Kuna taasisi za serikali watumishi wake wananuka madeni kama wamelaaniwa

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,702
36,121
Habari!

Katika pilikapilika za hapa na kule nilifika ofisi moja ya umma (Shirika la umma). Watumishi wamejaa madeni sio poa, mtumishi anadaiwa na Bank mpaka tatu, au benki moja kuna deni juu ya deni.

Hapo kuna mikopo ya wakopesha pesa kwa riba, yaani pesa za mkononi. Akipata posho analipa deni anakopa tena.

Nilimuhoji mmoja wa watumishi ambaye huwakopesha wenzake alisema karibu watumishi wote wana madeni ya namna hiyo.

Yeye mtaji wake ni mdogo, hivyo alinishauri nifungue ofisi ya kukopesha karibu na ofisi yao endapo nitakuwa na mtaji mkubwa. Alinihakikishia kuwa nitafanikiwa kiuchumi haraka.

Ni wakati sasa wataalamu wa uchumi kutoa semina elekezi za lazima kwa watumishi wa umma.

Tatizo sio MISHAHARA midogo tu bali tatizo hasa ni ukosefu wa elimu muhimu ya fedha.
 
Kuna mmoja ni afisa mikopo bank lakin sasa ana madeni kila mahala kuanzia bank, mitaan mpaka kwenye vikundi shida yake huyu anatamani kumiliki kila kitu hapa duniani,kila akisikia nyumba inauzwa anataman anunue.

Na huyu elimu ya hayo mambo anayo lakini ni tamaa
 
aliyekushauri kuchukua fursa kakushauri jambo zuri.au labda nawewe huna kitu umeshindwa.

yaani wewe umefika ofisi za watu badala ya kuafanya kilichokupeleka unaanza kufatilia nani anadaiwa na nani!!!
 
Kati ya kitu nitakuja fanya ni kukopesha pesa kwa kuweka mali yako.

Weka gari, Nipe Kadi, kadi tunabadili title holder, chukua hela, rudisha hela upewe gari.
Usiporudisha gari inauzwa
Maana riba nitaweka ndogo mf 5% kwa wiki ila itakuwa yaongezeka kila siku 1% ya deni husika

Laki kwa Laki na 5000
Usiporudisha inaongezeka 1500 kila siku
Kwa wiki 2, baada ya hapo mali yako inauzwa
 
Kati ya kitu nitakuja fanya ni kukopesha pesa kwa kuweka mali yako.

Weka gari, Nipe Kadi, kadi tunabadili title holder, chukua hela, rudisha hela upewe gari.
Usiporudisha gari inauzwa
Maana riba nitaweka ndogo mf 5% kwa wiki ila itakuwa yaongezeka kila siku 1% ya deni husika

Laki kwa Laki na 5000
Usiporudisha inaongezeka 1500 kila siku
Kwa wiki 2, baada ya hapo mali yako inauzwa
Ni biashara nzuri ila inahitaji uwe mtu mwenye kujua kudai ukiwa lelemama hatukulipi kwa wakati hapo bado sijaanza kukupigia magoti yaani mpaka utanisamehe mwenyewe
 
Ni biashara nzuri ila inahitaji uwe mtu mwenye kujua kudai ukiwa lelemama hatukulipi kwa wakati hapo bado sijaanza kukupigia magoti yaani mpaka utanisamehe mwenyewe
Nina mali yako tayari, mimi kazi itakuwa kukuandikia NOTISI tu, kupeleka kwa Balozi au Mjumbe wako akuletee.

Mkataba utakuwa upande wangu

NB ukishindwa lipa ndani ya muda fulani mali yako inabadilika na kuwa yangu
 
Back
Top Bottom