Kuna siku itakuja kila mtu atabaki mdomo wazi, ufalme utafitinika na kuvunjika vunjika

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Kwanza kabisa naomba nieleze kuwa baada ya kupata taarifa hizi za ghafla za kuhama Julius Mtatiro nilijiuliza sana kwanini? Baadaye nikagundua kuwa Mtatiro ameongea jambo moja la msingi sana kuwa "Sina jukwaa la kufanyia siasa kwa sasa" Hilo limemfanya ajione kuwa anapotea kisiasa akiwa bado kijana mdogo, uhuru wake umeminywa, hana jinsi. Anahitaji kujikuza kisiasa amebanwa mbavu na sasa hana jinsi.

Sasa basi hawa wanasiasa wanaohama upinzani wengi wao wamebanwa mbavu, wakitupiwa visenti kidogo tu wanayeyuka. Hata kina Tundu Lissu walipotaka kujinasua wakiwa huku upinzani waliishia kutwangwa risasi mchana kweupe tena hakuna kesi wala kuhoji na mbaya zaidi wala kuombea!

Hili linaonyesha wazi kuwa Rais Magufuli ni dikteta mbaya sana! Dikteta anayeiua Tanzania iliyokuwa imeanza kustawi kisiasa na Tanzania ya kuhoji! Huyu ni dikteta mbaya.

Naomba nimwambie wazi wazi Rais kuwa yeye alipatikana kirahisi sana kuwa mgombea wa CCM baada ya mtangulizi wake mzee JK kuruhusu serikali yake ichambuliwe, ikosolewe, ianikwe! Watuhumiwa wa ufisadi waliwekwa wazi, bunge liliwahoji na kupiga kelele hadharani. Hapa ndipo wanasiasa watarajiwa wa urais walianza kuonekana wachafu ndipo Magufuli akaibuka mbali na yeye kupewa uchafu wake. JK angekuwa mbinafsi kama alivyo Magufuli basi Urais angeusikia na kuuona maili milioni 100 kutoka alipo.


Sasa tunaona bunge halihoji tena, halipo huru, wanasiasa wanakosa majukwaa ya kisiasa huku chama dola kikitamalaki hapa kina Mtatiro lazima waibuke kama hawataweza kugangamala. Aibu ni kuwa leo Mtatiro anapokewa na yule yule aliyemsema kuwa ananunua wanaume wenzake! Asiogope kwani aibu ya upande huu kwa sasa ni dhaifu, aangalie tumbo lake. Zile siasa zake za face book na Twitter anaenda kuzitazama sijui tasemaje?

Sasa basi niitaadharishe hii CCM manunuzi kuwa walioenda huko wanaenda kutokana na kukosa namna. Huyu mtawala leo yupo kesho hayupo! Namna itarudi. CCM hii itavunjika vunjika, itapata shida sana.Kutakuwa na mparanganyiko mkubwa hapo mbele, najua wapo watakaobisha sasa ila tuombe uzima muda ambao si mrefu utakuja!

Hivi Kafulila, Mtatiro, Machali na wengine wanaunga mkono juhudi gani? Za rais kuonekana TBC kila mara? Maana aliyepita alikuwa hana huo muda! Za haya makelele tunayoyasikia kila mtendaji na kelele zake? Maana aliyepita alikuwa hana huo muda.

Nadhani gesi ya Mtwara ingegundulika kipindi cha Magufuli basi tusingelala maana wangehama kwa angalau kigezo kuwa "Amegundua gesi" "Wenzake walikuwa wanaikalia tu" Maana kama mtu anahama eti anasema kuwa Rais ameleta umeme wa Stiglers? Kweli? Eti amenunua ndege? Zinarejesha fedha zetu? Maana tulinunua kwa fedha zetu! Sasa kipi? Na hizo ndege angepewa bure si ndo tungewaomba wakenya wahamie Tanzania kuunga mkono juhudi?

