mwalimu Jr.
Member
- Aug 20, 2008
- 51
- 4
KWA MUJIBU wa Idhaa ya Kiingereza ya BBC kuna mbwia unga mmoja karibu kwa kila familia kisiwani Zanzibar.
Mara tu siasa ya Ujamaa ilipokufa na Tanzania kufungua milango yake wazi kwa kila aina ya biashara-haramu na halali kuingia nchini-utu, adabu, uungwana na maadili yote kwa ujumla yalitokea dirishani na madawa ya kulevya, umalaya, ulevi, mabaa na pombe, usenge na uhayawani wa kila aina ukaingia kupitia mlangoni.
Aidha tabia ya viongozi wa CCM ya kuwabagua na kuwaacha watu na hususan vijana wenye akili ambao hawataki kulamba miguu yao kwenye mataa kwa kutowapa fursa za kazi, usanii wala michezo kumechangia kwa kiasi kikubwa 'frustaration' zinazosababisha vijana wengi kuishia kwenye tabia ya kubwia madawa, kuwa wakorofi na wahalifu jambo ambalo kabla ya hapo lilikuwa nadra visiwani humo.
Jambo jingine ni upinzani kuibiwa ushindi katika chaguzi mbili-tatu zilizopita na Bara kuhakikisha imewarejesha nokoa wao wa visiwani madarakani kwa udi na uvumba ili lisitokee lile ambalo litafanya upinzani bara kuona ala kumbe CCM inang'oleka. Hivi sasa kisiwa hicho kimekaliwa na polisi na askari wengi kutoka bara ambao wakati mwingine hudaiwa kuipigia CCM kura wakati wa uchaguzi.
Pamoja na CUF kuwa inashinda mara zote katika asilimia 99 ya viti visiwani Pemba, CCM ya Unguja imekataa kata kata kuingia kwenye ubia au mseto au serikali mchanganyiko ili kutumia akili na vipaji vya Wazaznzibari wote kuleta maendeleo ya kweli na uhakika.
Visiwa vya Unguja na Pemba vina kila sababu ya kuwa Dubai au UAE ya Afrika Mashariki iwapo kutakuwa na haki za binadamu, kuheshimiwa demokrasia na watu wot kupewa fursa za kuchangia katika maendeleo ya visiwa hivyo bila ya ubaguzi wa aina yoyote hili. Hili halijawezekana hadi hivi leo na matokeo yake ni kuwaathiri vijana ambao hukata tamaa na kujiingiza kwenye madhambi mbalimbali ikiwemo hayo ya kujiduna sindano za heroin, ambalo nalo huzua jipya kutokana na watu wengi kuchangia sindano moja ukimwi umeanza kuvamia hususan kisiwa cha Unguja toka kaskazini hadi kusini.
Familia zilizonusurika ni zile ambazo zimewapeleka watoto wao kusoma na kufanya kazi nje na hivyo kuvinyang'anya visiwa hivyo watu wenye uwezo kiakili na kifikira. Viongozi wengi wa serikali kama walivyo watumishi wengi visiwani humo kwa hivi sasa ni watu wenye sifa zenye mashaka kielimu na kiutaalamu.
Wachunguzi wa mambo wanaamini laana ya kuwa na mateja kwa kila familia huko Unguja baadhi yao wakiwa wanatokea familia za viongozi na matajiri wakubwa visiwani huko haiwezi kuondoka hadi pale kutakapokuwepo na haki, usawa na uwajibikaji kisiasa visiwani humo.
Mara tu siasa ya Ujamaa ilipokufa na Tanzania kufungua milango yake wazi kwa kila aina ya biashara-haramu na halali kuingia nchini-utu, adabu, uungwana na maadili yote kwa ujumla yalitokea dirishani na madawa ya kulevya, umalaya, ulevi, mabaa na pombe, usenge na uhayawani wa kila aina ukaingia kupitia mlangoni.
Aidha tabia ya viongozi wa CCM ya kuwabagua na kuwaacha watu na hususan vijana wenye akili ambao hawataki kulamba miguu yao kwenye mataa kwa kutowapa fursa za kazi, usanii wala michezo kumechangia kwa kiasi kikubwa 'frustaration' zinazosababisha vijana wengi kuishia kwenye tabia ya kubwia madawa, kuwa wakorofi na wahalifu jambo ambalo kabla ya hapo lilikuwa nadra visiwani humo.
Jambo jingine ni upinzani kuibiwa ushindi katika chaguzi mbili-tatu zilizopita na Bara kuhakikisha imewarejesha nokoa wao wa visiwani madarakani kwa udi na uvumba ili lisitokee lile ambalo litafanya upinzani bara kuona ala kumbe CCM inang'oleka. Hivi sasa kisiwa hicho kimekaliwa na polisi na askari wengi kutoka bara ambao wakati mwingine hudaiwa kuipigia CCM kura wakati wa uchaguzi.
Pamoja na CUF kuwa inashinda mara zote katika asilimia 99 ya viti visiwani Pemba, CCM ya Unguja imekataa kata kata kuingia kwenye ubia au mseto au serikali mchanganyiko ili kutumia akili na vipaji vya Wazaznzibari wote kuleta maendeleo ya kweli na uhakika.
Visiwa vya Unguja na Pemba vina kila sababu ya kuwa Dubai au UAE ya Afrika Mashariki iwapo kutakuwa na haki za binadamu, kuheshimiwa demokrasia na watu wot kupewa fursa za kuchangia katika maendeleo ya visiwa hivyo bila ya ubaguzi wa aina yoyote hili. Hili halijawezekana hadi hivi leo na matokeo yake ni kuwaathiri vijana ambao hukata tamaa na kujiingiza kwenye madhambi mbalimbali ikiwemo hayo ya kujiduna sindano za heroin, ambalo nalo huzua jipya kutokana na watu wengi kuchangia sindano moja ukimwi umeanza kuvamia hususan kisiwa cha Unguja toka kaskazini hadi kusini.
Familia zilizonusurika ni zile ambazo zimewapeleka watoto wao kusoma na kufanya kazi nje na hivyo kuvinyang'anya visiwa hivyo watu wenye uwezo kiakili na kifikira. Viongozi wengi wa serikali kama walivyo watumishi wengi visiwani humo kwa hivi sasa ni watu wenye sifa zenye mashaka kielimu na kiutaalamu.
Wachunguzi wa mambo wanaamini laana ya kuwa na mateja kwa kila familia huko Unguja baadhi yao wakiwa wanatokea familia za viongozi na matajiri wakubwa visiwani huko haiwezi kuondoka hadi pale kutakapokuwepo na haki, usawa na uwajibikaji kisiasa visiwani humo.