MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 20,897
- 63,783
Mtu unaamka unataka kununua umeme au maji kwa kupitia mtandao wa Airtel au VodaCom. Unafanya manunuzi unaambiwa muhamala haujafanikiwa lakini pesa wanakata. Halafu ukiwapigia simu huduma kwa wateja wanasema watarudisha muhamala huo ndani ya masaa 96 ya kazi yaani siku nne.
Kipindi cha nyuma tatizo kama hili likitokea pesa ilikuwa haikatwi kabisa (Nadra sana na likitokea aidha utapata huduma kwa haraka au pesa yako), lakini siku hizi wanakata hata mara mbili bila kuogopa.
Hili tatizo lingekuwa linatokea kwa nadra basi tungesema ni bahati mbaya, lakini linatokea mara nyingi sana na wanakata pesa zetu nyingi na huduma hatupati. Kibaya zaidi huu uzembe hauchukuliwi kabisa hatua na mamlaka husika. Ila bahati mbaya sisi wengine tuna masikio makubwa na tumeanza kupata minong'ono ya kinachoendelea nyuma ya pazia: Sababu zinazopelekea haka kamchezo kufanyika lakini tukaamua kuzipuuza.
Sisi yetu macho.
Kipindi cha nyuma tatizo kama hili likitokea pesa ilikuwa haikatwi kabisa (Nadra sana na likitokea aidha utapata huduma kwa haraka au pesa yako), lakini siku hizi wanakata hata mara mbili bila kuogopa.
Hili tatizo lingekuwa linatokea kwa nadra basi tungesema ni bahati mbaya, lakini linatokea mara nyingi sana na wanakata pesa zetu nyingi na huduma hatupati. Kibaya zaidi huu uzembe hauchukuliwi kabisa hatua na mamlaka husika. Ila bahati mbaya sisi wengine tuna masikio makubwa na tumeanza kupata minong'ono ya kinachoendelea nyuma ya pazia: Sababu zinazopelekea haka kamchezo kufanyika lakini tukaamua kuzipuuza.
Sisi yetu macho.