Lakini pia tunapata funzo sasa kuwa watanzania wengi sana hawajaweza kujisimamia, kama hawa ambao wanaonekana afadhali wako tayari kujiacha utupu, vipi kwa wale kajamba nani? Tunapata ujumbe kuwa Tanzania bado haijawa na wanasiasa wengi waliokomaa. Ni aibu mtu anahama chama na hata kuuacha ubunge eti kwenda kuunga mkono Rais kujenga barabara! Aibu aibu! Lakini haya yote ni baada ya mbinu za kidikteta kutumika.
 
Kinachomiandama ni laana ya dakta Slaa kumtema mzee wa watu kwa karanga za kuonja.
 
Umenena vizuri sana. Hayo hayana muda mrefu. Nagufuli sio wa kudumu ktk uraisna ccm. Akiondoka watakosa pa kusimama na sababu ya kuwa huko. Anguko la CCM litakuwa kubwa sana. Haya maandiko yakae kama kumbu kumbu ili wakati huo yatumike kama rejea. Watakuja lia sana wakose wa kuwabembeleza maana raha ya kulia ni kubembelezwa usipo bembekezwa kilio kinakuwa kikavu na kwikwi kali.
 
Umesema maneno kuntu sana. Nashangaa hawa ccm wanaoshangilia wimbi la viongozi wa upinzani wanao unga mkono 'juhudi za Magufuli' wanapokuja huko kwao.
Maana halisi ni kuwa hawaifati ccm bali wanamfata Magufuli ili wapewe chao na vyeo kukabiliana na magumu wayapatayo.
Ndio maana mpango huo wa 'kuunga mkono' unapokamilika kinafuatia cheo na wao ccm 'itikadi' wanabaki wanasugua makalio.
Anayedhani ccm ipo kwa sasa anajidanganya kabisa kwani sasa hivi hakuna Chama chanye jina hilo mioyoni ila kwenye daftari la msajili na ofisi zao tuu.
Wapeleke Mtatiro, Kafulila, Msando hata Lipumba kuwapima na kipimo cha Lie detector utakutana na majibu utashindwa kuamini!
Waweza kukuta majibu kuwa Mtatiro au Kafulila anamchukia sana Magu kuliko amchukiavyo shetani.
Ila tukirudi kwenye hoja yako, ccm inaweza kuja kuzima kama kibatali siku Magu akitoka au kulazimishwa kutotumia dola kudhibiti upinzani maana sasa hivi ni Opposition vs Police na sio Opposition vs Ccm
 
Ni maoni yako mkuu na hamna objection. Siasa ni mchezo machafu sana, I wonder kama hawa wote wanaohama wananunuliwa. Kuna mambo pia upande wa pili yanawavuruga na hawayapendi. Hivyo basi ni utashi wa mtu kuamua nini afanye. Iwe kuhama au kutohama.

Mi sipendi staili ya kuhama chama kutumika kama mbadala wa kutatua matatizo yaliyopo vyama vya upinzani. Na ambavyo vyama vya upinzani vinapuuza malalamiko kwa kurahisisha kuwa '' wamenunuliwa ''. Sijui ila mi hainiingii vizuri akilini.

Mwisho, Tanzania ni zaidi ya Jiwe na vyama vya siasa. I wish tungeadopt system ya USA. Ili Uraisi isiwe '' one man show''. Na siasa iwe ni itikadi badala ya Kazi/ajira. Watu wanacompromise National agendas to suit their own interests. Sasa hii ndio democrasia gani? maana tunaitafsiri vibaya, mbona wazungu wameweza?
 
Umesema maneno kuntu sana. Nashangaa hawa ccm wanaoshangilia wimbi la viongozi wa upinzani wanao unga mkono 'juhudi za Magufuli' wanapokuja huko kwao.
Maana halisi ni kuwa hawaifati ccm bali wanamfata Magufuli ili wapewe chao na vyeo kukabiliana na magumu wayapatayo.
Ndio maana mpango huo wa 'kuunga mkono' unapokamilika kinafuatia cheo na wao ccm 'itikadi' wanabaki wanasugua makalio.
Anayedhani ccm ipo kwa sasa anajidanganya kabisa kwani sasa hivi hakuna Chama chanye jina hilo mioyoni ila kwenye daftari la msajili na ofisi zao tuu.
Wapeleke Mtatiro, Kafulila, Msando hata Lipumba kuwapima na kipimo cha Lie detector utakutana na majibu utashindwa kuamini!
Waweza kukuta majibu kuwa Mtatiro au Kafulila anamchukia sana Magu kuliko amchukiavyo shetani.
Ila tukirudi kwenye hoja yako, ccm inaweza kuja kuzima kama kibatali siku Magu akitoka au kulazimishwa kutotumia dola kudhibiti upinzani maana sasa hivi ni Opposition vs Police na sio Opposition vs Ccm
Kabisa mkuu, mtu akichambua kwa umakini basi sababu ha hawa wanaohama ipo na inaonekana. Hizo wanazotoa hazijawahi kuwa sababu na hazitokaa ziwe.
 
Magu amekuja wakat mwafaka. anatupa elimu ya kiraia kwa lazma. akija kuondoka tutakua tumekomaa. na watetez wa kweli wa wananchi watakua wamejulikana. kwa sasa ngano na magugu viko pamoja
hili nalo neno! Hadi JPM anaondoka kwakwel tutakuwa tumejua ipi ngano na yapi magugu kwa pande zote mbili
 
Ni maoni yako mkuu na hamna objection. Siasa ni mchezo machafu sana, I wonder kama hawa wote wanaohama wananunuliwa. Kuna mambo pia upande wa pili yanawavuruga na hawayapendi. Hivyo basi ni utashi wa mtu kuamua nini afanye. Iwe kuhama au kutohama.

Mi sipendi staili ya kuhama chama kutumika kama mbadala wa kutatua matatizo yaliyopo vyama vya upinzani. Na ambavyo vyama vya upinzani vinapuuza malalamiko kwa kurahisisha kuwa '' wamenunuliwa ''. Sijui ila mi hainiingii vizuri akilini.

Mwisho, Tanzania ni zaidi ya Jiwe na vyama vya siasa. I wish tungeadopt system ya USA. Ili Uraisi isiwe '' one man show''. Na siasa iwe ni itikadi badala ya Kazi/ajira. Watu wanacompromise National agendas to suit their own interests. Sasa hii ndio democrasia gani? maana tunaitafsiri vibaya, mbona wazungu wameweza?
Kama huamini kuwa wananunuliwa basi jipe muda kila kitu kitakuwa wazi.
 
Kwanza kabisa naomba nieleze kuwa baada ya kupata taarifa hizi za ghafla za kuhama Julius Mtatiro nilijiuliza sana kwanini? Baadaye nikagundua kuwa Mtatiro ameongea jambo moja la msingi sana kuwa "Sina jukwaa la kufanyia siasa kwa sasa" Hilo limemfanya ajione kuwa anapotea kisiasa akiwa bado kijana mdogo, uhuru wake umeminywa, hana jinsi. Anahitaji kujikuza kisiasa amebanwa mbavu na sasa hana jinsi.

Sasa basi hawa wanasiasa wanaohama upinzani wengi wao wamebanwa mbavu, wakitupiwa visenti kidogo tu wanayeyuka. Hata kina Tundu Lissu walipotaka kujinasua wakiwa huku upinzani waliishia kutwangwa risasi mchana kweupe tena hakuna kesi wala kuhoji na mbaya zaidi wala kuombea!

Hili linaonyesha wazi kuwa Rais Magufuli ni dikteta mbaya sana! Dikteta anayeiua Tanzania iliyokuwa imeanza kustawi kisiasa na Tanzania ya kuhoji! Huyu ni dikteta mbaya.

Naomba nimwambie wazi wazi Rais kuwa yeye alipatikana kirahisi sana kuwa mgombea wa CCM baada ya mtangulizi wake mzee JK kuruhusu serikali yake ichambuliwe, ikosolewe, ianikwe! Watuhumiwa wa ufisadi waliwekwa wazi, bunge liliwahoji na kupiga kelele hadharani. Hapa ndipo wanasiasa watarajiwa wa urais walianza kuonekana wachafu ndipo Magufuli akaibuka mbali na yeye kupewa uchafu wake. JK angekuwa mbinafsi kama alivyo Magufuli basi Urais angeusikia na kuuona maili milioni 100 kutoka alipo.


