Kuna tatizo kwa Waisilamu. Safari hii lisijirudie

Kulupango

JF-Expert Member
Mar 19, 2020
288
534
Kila ifikapo sikukuu ya Eid, iwe Eid ya kuchinja (Udhu-hiya) au Eid ya baada ya Ramadhani (Eidil - Fitir). BAKWATA hualika viongozi wa Serikali kuja kwenye baraza la Eid, cha ajabu zaidi sio kwa kiongozi mualikwa wala Mashekhe mada kubwa huwa ni kuzungumzia AMANI.

Sasa najiuliza waisilamu ndio watu wa vurugu kwenye nchi hii mpaka kila sherehe yao kuzungumze mada ya amani na tafaruku za nchi?

kwanini sikukuu ya kuchinja yasitolewe mawaidha ya Kisa cha kuchinja kutoka kwa Baba wa Imani Nabii Ibrahimu. Badala yake wanaalikwa viongozi kuja kuzungumza mambo ya Amani na kutolewa mifano ya nchi zilizo athiriwa na vita? Mbona sherehe za Pasaka na X-Mas hatuoni mada hizi za Amani zikizungumzwa?

Niwaombe viongozi wa BAKWATA, tumechoka na hizi taratibu zenu za kuja kuzungumza mambo ya Amani badala ya kuzungumza mafunzo husika ya siku hiyo. Hata kwenye mashindano ya visomo vya QUR'AN uwanja wa Taifa, anakuja kiongozi anazungumza mambo ya Amani. (sijui kuna tatizo gani hapa)

Na vipi mtu asiye muisilamu akawa mgeni rasmi kwenye mambo ya imani?. Yani kwa mfano sisi tupo kwenye sherehe ya pasaka kisha utuletee kiongozi wa serekali ambae ni muisilamu aje kuwa mgeni rasmi kwenye imani yetu ya kikristo, ilihali hafahamu chochote kuhusiana na pasaka.

Niombe viongozi wa serekali wasihusishwe kwenye shughuli za imani ya dini kama ''wageni rasmi'' kwasababu serekali haina dini. Na wakihusishwa basi wahudhurie kama watu wa kawaida. TUMECHOKA

maxresdefault.jpg
 
Tatizo ni kujishtukia coz wanajua mziki wa wananchi, pia baadhi ya mashekhe na mapadri wapo kimaslah zaidi ktk serikali so usishangae kwa hilo
 
Kwamba kiongozi wa kiislamu asiijue pasaka wakati ilikuwepo kabla ya ukristo na uislamu
 
Kila ifikapo sikukuu ya Eid, iwe Eid ya kuchinja (Udhu-hiya) au Eid ya baada ya Ramadhani (Eidil - Fitir). BAKWATA hualika viongozi wa Serikali kuja kwenye baraza la Eid, cha ajabu zaidi sio kwa kiongozi mualikwa wala Mashekhe mada kubwa huwa ni kuzungumzia AMANI.

Sasa najiuliza waisilamu ndio watu wa vurugu kwenye nchi hii mpaka kila sherehe yao kuzungumze mada ya amani na tafaruku za nchi?

kwanini sikukuu ya kuchinja yasitolewe mawaidha ya Kisa cha kuchinja kutoka kwa Baba wa Imani Nabii Ibrahimu. Badala yake wanaalikwa viongozi kuja kuzungumza mambo ya Amani na kutolewa mifano ya nchi zilizo athiriwa na vita? Mbona sherehe za Pasaka na X-Mas hatuoni mada hizi za Amani zikizungumzwa?

Niwaombe viongozi wa BAKWATA, tumechoka na hizi taratibu zenu za kuja kuzungumza mambo ya Amani badala ya kuzungumza mafunzo husika ya siku hiyo. Hata kwenye mashindano ya visomo vya QUR'AN uwanja wa Taifa, anakuja kiongozi anazungumza mambo ya Amani. (sijui kuna tatizo gani hapa)

Na vipi mtu asiye muisilamu akawa mgeni rasmi kwenye mambo ya imani?. Yani kwa mfano sisi tupo kwenye sherehe ya pasaka kisha utuletee kiongozi wa serekali ambae ni muisilamu aje kuwa mgeni rasmi kwenye imani yetu ya kikristo, ilihali hafahamu chochote kuhusiana na pasaka.

Niombe viongozi wa serekali wasihusishwe kwenye shughuli za imani ya dini kama ''wageni rasmi'' kwasababu serekali haina dini. Na wakihusishwa basi wahudhurie kama watu wa kawaida. TUMECHOKA

View attachment 1520292
Magaidi utawajua tu
 
Umeongea vyema sana.
Kama hujaoa nakupa binti yangu bure pamoja na mtaji wa biashara endapo ukipenda.
Sharti la kuzingatia usiwe Utopolo.
Vijana wa leo hawajafika kukuuliza kama huyo binti ana CHURA? ngoja waje wakuulize.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom