Kuna rocket imetumwa huko angani ikagonge mwamba unaohatarisha kugonga dunia

Vijana wa bongu ujuaji Mnapinga hata tu. Hata hoja kidogo hamna

Tunaifa la hovyo sana
Hivi katika hii mada ulivyo isoma hujajiuliza chochote kuhusu ukweli wa mada husika au umependa stori na picha ?

Mimi nilivyo soma hii mada cha kwanza nilianza kuhoji au kujiuliza juu ya picha ukiangalia kwa umakini hizo picha ni picha bunifu hakuja picha hata moja ambayo ni halisi.

Kingine kuhusu vipimo na utoaji wa majina na maelezo ya jambo husika,maelezo yanaonyesha ya kuwa wahusika hawana maarifa sahihi juu ya anga na vilivyomo. Swali la msingi nililo jiuliza ni kuwa wametumia mchakato gani kujia ukubwa wa hilo jiwe ?

Nani wa kwanza kutambua uwepo wa jiwe hilo na ilikuwa lini na alijuaje kuhusu jiwe hilo ?
 
waache kujipa kiki hao jamaa!!Dunia italindwa na yule alieitengeneza Dunia ilivyo!!!!Tena wasije wakafanya yao wakidhani wanatengeneza kumbe ndio majanga yakazidi kwa Dunia!!Hekima ya Binadamu ni upumbavu kwake yeye alieitengeneza Dunia!!WATAJUAJE KAMA HILO JIWE NDIO NGUZO YENYE KANI ISABABISHAYO UTULIVU KWA SAYARI ZOTE???
Mwana kulitafuta,mwana kulipata! Bado Corona walioichokonoa uko China haijatuacha!!
 
Ukisoma comments za humu na ukaambiwa Hawa ni watu wazima wenye makende yaliyokomaa unaweza ukachoka Aisee,
Hivi wabongo aliyewafundisha ujuaji ni nani?
Watu wapo field wanapiga kazi watu Kama nyie kutoka huko Nanjilinji na namtumbo mmeshika simu za android kupinga project za wanaume wa kazi et AAA uongo,chai,haiwezekani,
bla bla za Mungu wenu sijui kufuru,wanamjaribu Mungu,Mungu Ndie atakaye tulinda,huo ni mpango wa ibilisi sijui hawatafanikiwa!
Daaaaaaa inasikitisha Sana!

Maujinga tu yapo vichwani mwenu Tena wengine ni members ambao hua naona angalau kidogo akili zenu zinachaji kumbe likija swala la kisayansi lakugusa dini zenu mnajulikana Kwa ujuha wenu
Shwain!

Elimu! Elimu!Elimu!
 
Wakati huohuo viongozi wa Tanzania wakiwaza jinsi ya kupambana na tatizo la maji na umeme ndani ya miaka 60 ya uhuru👇😁😁😁
1637308571637308570.jpg

4321image12.png
 
Kuna faida gani katika kuwekeza katika maigizo zaidi ya kujitekenya na kucheka mwenyewe. Maana ya maigizo ni kuongeza au kupunguza katika uhalisia bora uendelee kuwa maskini na nyuma kimaendeleo ila ukaishi katika uhalisia kuliko kuishi katila maigizo na kufurahisha mioyo yao.

Katika Sayansi iliyo feli na iliyo kaa kimaigizo ni Sayansi ya anga,kwayo mtu unakuwa na maswali ambayo hayajibiki wala wanaofanya tafiti za anga hawajahi kufikiria.

Endapo mtu ukiwa ni mwenye tabis ya kufikiri japo kidogo utapata maswali ambayo hayajibiki. Shida ya wengi wanapenda kuona wenye mambo yao washajua ya kuwa watu wanapenda kuona sana kuliko kuhoji,basi wahusika wanawaonyesha tu. Teknolojia imefika mbali sana na watu hawahoji juu ya teknolojia,mtu akifanya animation utajuaje akitengeneza picha utajuaje ila ukiwa mtu wa kuhoji uongo lazima ujitenge.

Ukiijadili hii mada kwa jicho la uhojaji na elimu hutapata uhalisia hata mmoja zaidi ya sanaa tu.
Umeongea point shida yetu hatuko huru kimawazo kwasababu tunatetea vile tulivyoaminishwa kuwa ndivyo vilivyo na tunapinga vile ambavyo vipo nje ya kile tunavyovifahamu au tulivyoaminishwa ni kama tuko programmed naamini ukweli wa kila jambo upo ndani yetu haya ya nje ni kama milunzi mingi usipojitambua itakupoteza.
 
waache kujipa kiki hao jamaa!!Dunia italindwa na yule alieitengeneza Dunia ilivyo!!!!Tena wasije wakafanya yao wakidhani wanatengeneza kumbe ndio majanga yakazidi kwa Dunia!!Hekima ya Binadamu ni upumbavu kwake yeye alieitengeneza Dunia!!WATAJUAJE KAMA HILO JIWE NDIO NGUZO YENYE KANI ISABABISHAYO UTULIVU KWA SAYARI ZOTE???
walokole utawajua tu
 
Ukisoma comments za humu na ukaambiwa Hawa ni watu wazima wenye makende yaliyokomaa unaweza ukachoka Aisee,
Hivi wabongo aliyewafundisha ujuaji ni nani?
Watu wapo field wanapiga kazi watu Kama nyie kutoka huko Nanjilinji na namtumbo mmeshika simu za android kupinga project za wanaume wa kazi et AAA uongo,chai,haiwezekani,
bla bla za Mungu wenu sijui kufuru,wanamjaribu Mungu,Mungu Ndie atakaye tulinda,huo ni mpango wa ibilisi sijui hawatafanikiwa!
Daaaaaaa inasikitisha Sana!

Maujinga tu yapo vichwani mwenu Tena wengine ni members ambao hua naona angalau kidogo akili zenu zinachaji kumbe likija swala la kisayansi lakugusa dini zenu mnajulikana Kwa ujuha wenu
Shwain!

Elimu! Elimu!Elimu!
Tunawasiwasi na matokeo ya hizo tafiti zenu za ki sayansi, maana lolote lile linawezekana,unaweza pata matokeo chanya au matokeo hasi! Na hiyo ndiyo maana ya tafiti unajaribu kitu usichokijua matokeo yake yatakuwaje!!
 
waache kujipa kiki hao jamaa!!Dunia italindwa na yule alieitengeneza Dunia ilivyo!!!!Tena wasije wakafanya yao wakidhani wanatengeneza kumbe ndio majanga yakazidi kwa Dunia!!Hekima ya Binadamu ni upumbavu kwake yeye alieitengeneza Dunia!!WATAJUAJE KAMA HILO JIWE NDIO NGUZO YENYE KANI ISABABISHAYO UTULIVU KWA SAYARI ZOTE???
Umeandika kwa kutumia maarifa yepi? Dini? Uraia? Uchumi? Au uwezo wako tu wa kufikiri? Kz kifuatacho utaanza kusema hata zile satellites wanazituma Mars siyo kweli.. Nijuavyo hii project ya kujifunza ku-diverge miamba mikubwa imeanza miaka mingi--- sasahivi wapo kwa testing the implementation..
Na siku nilipojua kuwa ndugu wanamonitor kila asteroid angani kupitia deep space network zao za Spain, Australia na Carlifornia, na wanapeana shifts kama intern Doctor hospitalini, siku ile ndo nikajifuta macho na kujiuliza what role am i playing hapa duniani?
Acha sisi tuendelee kubeza ila ukweli ni kwamba people are very serious!
 
Title yako imekaa kishabiki shabiki na kiumbea umbea mno. Unnecessary sensationalism!

Wanasayansi wanaamini kuwa huko nyuma dunia ilishawahi kugongwa na mawe haya makubwa (asteroids) na wana ushahidi huo. Jiwe la mwisho ni hili lililoua viumbe wengi duniani na kuondoa ufalme wa akina dinosaurs; na wanyama wengine lukuki.

Mawe haya yanasafiri kwa kasi ya ajabu na yanapopiga uso wa dunia yanavuvumua vumbi na uchafu mwingi ambao unaweza kubakia angani kwa miaka mingi. Vumbi na uchafu huu huenea dunia nzima na kuziba miali ya jua kabisa kabisa mpaka dunia inaingia katika kile wanachokiita deep freeze. Ina maana dunia inaganda kabisa na kutandwa na barafu kwa vile hakuna mwanga wa jua kwa muda mrefu. Na bila mwanga wa jua ina maana hakuna photosynthesis wala nishati ya aina yo yote. Matokeo yake ni vifo vya jumla kwa viumbe wengi.

Yapo mawe yanayoonyesha kuwa yatakuja kuipiga dunia huko mbele ya safari na NASA wana kitengo maalum kinachoshughulika na tatizo hili na mpaka sasa kuna nadharia tatu zilizopendekezwa kuweza kujiponya siku ikigundulika kuwa kuna jiwe linatujia huko:

1. Kurusha chombo chenye uzito na nishati maalum na kwenda kuligonga hilo jiwe huko angani likiwa mbali na dunia. Lengo hapa siyo kulisambaratisha bali ni kujaribu kulisukuma kidogo (nudge) ili liweze kuacha njia yake ya mzunguko (orbit) na hivyo kuliepusha kugongana na dunia.

2. Kurusha rocket yenye nguvu iliyobeba bomu kubwa la nyuklia na kwenda kulitandika hilo jiwe na kulisambaratisha. Hii hata hivyo inaweza tu kuishia kulimega hilo jiwe katika vipande vingi ambavyo vinaweza kuleta hatari zaidi duniani. Na kukitokea mushkeli wakati wa kurusha hiyo rocket hilo bomu linaweza kuturipukia hapa hapa duniani na kuleta madhara makubwa.

Ili kuepuka kulimega vipande vipande lipo pendekezo la kwenda kulipua bomu hilo karibu na jiwe hilo. Ile nguvu ya mripuko (boom) inaweza kutosha kulisukuma kidogo likiwa zima na kuliondoa katika orbit yake.

3. Kurusha chombo chenye monzi mikali ya laser na kwenda kujaribu kulimulika jiwe hilo na mionzi hiyo. Mawe haya mengi yana barafu iliyoganda na likipigwa na mionzi mikali kwa muda barafu inaweza kuyeyuka na hivyo kupunguza uzito wake na hii, wanadai, inaweza kusababisha liondoke kwenye orbit yake inayolifanya ligongane na dunia.

Hata bila kuyeyusha barafu yake, mionzi hii ya laser inaweza kufanya kazi sawa na utando wa buibui na hivyo kulisogeza jiwe hilo polepole nje ya orbit yake na hivyo kuepusha mgongano wake na dunia.

NASA leo wamerusha chombo kujaribu nadharia ya kwanza kama inafanya kazi kwa sababu dunia kupigwa na asteroid nyingine ni suala la muda tu. Elon Musk anarusha maroketi haya kila leo hatusikii cho chote lakini leo umeshusha ushabiki wa kufa mtu eti anga lilibadilika. Lilibadilika wapi? Labda kama ulikwenda kushuhudia wakati roketi hilo likirushwa huko California. Ni wazi hii habari hukuiandika mwenyewe na umefanya plagiarism mahali fulani (BBC Swahili) na sina uhakika kama una ufahamu wa kutosha na habari yenyewe pamoja na implications za kiujumla za kinachozungumziwa.

Wakati tunahangaika na tozo, ufisadi wa kutisha, kutengeneza madawati, kujenga nyumba za walimu, kujenga vyoo vya shimo vya kutosha mashuleni, ushirikina, ukosefu wa umeme na maji, siasa za hovyo za kuoneana hizi, wenzetu huko hawalali wanahangaika na mambo kama haya mazito. Tuombe wafanikiwe kwa sababu siku moja pengine wataweza kuokoa maisha ya viumbe hapa duniani. Hata wakishindwa wao pia wanahangaika kutafuta makazi katika sayari zingine huko wanaweza wakaondoka zao na kutuacha hapa siku mambo yakibumburuka!
Nimekukubali mzee.. Ukweli ni kwamba watu wapo serious na haya maisha, na hii dunia yetu.
 
Hili ni dili la kuchota matrillion kwa kutishiana vitu ambavyo havipo, hapa nchi zote tutachangishwa pesa kwa madai wanarusha makombora ya kulipiga hilo jiwe, kumbe wanarusha sattelite zao tu, na mchango tunalipishwa
Lini ulishalipishwa pesa!? Tuna pesa za kuwalipa NASA kweli!!?? Wakati mwingine ni vema tukawa wasomaji na watazamaji tu.
 
Umeandika kwa kutumia maarifa yepi? Dini? Uraia? Uchumi? Au uwezo wako tu wa kufikiri? Kz kifuatacho utaanza kusema hata zile satellites wanazituma Mars siyo kweli.. Nijuavyo hii project ya kujifunza ku-diverge miamba mikubwa imeanza miaka mingi--- sasahivi wapo kwa testing the implementation..
Na siku nilipojua kuwa ndugu wanamonitor kila asteroid angani kupitia deep space network zao za Spain, Australia na Carlifornia, na wanapeana shifts kama intern Doctor hospitalini, siku ile ndo nikajifuta macho na kujiuliza what role am i playing hapa duniani?
Acha sisi tuendelee kubeza ila ukweli ni kwamba people are very serious!
Wabongo sisi kwa kuwa hakuna tunachokijua,basi tumebaki kupinga tu.wenzetu wako busy kuilinda dunia.
 
Bado watu wengi wanaamini kwamba dunia ni flat, yaani kama uwanja wa mpira - na ngumu kuamini kuna eti sayari nyingi zinazunguka jua bila kugongana miaka mabillion kwa mabillion. Wachache wameanza kuamini ni duara baada ya kuona kwenye TV watu wa Asia ama marekani wanashangilia mwaka mpya ili hali sisi bado tumelala ama mchana kweupe.

Hii sayansi ya unajimu kwa mtu asiyeelewa ni kama unamwelezea uchawi.

Kwangu mie habari hii n i njema na nasubiri na sisi Watanzania ni lini tutarusha satellite yetu kwenye anga za mbali kufanya security ya dunia nikingali hai.
 
Nimegundua Wabongo wengi ni watu wapumbavu na wajinga wajinga sana ndio maana ni maskini nadhani hatuna elimu stahiki na tumekua brainwashed na imani wakati imani yenyewe inasema tutumia maarifa ku solve problem

Huwezi kaa tu ukatengemes imani itakuponya kama hujitumi kwa maarifa ulionayo ebu tujifunze jamani tupate elimu ya vitu tuache kusema wazungu ni waongo wakati wanafanikiwa kupitia maarifa yao
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom