Kuna tukio la kishirikina liliwahi kunitokea miaka kama 20 iliyopita na limebadilisha maisha yangu

Mabibi na Mabwana wa JF,

Naandika uzi huu hii ikiwa mara ya kwanza kabisa mimi kushare habari hii mahali popote. Sijawahi kumwambia mtu, hata familia yangu haijui kuhusu hili.

Nalileta kwenu kwa sababu nimenuia kabisa hili suala lazima nilitatue mwaka huu. Najaribu kuendelea kutambua watu ambao wanaweza kunisaidia kwa sababu nguvu inayonishikilia naona inaendelea kukaza kamba kweli kweli yaani siyo utani.

Kiufupi, kuna siku moja nikiwa kijana mdogo nilikuwa napanda basi wakati naelekea kukaa kwenye siti njiani nikapishana na mtu mmoja amevaa baibui jeusi amejifunika hadi usoni. Ilikuwa ni hapa hapa Dar es Salaam. Nakumbuka hadi kituo nilichokuwa nimepanda. Wakati napishana naye akaniwekea vidole machoni. Mimi nikapata kama bumbuazi fulani hivi yeye nadhani akashuka.

Kiufupi, maisha yangu hayajawa sawa toka wakati huo. Mimi ni mtu mwenye uwezo sana kiakili ila hata chuo niliishia katikati tena GPA yangu ikiwa ya juu. Wenzangu wamesogea sana na wengine wanaitwa waheshimiwa sasa hivi wakati mimi nimekuwa mtu ambaye hata nijaribu vipi niko pale pale. Na hata familia yangu kiujumla ukianzia kaka na dada zangu wana hali fulani ya kuhangaika tu wote. Tungeweza kufanya mambo makubwa binafsi na hata pamoja ila hakuna tunaloweza kuonyesha mpaka sasa.

Story yangu ni ndefu sana na nimepitia mengi mno nisingependa kuyaelezea hapa.

Kuna wakati tukio hili huwa linaondoka kwenye fikra zangu ila kuna wakati vitu fulani vinatokea mfululizo halafu nakumbuka siku ile.

Mimi ni mtu wa maombi, najaribu sana kuwa hivyo. Sijakata tamaa na sitakata tamaa, lakini najiulizaga nitasubiri mpaka lini?

Naomba ushauri tafadhali. Hali yangu lazima ibadilike sasa hivi.
Pole sana kwa mambo uliyokumbana nayo, kawaida binadamu tunapo kabiliana na mambo magumu maishani basi mawazo na hisia huwa nyingi sana sana.

Kwa maelezo yako bado itakuwa ngumu sana hapa kukupa ushauri, hebu funguka yote ilibiwe rahisi kusaidiw mawazo.

Hilo la kusema ulikutana na mtu amevaa baibui na akakuwekea vidole halina nguvu kwani mwenyewe umesema hata familia yenu inakabilina na matatizo hayo hayo.

Nakushauri funguka zaidi kwani mara nyingi mambo kama haya huwa yaaanzia mbali ndani ya ukoo wenu..chunguza hili.

Pia pitia hili bandiko hapa utajifunza mambo mengi hapa.
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako! - JamiiForums

Sent using Jamii Forums mobile app
 
If you are desperate then you are closer to your Answer. God is near press on and you shall find. Cry out to God He will Answer from heaven.
The opportunity that God gave us (the human beings) is to be able to kneel down, lift up our hands, close our eyes and speak to Him. Use it till you are satisfied in your soul There is no other creature have such opportunity except you and me. God bless you
 
If you are desperate then you are closer to your Answer. God is near press on and you shall find. Cry out to God He will Answer from heaven.
The opportunity that God gave us (the human beings) is to be able to kneel down, lift up our hands, close our eyes and speak to Him. Use it till you are satisfied in your soul There is no other creature have such opportunity except you and me. God bless you

Amen. Asante sana kwa maneno yako ya faraja. Na mimi pia naamini kabisa nimepita kwenye tanuru la moto ili niwe Ushuhuda kwa Mataifa.
 
Pole sana kwa mambo uliyokumbana nayo, kawaida binadamu tunapo kabiliana na mambo magumu maishani basi mawazo na hisia huwa nyingi sana sana.

Kwa maelezo yako bado itakuwa ngumu sana hapa kukupa ushauri, hebu funguka yote ilibiwe rahisi kusaidiw mawazo.

Hilo la kusema ulikutana na mtu amevaa baibui na akakuwekea vidole halina nguvu kwani mwenyewe umesema hata familia yenu inakabilina na matatizo hayo hayo.

Nakushauri funguka zaidi kwani mara nyingi mambo kama haya huwa yaaanzia mbali ndani ya ukoo wenu..chunguza hili.

Pia pitia hili bandiko hapa utajifunza mambo mengi hapa.
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako! - JamiiForums

Sent using Jamii Forums mobile app

Asante sana. Ngoja nijaribu kutafakari nini zaidi cha kuongeza ila kiukweli ni mambo mengi sana. Kuna mengine roho yangu imejaribu kunisahaulisha kwa sababu nikikumbuka baadhi ya mambo nasononeka sana. Kila nikiuchunguza moyo wangu na tabia zangu bila kujidanganya najiona kabisa sistahili masahibu niliyopitia. Sisemi mimi ni perfect. Nimekuwa na madhaifu yangu kama binadamu na kuna makosa yamefanyika pia ila yote hayo hayawezi kutoa maelezo ya mateso yangu.

Kuhusu karma, naifahamu vizuri na kuna wakati nilisoma hata mafundisho ya Buddhism yanayoielezea. Lakini kumbuka mafundisho mengine inabidi usome ukiwa na msingi wa imani ili usije ukayumbishwa au kupotoshwa. Unachukua kilicho kizuri unaacha vingine. Story ya Ayubu ni mfano mmoja wapo.
 
Ulijitune tu kisaikolojia.. hamna kitu hapo wakati mwingine imani mpya unayoiwaza inaingia na kuwa sehemu ya vipokeo vipya kwenye ubongo.

Vipi saivi unaweza kukalili mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo nimesummarize tu mkuu ... Kuna matatizo zaidi nilikumbana nayo... Tatizo halikuwa kukalili tu ..yani nilikuwa sielewi kitu kabisa na homa zisizo eleweka zilinisumbua sana... Nilipata tabu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna matukio yanweza kutokea kwa mtu mwingine akadhani ni masihara.
Kwa mfano kule ulongoni Gongolamboto kuna shule moja ya msingi kuna msichana mmoja anaongoza ktk mitihani. Sasa wenzake hawajafurahia hiyo hali ya kuongozwa wakaanza kumtishia kumtoboa macho. Hapohapo kuna mwanafunzi mwingine akatobolewa macho. Yaani mzazi mwenyemtoto anasikitika sana...mtoto wake amekuwa na hofu na amepunguza bidii ya kusoma na mwaka ulioisha amefanya vibaya sana shuleni.

Mambo yasiwe mengi, mengi yasiwe mambo
 
Inashangaza watu wamejikita kwenye vazi na si hoja. Yaani kuna watu kabisa kutajwa hilo vazi wamesha hemkwa hawataki kabisa kufikiria jambo lingine.mimi sioni kosa kwa mtoa mada kuelezea kilichotokea. Hata kama mhusika angevaa suit au bukta.

Kwa nini watanzania tunakuwa na akili kondefu? Mbona wapo wengi majambazi wanavaa baibui, makahaba na makaka poa pia?

Why watu wakazanie baibui au kuna mtu humu ndo alifanya hivyo siku hiyo anajitetea?
 
Labda unalosema ni kweli lakini kwa nini umekuja na conclusion hiyo na siyo ya kwangu? Nilikuwa bwa mdogo sana kufikiria lolote wakati ule. Tukio nililisahau au sikuliweka katika mawazo yangu kabisa mpaka baadae miaka ikapita ndiyo nikagundua kuna vitu vinavyoshabihiana vinajirudiarudia.
Yaani huyo dada ndiye huwa aliyefunga macho yako mtu wa GPA nzuri mpaka ukashindwa paper za mithani ya uhandisi? Wengine tumefanya kazi maeneo mnayosema mabaya km handeni, mafia mtwara, mara, dodoma, mpaka sumbawanga na hatuna chanjo yoyote. Mwisho kwa wanyaturu na tuko ok. MUNGU NDIO KILA KITU. ACHANA NA MAFIKIRA YA UCHAWI. WANALOGANA WANAOJUANA NA WACHAWI TU. Wewe ni NANI? HAYA NDIO WANAVYOSEMA WACHAWI . Wewe hawajakuambia hakulogi mtu asiyekujua? SASA KWANI UMSHUKU YULE DADA WA WATU? KWANZA NADHANI UJUMBE ALIOKUPA UMFUATE HAUKUELEWA HAUKO SHARP. SIO KUKULOGA
 
Pole ndugu kwa matatizo
Kikubwa jitahidi kufuta hiyo dhana ya kurogwa, mikosi na laana
Just think postive & believe yourself
 
Una maana huyo mchawi alikuroga wewe na familia yako? You're being delusional mkuu, usitafute mchawi wakumpa lawama sababu uchawi wenyewe haupo pambana.
Unaposema uchawi haupo nakataa. Mimi naishi na ushuhuda wa wazi wa uchawi niliofanyiwa. Nilipopata umri wa miaka 15 na kidogo hivi, nikiwa usingizini usiku mmoja, ghafla nilshtuka na kuamka. Nikahisi kama kinywa changu kimepwaya mno. Nikapeleka vidole mdomoni. Nikakuta kinywani hakuna jino hata moja!!!! Kwa mshangao na hofu nikapiga kelele kubwa sana hata majirani waliamka kuja kujua kuliokoni. Wote, wazazi na majirani walitunduwaa kuona sina jino hata moja!! Wakaniamuru nirudi kulala na kutulia tuli ili walioazima meno yangu wanirudishie baada ya kuyatumia!
Nikarudi kulala hadi asubuni. Meno yangu hayakurudishwa hadi leo niingiapo umri mpevu. Ninatumia meno ya bandia. Na sikuweza kuyafaidi meno yangu kutoka siku hiyo ambapo nlikuwa mpenzi wa kande, miwa na bisi.
Niliambiwa nilifanya kosa kupiga kelele baada ya kuona meno yangu hayapo. Eti ningebaki kimya na kuendelea na usingizi kusubiria wachawi wanirudishie meno yangu.
Kwa utoto sikuwa najua hili. Kumbe meno yalikuwa yakiazimwa bila mwenye meno kujua na kurudishiwa.
Anayesema uchawi haupo hayajamkuta. Tupo sisi ambao ni ushuhuda unaoishi wa vitendo vya kichawi kuwepo duniani


