Kuna tukio la kishirikina liliwahi kunitokea miaka kama 20 iliyopita na limebadilisha maisha yangu

Labda unalosema ni kweli lakini kwa nini umekuja na conclusion hiyo na siyo ya kwangu? Nilikuwa bwa mdogo sana kufikiria lolote wakati ule. Tukio nililisahau au sikuliweka katika mawazo yangu kabisa mpaka baadae miaka ikapita ndiyo nikagundua kuna vitu vinavyoshabihiana vinajirudiarudia.
Mambo gani yanayoshabihiana na kujirudiarudia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaribu kuwaona na kuwaeleza yanayokusibu kifikra, wataalamu wa Masuala ya afya ya akili na saikoloji.
Wanawezavkukupa amani unayotaka kuhakikishiwa juu ya maisha yako.
Mpaka leo kukumbuka baibui, je unakumbuka abiria wengine walivaa nini?
Pengine ulimtolea macho mpaka mwenyewe akagutuka, na kutaka kukutanabahi kwamba, ' acha kunitolea macho', ndio akakugusa machoni, kutenda ambacho sio cha kawaida na hukukitegemea. Ndio ikakufanya uzidi kuchanganyikiwa zaidi. Yaliyofuata baada ya hapo, nina imani wataalamu watakusaidia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vua uhoga na dhana dhaifu,mabadiliko yako kwako mwenyewe
Hawa wanaokejeli ndio wachawi wenyewe ,wewe unaposema uchawi haupo unataka kutuaminishisha shetani hayupo?Ili muendelee kuroga watu vizuri. Misingi ya dini zote ni kumpinga shetani.Mtu mzima kufikia kuleta uzi hapa ujue amepambana alivyoweza imeshindikana.
Washirikina wengi wanatumia nyota za watu kujipatia mafanikio.
Ndugu mleta mada endelea kuomba,shirikisha watu unaowaamini muombe pamoja,mmoja hufukuza maelfu ,wawili hufukuza makumi elfu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una maana huyo mchawi alikuroga wewe na familia yako? You're being delusional mkuu, usitafute mchawi wakumpa lawama sababu uchawi wenyewe haupo pambana.
Ninyi ndo wachawi wenyewe una uhakika uchawi haupo uko dunia gani? Acha uchawi Mungu anakuona.
 
Kama hujawahi kulogwa usicomment. Maisha yana tiba mbalimbali usidanganywe nenda kwa waganga pia nyumba za Ibada bora usiende kwa nia ya kudhuru mtu. Wote ni wa Mungu. Tumedanganywa na wazungu kwa maslahi yao.
 
kijana nenda kwa watu wa saikolojia wakakutibue uwe sawa naona unalaumu kila kitu... nadhani huo urefu wa story yako ndo changamoto ya maisha yako, kuna muda wa ku focas mbele.. mbali...
 
Kama hujawahi kulogwa usicomment. Maisha yana tiba mbalimbali usidanganywe nenda kwa waganga pia nyumba za Ibada bora usiende kwa nia ya kudhuru mtu. Wote ni wa Mungu. Tumedanganywa na wazungu kwa maslahi yao.
Hivi katk hiyo story umeona proof ya yeye kurogwa? Watu hawakatai kama hakuna uchawi, ila kwa alichojielezea yeye uchawi hauonekani. Hiyo taaluma ina misingi yake mkuu, Haiendi kwa hisia tu.
YAANI KAMA KAROGWA SIYO KATIKA TUKIO HILO. Kwanza aeleze vizuri aliachaje shule.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi katk hiyo story umeona proof ya yeye kurogwa? Watu hawakatai kama hakuna uchawi, ila kwa alichojielezea yeye uchawi hauonekani. Hiyo taaluma ina misingi yake mkuu, Haiendi kwa hisia tu.
YAANI KAMA KAROGWA SIYO KATIKA TUKIO HILO. Kwanza aeleze vizuri aliachaje shule.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unasema hivyo kwasababu tukio limehusisha baibui? Wakati watu wa vazi hilo ndio wenyewe kwa yale mambo. Acheni ujinga kuna tatizo hapo na msaada unahitajika. Ndugu nenda kwenye maombi ya watumishi wa Mungu aliye hai, YESU KRISTO na utapona kabisa.
 
Unasema hivyo kwasababu tukio limehusisha baibui? Wakati watu wa vazi hilo ndio wenyewe kwa yale mambo. Acheni ujinga kuna tatizo hapo na msaada unahitajika. Ndugu nenda kwenye maombi ya watumishi wa Mungu aliye hai, YESU KRISTO na utapona kabisa.
Unajua ukiumwa ukaenda hospitali hushangaaji dr ana kukuuliza maswali ambayo kwa kawaida unawza kuona hayana uhusiano na ugonjwa wako? Mfano unaishi wapi? Unafanya kazi gani? Mara ya mwisho umekula nini? Unatumia mafuta gani ? Umeolewa? Una mpnz?
Ulishajiuliza niini msingi wa hayo maswali with relation na ugonjwa wako?
Sasa yeye mhanga wa baibui haya na hao ndugu zake huko nyumbani ambao ni wakubwa kuliko yeye? Nao walipitiwa na baibui?
Muulize vizuri akuelezee maisha ya familia yao kabla ya kuzaliwa kwake, kisha akuelezee maisha yako toka alivyo darsa la kwanza. Akupe maisha toka anaanza chuo na mahusiano. Yachanganua kisha utaona tatizo la mshikaji.
TATIZO LAKE LIKPO KICHWANI MWAKE YEYE MWENYEWE. HAJAROGWA.
Uchawi una kikomo cha muda kwanza ujue.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabibi na Mabwana wa JF,

Naandika uzi huu hii ikiwa mara ya kwanza kabisa mimi kushare habari hii mahali popote. Sijawahi kumwambia mtu, hata familia yangu haijui kuhusu hili.

Nalileta kwenu kwa sababu nimenuia kabisa hili suala lazima nilitatue mwaka huu. Najaribu kuendelea kutambua watu ambao wanaweza kunisaidia kwa sababu nguvu inayonishikilia naona inaendelea kukaza kamba kweli kweli yaani siyo utani.

Kiufupi, kuna siku moja nikiwa kijana mdogo nilikuwa napanda basi wakati naelekea kukaa kwenye siti njiani nikapishana na mtu mmoja amevaa baibui jeusi amejifunika hadi usoni. Ilikuwa ni hapa hapa Dar es Salaam. Nakumbuka hadi kituo nilichokuwa nimepanda. Wakati napishana naye akaniwekea vidole machoni. Mimi nikapata kama bumbuazi fulani hivi yeye nadhani akashuka.

Kiufupi, maisha yangu hayajawa sawa toka wakati huo. Mimi ni mtu mwenye uwezo sana kiakili ila hata chuo niliishia katikati tena GPA yangu ikiwa ya juu. Wenzangu wamesogea sana na wengine wanaitwa waheshimiwa sasa hivi wakati mimi nimekuwa mtu ambaye hata nijaribu vipi niko pale pale. Na hata familia yangu kiujumla ukianzia kaka na dada zangu wana hali fulani ya kuhangaika tu wote. Tungeweza kufanya mambo makubwa binafsi na hata pamoja ila hakuna tunaloweza kuonyesha mpaka sasa.

Story yangu ni ndefu sana na nimepitia mengi mno nisingependa kuyaelezea hapa.

Kuna wakati tukio hili huwa linaondoka kwenye fikra zangu ila kuna wakati vitu fulani vinatokea mfululizo halafu nakumbuka siku ile.

Mimi ni mtu wa maombi, najaribu sana kuwa hivyo. Sijakata tamaa na sitakata tamaa, lakini najiulizaga nitasubiri mpaka lini?

