Miaka ya huko nyuma Umoja huu wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) ulisifika sana kwa kuandaa viongozi bora , wenye weledi na uongozi, wenye maarifa, uzalendo na nchi yao, wachapa kazi na wenye misingi ya haki, utu na maadili ya kutosha mfano wa ni pamoja na Waziri Mwandamizi wa siku nyingi anayehudumu Wizara ya Ardhi Mh. William Lukuvi na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro waa sasa Martin Shigella.
Lakini miaka ya hivi karibuni Umoja huo umekuwa ukitoa viongozi wasio sifa wenye na mifano mmibaaya kwa Taifa, mf. mwaka 2014 Paulo Makonda aliyepikwa kwenye umoja huo alimpiga vibao Waziri Mkuu M staafu Jaji Joseph Sinde Warioba. Mwaka 2015 tukamwona aliyekuwa Mwenyekiti wa muda mrefu Dr.Emmanuel Nchimbi akipinga maamuzi ya Halmashauri Kuu ya Chama na kuongoza kikundi wakiimba wana imani na Lowassa.
Alipoingia Magufuli kwenye uenyekiti wa chama na kumpa mpwa wake kuongoza umoja huo, Kheri James naye akatoka adharani na kutishia kuwandunga watu wa upinzani na sindano za sumu. Aliyekuwa Mwenyekiti wa umoja huo mkoa wa Arusha 2017, Lengai Ole Sabaya alishtakiwa kwa kesi ya forgery kujifanya usalama wa Taifa na sasa yupo Kisongo na kesi ya kuendesha genge la wahalifu.
Je nini kumetokea ktk UVCCM imeacha kupika viongozi wazuri na sasa kutengeneza wahalifu, wapiga deal na wachumia tumbo?