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uwongo wako usilete hapa hata mara moja,Nenda kaombewe kanisani
Such a low minded person, kwakua haijakutokea wewe then huna mamlaka ya kumuita mtu ni muongo, you're showing us how stupid you are... Pia iwapo nimepata tatizo na mhusika amevaa kama masista wa kikatoliki then katika kuelezea nishindwe kuelezea appearance ya mhusika kisa utakwazika sababu wewe ni mkatoliki?! Grow up, huu ni uwanja mpana huna la kuchangia keep your mouth shut

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabibi na Mabwana wa JF,

Naandika uzi huu hii ikiwa mara ya kwanza kabisa mimi kushare habari hii mahali popote. Sijawahi kumwambia mtu, hata familia yangu haijui kuhusu hili.

Nalileta kwenu kwa sababu nimenuia kabisa hili suala lazima nilitatue mwaka huu. Najaribu kuendelea kutambua watu ambao wanaweza kunisaidia kwa sababu nguvu inayonishikilia naona inaendelea kukaza kamba kweli kweli yaani siyo utani.

Kiufupi, kuna siku moja nikiwa kijana mdogo nilikuwa napanda basi wakati naelekea kukaa kwenye siti njiani nikapishana na mtu mmoja amevaa baibui jeusi amejifunika hadi usoni. Ilikuwa ni hapa hapa Dar es Salaam. Nakumbuka hadi kituo nilichokuwa nimepanda. Wakati napishana naye akaniwekea vidole machoni. Mimi nikapata kama bumbuazi fulani hivi yeye nadhani akashuka.

Kiufupi, maisha yangu hayajawa sawa toka wakati huo. Mimi ni mtu mwenye uwezo sana kiakili ila hata chuo niliishia katikati tena GPA yangu ikiwa ya juu. Wenzangu wamesogea sana na wengine wanaitwa waheshimiwa sasa hivi wakati mimi nimekuwa mtu ambaye hata nijaribu vipi niko pale pale. Na hata familia yangu kiujumla ukianzia kaka na dada zangu wana hali fulani ya kuhangaika tu wote. Tungeweza kufanya mambo makubwa binafsi na hata pamoja ila hakuna tunaloweza kuonyesha mpaka sasa.

Story yangu ni ndefu sana na nimepitia mengi mno nisingependa kuyaelezea hapa.

Kuna wakati tukio hili huwa linaondoka kwenye fikra zangu ila kuna wakati vitu fulani vinatokea mfululizo halafu nakumbuka siku ile.

Mimi ni mtu wa maombi, najaribu sana kuwa hivyo. Sijakata tamaa na sitakata tamaa, lakini najiulizaga nitasubiri mpaka lini?

Naomba ushauri tafadhali. Hali yangu lazima ibadilike sasa hivi.
Ulichukuliwa nyota

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naweza nikanywa chupa moja mara moja moja sana lakini naweza pia kwenda mwaka bila kuonja pombe na siyo kwa sababu nakuwa sina hela ya kunywa, ni kujicontrol tu. Siyo mfujaji wa hela kama ndiyo wasiwasi wako.

Umeenda mbali sana, lengo langu nilitaka kujua watumia au hutumii ili nikushauri. Pombe ndio tiba pekee ya ushirikina. Ukiwa mnywaji hakuna mahirikina atakusogelea wala uchawi. CC Mshana Jr


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilichogundua tatizo lako ni stress za maisha na ukosefu wa kipato wala sio huyo mwenye baibui, fanya kazi, zungusha akili, tafuta pesa utamsahau huyo mtu, acha kuamini vitu vya kijinga mimi narogwa kila siku naona vitu vya ajabu, ila huwa na amini ni ujinga wao!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeenda mbali sana, lengo langu nilitaka kujua watumia au hutumii ili nikushauri. Pombe ndio tiba pekee ya ushirikina. Ukiwa mnywaji hakuna mahirikina atakusogelea wala uchawi. CC Mshana Jr


Sent using Jamii Forums mobile app
Nyie ndio mnadanganyana vijiweni, pombe haijawahi kumzuia mchawi au jini kufanya kazi anayokusudia... We lewaaaaa, vuta bangeeee, kula kitimoto etc haisaidii kitu kama huna imani inakula kwako tu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom