiwani ).
 
Aidha kwa suali lako kama unataka mimi niwe specific kama ni muunguja au mpemba basi formation ya damu ni kama ifuatavyo (50% black/Unguja + 25% Oman + 25% black/Pemba).Yaani wazee wangu wawili mmoja anatoka Unguja (pure black)....na mwengine anatoka kisiwani Pemba akiwa 50-50 na muarabu wa Oman.

Sasa mie mwenyewe nashindwa kuwa specific naomba msaada kutoka kwako :D

Lakini kwa hoja hiyohiyo, huoni kuwa kwa sasa kuna 'watanzania' ambao hawawezi kujibainisha kuwa ni 'wazanzibari' au 'watanganyika'?
 
Hizi ni story zisizo na mshiko...pengine jiulize taifa la watu wa Zanzibar lilikuwepo kwa muda gani au limezaliwa lini?

Zanzibar kama jamhuri ni moja ya mataifa makongwe barani Afrika...na lipo kwa karne nyingi sana, kongwe zaidi hata hilo taifa la Tanganyika.

Sasa unaposema kuwa Zanzibar haiwezi kuwepo watabaguana....mimi sikufahamu.

Aidha kwa suali lako kama unataka mimi niwe specific kama ni muunguja au mpemba basi formation ya damu ni kama ifuatavyo (50% black/Unguja + 25% Oman + 25% black/Pemba).Yaani wazee wangu wawili mmoja anatoka Unguja (pure black)....na mwengine anatoka kisiwani Pemba akiwa 50-50 na muarabu wa Oman.

Sasa mie mwenyewe nashindwa kuwa specific naomba msaada kutoka kwako :D

Good huo unaitwa mchanganyiko kama mimi:
(15%/Black/Unguja+35%Mbongo+10%Mjerumani+5%Myemen+15%ComoroIslands)

Sasa sijui nijiite vipi
 
Mbona unataja mifano kidogo au ndio unakimbia hoja?...New Zealand,Jamaica,Seashells etc etc...hoja yako haina mshiko kuwa visiwa vyote vilivyokuwa ni mataifa kamili basi vinakuwa na instability...very very poor point.


Watu wote wenye muda na resources za kudumisha muungano wako na hali nzuri kiuchumi na maendeleo.Na nimejibu hii hoja vizuri tuu katika post iliyopita, kuwa Tanganyika na Zanzibar ni nchi miongozi mwa nchi fukara au masikini duniani.

Sasa unapokuwa na limitation ya resources inabidi ufanye priority kipi ni muhimu kuliko chengine.Matatizo na complexity ya kuunganisha nchi si jambo lenye high priority (japokuwa ni jambo muhimu)...inabidi JK adili na jinsi ya kupata chakula kwanza tusije kufa njaa, au unataka adili na matatizo ya muungano halafu tunakumbwa na ukame?:rolleyes:
Mfano East Timor tangu Uhuru/Kujitenga 2005 vurugu mtindo mmoja.

In April 2006, riots broke out in Dili following rivalry within the military and police; 40 people were killed and over 20,000 fled their homes. Fighting between pro-government troops and disaffected Falintil troops broke out in May 2006.[23] Upon the invitation of the Prime Minister, Australia, Malaysia, New Zealand, and Portugal sent troops to Timor, attempting to quell the violence.[24] On 26 June, Prime Minister Mari Alkatiri resigned as Prime Minister, following an ultimatum from President Xanana Gusmão that he would resign if Alkatiri did not.[25] José Ramos-Horta was appointed as Alkatiri's successor on July 8, 2006.[26] In April 2007, Gusmão declined another presidential term. In the build-up to the April 2007 presidential elections there were renewed outbreaks of violence in February and March 2007. José Ramos-Horta was inaugurated as [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/President_of_East_Timor"]President[/ame] on May 20, 2007, following his election win in the second round.[27] Gusmão was sworn in as Prime Minister on August 8, 2007. President Ramos-Horta was critically injured in [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/2008_East_Timor_coup_attempt"]an assassination attempt[/ame] on February 11, 2008, in a failed coup apparently perpetrated by [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Alfredo_Reinado"]Alfredo Reinado[/ame], a renegade soldier who died in the attack. Prime Minister Gusmão also faced gunfire separately but escaped unharmed. The Australian government immediately sent reinforcements to East Timor to keep order.[28]

Mara general Makame,kesho Captain Barhani Mungu tu epushe.
 
Mfano East Timor tangu Uhuru/Kujitenga 2005 vurugu mtindo mmoja.

Kama hiyo ndio hoja yako..think again.Zanzibar tuna riots kila siku na muungano upo na pengine ndio huo unaeleta riots.

Get your points straight b4 presenting them to us...pls do so :rolleyes:
 
Lakini kwa hoja hiyohiyo, huoni kuwa kwa sasa kuna 'watanzania' ambao hawawezi kujibainisha kuwa ni 'wazanzibari' au 'watanganyika'?

Zanzibar kuna mchanganyiko wa kila aina...tunao wanyamwezi, wamakonde, wahindi, waarabu, wazanzibari halisia (kwa maana hawana asili ya sehemu nyengine), washirazi...na wengineo nisio wajua.

Hawa wote ni wazanzibari...sifikirii kama kuvunja muungano manaake ni ugomvi na vita vya kuwa lazima Zanzibar kuwepo wazanzibari halisia pekee.Maana hii imeshindikana hata kwa wamasai huko kwenye border na Kenya.

Muungano unavunjika na kunakuja suala zima la wananchi waliochanganya damu kufanya maamuzi ya uraia gani watakao pendelea kuchukua.Hakuna nchi yenye watu wa aina au asili moja duniani...hili ni suala la kawaida ambalo naona nyie ndio munachanganya story baina ya kuwepo kwa Zanzibar huria na jinsia au asili za watu.

Kwa hiyo hili suala la kuvunja muungano tunazungumzia utenganisho wa kitaifa tuu...sio utenganisho wa watu na jinsia zao kama munavyojaribu kuweka hoja hiyo.
 
Back
Top Bottom