Kuna Tofauti Gani Kati ya Hizi Card? Na Nini Kimejificha Ndani Yake?

Pi Network

JF-Expert Member
Mar 22, 2016
290
319
Wakuu kwa kipindi kirefu nimekuwa nikitumia hizi Card mbili za bank kwa ajili ya kupata huduma za ki-fedha katika ATM zote zinazo ruhusu kutumia (Visa card & Master Card) zilizopo hapa nchini bila shaka na hata nje ya nchi. Lakini pia nimekuwa nikizitumia kununua bidhaa online, ikiwa ni pamoja na kulipia baadhi ya Apps muhimu pale inapohitajika.

Kwa kweli ni jambo zuri sana na ni mradi unaofaa zaidi hasa katika jamii yetu ukilinganisha na changamoto mbalimbali zilizopo ndani ya mabenki na uchache wa mabenki hasa huko vijijini na maeneo ya mashambani ambako hakuna bank isipokuwa ATM.

Lakini yote tisa, kumi, licha ya Card hizi kupigiwa debe duniani kote, na ma-Bank karibu yote hasa hapa nchini kuanza kutoa kadi hizi; bado sijajua tofauti kubwa iliyopo kati yake.

Na kwanini hizi Card? Nini kimejificha ndani ya hizi Card?
Je, kuna hatari yoyote iliyojificha ndani ya mpango huu?

Kuna siri nimeisikia japo ni kwa jujuu tu na sitaki kuiamini sana, hivyo pengine yawezekana humu ndani tunao watu wanaoijua vizuri zaidi na wanaweza kujuza na sisi.

Mwisho: nawatakieni weekend njema kwa ajili ya kuukaribisha mwaka mpya utakao ambatana na mambo mapya.
c41a058e1990cccd687e34b2ca056fd8.jpg
 
Kama ulikuwa unatoroka darasani, matokeo yake ndo haya umeshindwa jenga hoja... haueleweki
 
Hizi ni multinational financial services kwa hyo mtu unakua na option ya kupata huduma sehem tofauti.
 
Hazina tofauti kubwa sana. Kinachotofautisha kwanza ni majina,moja inaitwa Master Card na nyingine inaitwa Visa Card.

Pili,ni watengenezaji wa kadi zenyewe. Visa na Master Card hutengenezwa na benki au taasisi za fedha husika lakini kwa kutumia brand za kampuni tajwa. Yaani mfano mdogo ni CocaCola,kila mwekezaji anayevutiwa ana uwezo wa kutengeneza kinywaji hicho lakini kwa kufata Standards zilizowekwa na Cocacola Company ili uweze kupewa leseni ya kutumia jina ka kampuni kutengeneza na kuuza bidhaa zako.

Tatu,zote zinakubalika katika nchi nyingi sana katika swala zima la Transactions (locally and online). Ni vigumu sana kukuta baadhi ya sehemu zinakubali Master Card alafu zinakataa Visa Cards,ni chache sana.

Ni benki au watengenezaji wa kadi hizo ndiyo wana uwezo wa kuziwekea limits za matumizi hizo kadi. Mfano,CRDB wanaweza kuamua kadi fulani uwezo na mipaka yake ya kutumika ni hapa na Visa mipaka yake ya matumizi ni hapa. Hivyo tu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom