GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,278
- 6,672
Ijumaa nilikuwa kwenye bar moja inaitwa TAXIDO, Nikiwa mwenye mawazo
tele niliona hiyo kama ni sehemu Muafaka ya kupunguza mawazo kwani kila
Ijumaa huwa kuna LIVE BAND zinapiga hapo na nyimbo zao nyingi huwa
zilipendwa.
Nikiwa hapo niliagiza Nyama choma ya mbuzi ambayo ilikaushwa vizuri kwenye
moto na wataalamu wa kuchoma nyama, niliwekewa pilipili ya kutosha ndimu na
Kachumbari iliyotengenezwa kwa ustadi mkubwa sana nikashushia kwa Soda.
Katika kaa yangu ya hapo niligundua wanywaji wa Bia/pombe walikuwa na
Furaha sana, yaani wengi walichangamka tofauti na nilivyowaona wakati wanaingia.
Halafu ni watu naona kama wanajiamini katika mazungumzo ya mipango yao.
Naomba nifahamishwe Uzuri unaopatikana kwenye Bia kabla sijakata shauri ya kuanza
kunywa. Kiukweli natamani Ijumaa Ijayo nianze angalau na Bia tano au ile Chupa
ndogo ya Konyagi.
Vipi kuna ubaya wowote kuanza unywaji wakati nishakuwa Mtu mzima hivi?
tele niliona hiyo kama ni sehemu Muafaka ya kupunguza mawazo kwani kila
Ijumaa huwa kuna LIVE BAND zinapiga hapo na nyimbo zao nyingi huwa
zilipendwa.
Nikiwa hapo niliagiza Nyama choma ya mbuzi ambayo ilikaushwa vizuri kwenye
moto na wataalamu wa kuchoma nyama, niliwekewa pilipili ya kutosha ndimu na
Kachumbari iliyotengenezwa kwa ustadi mkubwa sana nikashushia kwa Soda.
Katika kaa yangu ya hapo niligundua wanywaji wa Bia/pombe walikuwa na
Furaha sana, yaani wengi walichangamka tofauti na nilivyowaona wakati wanaingia.
Halafu ni watu naona kama wanajiamini katika mazungumzo ya mipango yao.
Naomba nifahamishwe Uzuri unaopatikana kwenye Bia kabla sijakata shauri ya kuanza
kunywa. Kiukweli natamani Ijumaa Ijayo nianze angalau na Bia tano au ile Chupa
ndogo ya Konyagi.
Vipi kuna ubaya wowote kuanza unywaji wakati nishakuwa Mtu mzima hivi?