QEEN ADEMU1
Senior Member
- Dec 24, 2019
- 134
- 324
Kuna tofauti kubwa kati ya mwanaume kuwa baba wa mtoto wako na mwanaume kuwa mwanaume uliyezaa naye.
Kuzaa na mwanaume fulani haimaanishi kuwa yeye ni baba kwa mtoto huyo.
Kuna wanaume hawajui jinsi ya kuwa baba, wanajua tu kugawa mimba, kisha wanatelekeza mimba na watoto. Kisha wao wanaendelea kula bata na kuku. Wengine umri mkubwa tu lakini hooooovyooooo!
Wanatelekeza watoto!
Mwisho wa siku mtoto amekua kwa jitihada za mama tu ndipo nao wanajipendekeza kwa mtoto eti "Fulani ni mtoto wangu".
Wasipopata msaada wa watoto hao wanahisi watoto hawawajali. Wanasahau kuwa nao waliwatelekeza hao watoto enzi zile.
.
MWANAMKE: Usifikiri kuwa kuzaa tu na mwanaume fulani kutamfanya awe baba wa mtoto wako. Sahau, kuwa makini. Usikurupukie tu kuzaazaa kama mbwa. Unataka kuonesha na wewe una uzazi kila rungu likipita mimba tuliaoa zipo ukiwa makini ndoa. Mimba sio gundi ya kukufanya uolewe.
.
MWANAUME: Jifunze kuwa baba. Umempa binti wa watu mimba muhudumie. Kutelekeza mimba na mtoto ni upumbavu. Halafu baadaye unaanza kujipendekeza, "Ile damu yangu kabisa lakini kanitupa. Nitammwagia radhi." Mwaga tu, zitakumwagikia mwenyewe.
Leo yako unayeiandaa ni wewe, ukicheza vibaya hao unaokula nao bata unaagiza bia mezani zinajaa unaona ujanja wakati watoto wako wako kwa bibi yao suruali zimechanika, hawana mashati. Hivi wewe ni mwanaume kweli?
Hao unaofurahia nao kuna siku watakuacha huna hata wa kukulipia bili ya dawa hospitali, utaaanza niitieni mwanangu!
MWANAMKE: Jifunze kujiongeza njia za uzazi wa mpango zipo nyingi sipendi nizitaje. Usitake tu kuzaaa halafu watoto unampelekea mama yako unarudi tena mjini. Unajua huzuni juu ya hao watoto unaowazaa na kuwaficha huko kijijini, hivi umewahi kulifikiria hilo?
Wanaume wenzangu najua wengi ukiulizwa una watoto wangapi unataja idadi unasahau wengine wapo wengi tu. Unakumbuka mimba uliyompa housegirl mama yako akamtimua; unajua mtoto ana umri gani sasa?
We mwanaume unakumbuka uliyempa binti yule dada muuza chakula halafu ukahama na kwenda kula pale? Hata kama humpendi mjali basi mwanao.
#Sijakasirika
#Usitelekeze #mimba #Mtoto
Sent using i phone x
Kuzaa na mwanaume fulani haimaanishi kuwa yeye ni baba kwa mtoto huyo.
Kuna wanaume hawajui jinsi ya kuwa baba, wanajua tu kugawa mimba, kisha wanatelekeza mimba na watoto. Kisha wao wanaendelea kula bata na kuku. Wengine umri mkubwa tu lakini hooooovyooooo!
Wanatelekeza watoto!
Mwisho wa siku mtoto amekua kwa jitihada za mama tu ndipo nao wanajipendekeza kwa mtoto eti "Fulani ni mtoto wangu".
Wasipopata msaada wa watoto hao wanahisi watoto hawawajali. Wanasahau kuwa nao waliwatelekeza hao watoto enzi zile.
.
MWANAMKE: Usifikiri kuwa kuzaa tu na mwanaume fulani kutamfanya awe baba wa mtoto wako. Sahau, kuwa makini. Usikurupukie tu kuzaazaa kama mbwa. Unataka kuonesha na wewe una uzazi kila rungu likipita mimba tuliaoa zipo ukiwa makini ndoa. Mimba sio gundi ya kukufanya uolewe.
.
MWANAUME: Jifunze kuwa baba. Umempa binti wa watu mimba muhudumie. Kutelekeza mimba na mtoto ni upumbavu. Halafu baadaye unaanza kujipendekeza, "Ile damu yangu kabisa lakini kanitupa. Nitammwagia radhi." Mwaga tu, zitakumwagikia mwenyewe.
Leo yako unayeiandaa ni wewe, ukicheza vibaya hao unaokula nao bata unaagiza bia mezani zinajaa unaona ujanja wakati watoto wako wako kwa bibi yao suruali zimechanika, hawana mashati. Hivi wewe ni mwanaume kweli?
Hao unaofurahia nao kuna siku watakuacha huna hata wa kukulipia bili ya dawa hospitali, utaaanza niitieni mwanangu!
MWANAMKE: Jifunze kujiongeza njia za uzazi wa mpango zipo nyingi sipendi nizitaje. Usitake tu kuzaaa halafu watoto unampelekea mama yako unarudi tena mjini. Unajua huzuni juu ya hao watoto unaowazaa na kuwaficha huko kijijini, hivi umewahi kulifikiria hilo?
Wanaume wenzangu najua wengi ukiulizwa una watoto wangapi unataja idadi unasahau wengine wapo wengi tu. Unakumbuka mimba uliyompa housegirl mama yako akamtimua; unajua mtoto ana umri gani sasa?
We mwanaume unakumbuka uliyempa binti yule dada muuza chakula halafu ukahama na kwenda kula pale? Hata kama humpendi mjali basi mwanao.
#Sijakasirika
#Usitelekeze #mimba #Mtoto
Sent using i phone x