Sasa tunaona bunge halihoji tena, halipo huru, wanasiasa wanakosa majukwaa ya kisiasa huku chama dola kikitamalaki hapa kina Mtatiro lazima waibuke kama hawataweza kugangamala. Aibu ni kuwa leo Mtatiro anapokewa na yule yule aliyemsema kuwa ananunua wanaume wenzake! Asiogope kwani aibu ya upande huu kwa sasa ni dhaifu, aangalie tumbo lake. Zile siasa zake za face book na Twitter anaenda kuzitazama sijui tasemaje?

Sasa basi niitaadharishe hii CCM manunuzi kuwa walioenda huko wanaenda kutokana na kukosa namna. Huyu mtawala leo yupo kesho hayupo! Namna itarudi. CCM hii itavunjika vunjika, itapata shida sana.Kutakuwa na mparanganyiko mkubwa hapo mbele, najua wapo watakaobisha sasa ila tuombe uzima muda ambao si mrefu utakuja!

Hivi Kafulila, Mtatiro, Machali na wengine wanaunga mkono juhudi gani? Za rais kuonekana TBC kila mara? Maana aliyepita alikuwa hana huo muda! Za haya makelele tunayoyasikia kila mtendaji na kelele zake? Maana aliyepita alikuwa hana huo muda.

Nadhani gesi ya Mtwara ingegundulika kipindi cha Magufuli basi tusingelala maana wangehama kwa angalau kigezo kuwa "Amegundua gesi" "Wenzake walikuwa wanaikalia tu" Maana kama mtu anahama eti anasema kuwa Rais ameleta umeme wa Stiglers? Kweli? Eti amenunua ndege? Zinarejesha fedha zetu? Maana tulinunua kwa fedha zetu! Sasa kipi? Na hizo ndege angepewa bure si ndo tungewaomba wakenya wahamie Tanzania kuunga mkono juhudi?

Lakini pia tunapata funzo sasa kuwa watanzania wengi sana hawajaweza kujisimamia, kama hawa ambao wanaonekana afadhali wako tayari kujiacha utupu, vipi kwa wale kajamba nani? Tunapata ujumbe kuwa Tanzania bado haijawa na wanasiasa wengi waliokomaa. Ni aibu mtu anahama chama na hata kuuacha ubunge eti kwenda kuunga mkono Rais kujenga barabara! Aibu aibu! Lakini haya yote ni baada ya mbinu za kidikteta kutumika.
Hizi wishful thinking sijui zitaisha lini na kuanza siasa za ukweli? Kila siku watu wa upinzani wako ktk fantasy world.
 
hili nalo neno! Hadi JPM anaondoka kwakwel tutakuwa tumejua ipi ngano na yapi magugu kwa pande zote mbili
Tatizo hawa wahamaji hata hawafichi aibu. Hili linaonyesha wazi kuwa hawana namna. Ila Mtatiro kasema kuwa kwa sasa hana pa kusemea hivyo ameona akatafute pa kusemea.
 
Business Exchange Zone
Kama unahitaji huduma ama bidhaa yoyote, hapa ndio mahali sahihi na salama kwa ajili yako, sisi tunakukutanisha na wateja, wafanya biashara mbalimbali.
ANGALIZO. Malipo ya Huduma au Bidhaa zozote yatakayofanyika nje ya mfumo wetu hatutahusika nayo.
Business Exchange Zone
 
Kinachomiandama ni laana ya dakta Slaa kumtema mzee wa watu kwa karanga za kuonja.
Hapana, hakuna laana hapa ni matokeo ya machaguo yao. Lkn pia ni namna Mungu alivyo amuwa kumuweka hai hadi sasa vinginevyo kama angebaki upande ule, kundi la Magu la wasio julikana lingesha ivuna roho yake zamani.
 
Back
Top Bottom