Naomba ushauri tafadhali. Hali yangu lazima ibadilike sasa hivi.
Mtoa mada yaani mtu akutie vidole machoni unamwangalia tu!
Ingekuwa mimi ndani ya dakika 2 hana meno yote ya mbele

Sent by Diaspora
 
Unajua ukiumwa ukaenda hospitali hushangaaji dr ana kukuuliza maswali ambayo kwa kawaida unawza kuona hayana uhusiano na ugonjwa wako? Mfano unaishi wapi? Unafanya kazi gani? Mara ya mwisho umekula nini? Unatumia mafuta gani ? Umeolewa? Una mpnz?
Ulishajiuliza niini msingi wa hayo maswali with relation na ugonjwa wako?
Sasa yeye mhanga wa baibui haya na hao ndugu zake huko nyumbani ambao ni wakubwa kuliko yeye? Nao walipitiwa na baibui?
Muulize vizuri akuelezee maisha ya familia yao kabla ya kuzaliwa kwake, kisha akuelezee maisha yako toka alivyo darsa la kwanza. Akupe maisha toka anaanza chuo na mahusiano. Yachanganua kisha utaona tatizo la mshikaji.
TATIZO LAKE LIKPO KICHWANI MWAKE YEYE MWENYEWE. HAJAROGWA.
Uchawi una kikomo cha muda kwanza ujue.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa umenena mkuu, nyie ndio mnatakiwa katika jamii na kuonesha mmekomaa kiakili kuliko hao wengine wanakuja kwa kejeli kusema mleta mada ni muongo... Ulichosema ni sahihi kabisa, sometimes mtu anahisi amerogwa kisa mambo hayaendi na familia imevurugika ila kumbe tatizo hata sio kulogwa ni mfumo wao mbovu wa uendeshaji wa maisha yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabibi na Mabwana wa JF,

Naandika uzi huu hii ikiwa mara ya kwanza kabisa mimi kushare habari hii mahali popote. Sijawahi kumwambia mtu, hata familia yangu haijui kuhusu hili.

Nalileta kwenu kwa sababu nimenuia kabisa hili suala lazima nilitatue mwaka huu. Najaribu kuendelea kutambua watu ambao wanaweza kunisaidia kwa sababu nguvu inayonishikilia naona inaendelea kukaza kamba kweli kweli yaani siyo utani.

Kiufupi, kuna siku moja nikiwa kijana mdogo nilikuwa napanda basi wakati naelekea kukaa kwenye siti njiani nikapishana na mtu mmoja amevaa baibui jeusi amejifunika hadi usoni. Ilikuwa ni hapa hapa Dar es Salaam. Nakumbuka hadi kituo nilichokuwa nimepanda. Wakati napishana naye akaniwekea vidole machoni. Mimi nikapata kama bumbuazi fulani hivi yeye nadhani akashuka.

Kiufupi, maisha yangu hayajawa sawa toka wakati huo. Mimi ni mtu mwenye uwezo sana kiakili ila hata chuo niliishia katikati tena GPA yangu ikiwa ya juu. Wenzangu wamesogea sana na wengine wanaitwa waheshimiwa sasa hivi wakati mimi nimekuwa mtu ambaye hata nijaribu vipi niko pale pale. Na hata familia yangu kiujumla ukianzia kaka na dada zangu wana hali fulani ya kuhangaika tu wote. Tungeweza kufanya mambo makubwa binafsi na hata pamoja ila hakuna tunaloweza kuonyesha mpaka sasa.

Story yangu ni ndefu sana na nimepitia mengi mno nisingependa kuyaelezea hapa.

Kuna wakati tukio hili huwa linaondoka kwenye fikra zangu ila kuna wakati vitu fulani vinatokea mfululizo halafu nakumbuka siku ile.

Mimi ni mtu wa maombi, najaribu sana kuwa hivyo. Sijakata tamaa na sitakata tamaa, lakini najiulizaga nitasubiri mpaka lini?

Naomba ushauri tafadhali. Hali yangu lazima ibadilike sasa hivi.

Pole kama ni kweli, na naomba kinachokuumiza kisiwe hiko cha wenzio kuitwa waheshimiwa, maana hapa ndio naona kuna kiini cha wewe kuteseka na si uchawi,
Ushauri, kila mtu amezaliwa akiwa na bahati yake ya mafanikio, wapo wanaozaliwa nakukuta mafanikio yako ndani ya familia, wapo wanaozaliwa nakukuta familia haina kitu na wao wakawa chachu ya mafanikio,
Fahamu kwamba kila mja anabahati yake ambayo huja kwa wakati wake, hata kama si kesho ikawa uzeeni mwako ndio ulipangiwa utoboe ukiwa na miaka hiyo 60 or 70.

Riziki hugawiwa na Mungu binadamu huizuia tu
 

Similar Discussions

6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom