Kuna nini KCMC?

tankibovu

Member
Jan 5, 2010
42
16
Miaka 30 na iliyopita mtumishi wa Mungu Askofu Stephano Moshi wa KKKT alipata maono...Kilimanjaro Christian Medical Centre kwa kushirikiana na wengine akiwemo Prof Otto Walter hospitali hii mashuhuri na aina yake ikajengwa...ikakua.
Leo hii KCMC imekuwa makao ya mapepo na wachawi wenye uchu wa madaraka , mafisadi. Prof John Shao anainajisi KCMC ili kulinda cheo chake. Waganga wapiga ramli wanacheza na kuweka tunguli, kisa cheo!


Prof Shao amekuwa kiongozi hapa kwa zaidi ya miaka 10. Mwanzoni alifanya mema sasa hivi amenogewa hataki kuondoka...patamu pesa, wanawake, madaraka.
KCMC imekuwa danguro....viongozi kuzaa na watumishi...hakuna maadili tena. Waliokuwa wakisali kutwa kwa ajili KCMC wameondoka , wamestaafu...msarakambo
1. Prof Shao mwaka 2006 alifukuza kundi la madaktari bingwa waliohoji ukomo wa uongozi wake. Watu hawa wakiwemo Dr Ole, Prof Mlay...walijitolea muda kufundisha chuo cha madaktari na kuiweka KCMC ilipo.
kosa lao ..walihoji uongozi wa Shao kila mmoja ...alisambaratishwa..Mbeya rufaa mradi mabingwa walijikuta wakiwa njiani..

2. Kwa kushirikiana na watiifu wachache amekuwa akijipatia 10% toka kila mradi wa research.

3. TAKUKURU mwaka 2009 walifanya utafiti na kukuta uozo mkubwa katika ulaji wa mishahara ya serikali na forgery ya majina ya watumishi wanaolipwa na serikali. kwa mfano Dr Anna Mushi aliyeondoka siku nyingi KCMC eti hadi 2009 yuko kwenye payroll wengine hata marehemu.

4. Viongozi wa Wizara wanapolalamikiwa wakifika KCMC huzibwa midomo kwa pesa..

5. Viongozi wa kanisa nao wametumbukia kwenye mkumbo hupewa fedha nao hukaa kimya.

6. Wastaafu watumishi wa KCMC karibu wote wanalia na kusaga meno hakuna mfumo wa pensheni zao zimepotea.
7. Mwanae asiyejua kukamilisha sentensi ya kiingereza anapewa cheo cha u head wa IT, jamani muogopeni Mungu.

Prof Shao ni mungu mtu hakuna wa kumgusa si Ask Malasusa wala nani anaendesha KCMC anavyotaka.

Ndugu zangu tuiombee KCMC

Sasa baada ya kashfa ya TAKUKURU 2009...amefukuza madakatari wengine bingwa akiwa na wasiwasi nao...

Hii ndio KCMC ya vitisho, mambo ya giza, ubadhirifu wa pensehni n.k
 
Du..inasikitisha sana...Watu wenye taaluma za heshima wanapoanza kusahau jamii walimo na kujifikiria binafsi, aidha kutumia vyeo walivyo navyo kuwatesa watu wa chini yao.

Nijuavyo KCMC ilikuwa ni hospitali iliyojijengea heshima sana machoni pa jamii ya kitanzania, Africa na Dunia nzima, kwa habari ya tiba, taaluma na huduma.

Lakini mleta mada, embu weka sawa mambo hapa, je baada ya kuja TAKUKURU, matokeo yake ninini? au nao ndo wamefumbwa mdomo na huyu daktari mkuu?

Tumieni machinery zinginezo kumuumbua huyu jamaa bana, kuna altenative ambazo dakika tu yuko chali!...huwezi kuiweka hospitali mahala pa ugagura... shit!
 
Thats sad, malalmiko ya huyu bwana yamezidi sana hapa moshi. Wampe Dr. M. Swai aiongoze ambaye ndio director hivi sasa
 
Tankibovu hata salamu mkuu, naona umeingia moja kwa moja na attack. Haya karibu.
 
Salama mkuu,
mambo mengine yanakuwa ovyo sana. Hii ni aibu kwa institution ya kanisa.
 
kwako Tankibovu na Nyivonduma nyinyi nyote ni wamoja rejea tarehe yakujiunga nasi jamiiforums,
inawezekana kukawa na tatizo la uendeshaji lakini namna ulivyowasilisha maoni yako ni kama mashambulizi binafsi........Tupe report ya TAKUKURU Iliishia wapi, tueleze je Pro Shao anamalaka yakumuhaishia daktari kwenda rufaa Mbeya ama hospitali nyingine ya rufaa hapa Tz, je Askofu anaweza kuwaziba midomo wafanyakazi wa Wizara ya afya kwa maslahi gani anayowapa ?
 

Heshima kwako Tankibovu,

Kwanza karibu jamvini naona umeingia bila hata hodi.

Nimesoma kwa makini hoja ulizoleta kwa kweli zinasikitisha sana kama ni kweli mambo yako hovyo kiasi hicho.Nakumbuka miaka ya nyuma KCMC ilipokuwa chini serekali hali ilikuwa mbaya na ya kusikitisha lakini kama sijakosea Good samaritan waliporejeshewa KCMC ilianza kubadilika kuanzia usafi na matengenezo makubwa yalifanyika.

Mara nyingi Hospitals na shule zinazoendeshwa na kanisa zimekuwa zikitoa huduma nzuri,nashindwa kuamini imnakuwaje tena KKKT dayosisi ya kaskazini chini ya Askofu Shayo na mkuu wa kanisa KKKT Askofu Malasusa kushindwa kusimamia KCMC.

Kuna wakati nilisikia pia mgogoro kati ya Prof Shayo na baadhi ya madaktari bingwa sijui mgogoro umeishia wapi na ulikuwa kwa manufaa ya nani.

KKKT makao makuu kwa maana ya katibu mkuu ambae ni mtendaji mkuu wa shughuli za uendeshaji za kanisa hasa miradi wajaribu kuliangalia suala la KCMC kwa karibu.Sina hakika kama KCMC iko chini ya dayosisi ya kaskazini [Kilimanjaro] au ni mradi unaosimamiwa kitaifa kwa maana ya makao makuu ya KKKT.Tafadhali yoyote anayehusika asichelewe kushughulika na matatizo ya KCMC kwasababu yanahusiana na uhai wa watu.
 
Kwa kirefu KCMC= Kilimanjaro Christian Medical Centre. Hii ilikuwa ni hospital nzuri/bora kupita hata Muhimbili Hospital Kipindi kirefu sana. Kulikuwa na dedicated doctors and sistrers. Ilikuwa inapata misaada mingi kwa msamaria mwema (Lutheran agency ya nje) na serikali pia. Hata kwa sasa nafikiri kuna wafanyakazi wa kanisa pale ambao wanalipwa na msamaria na wale ambao wanalipwa 100% na serikali.

Hali ya KCMC iliharibika zaidi pale serikali ilipopunguza wafanyakazi wake (health sector reforms 1990s) kwa kuwa ilikuwa haina uwezo wa kuwalipa wote na kwa sababu walikuwa wanahitajika basi wengine walipewa hiari wachague kustaafu then waajiriwe kwa mkataba kwa msamaria au kuondoka kabisa baada ya mafao. Hivyo walikubali mafao ya serikali na kupata ajira mpya kwa mkataba kwa msamaria na wengine (waliobakishwa na serikali) kuendelea kulipwa na serikali kuu, i.e permanent and pensionable.

Uongozi tangu wakati huo, haukuwa wa kuridhisha tena. Kama alivyosema mleta mada Prof. Shao alihamisha wale madaktari wote ambao alijua watamtia hofu asiweze kufisadi kwa urahisi. Heshimika sana Dr. Johh Lyimo wa mifupa. Dr. Ikamba, Dr. Nkya, Dr. Eshleman na mkewe, Prof. Swai, Prof. Shayo, Dr. Saitoria, na wengine wengi. Baadhi yao pengine watakuwa wameitwa mbele ya haki ila kundi hili na wale ambao walikuwa na kundi hili ambao siwakumbuki walikuwa dedicated sana.

Sijafika KCMC kwa muda mrefu kiasi, na sijaelewa hali pale tena iko vipi.

I cry for you KCMC.
 
kwako Tankibovu na Nyivonduma nyinyi nyote ni wamoja rejea tarehe yakujiunga nasi jamiiforums,
inawezekana kukawa na tatizo la uendeshaji lakini namna ulivyowasilisha maoni yako ni kama mashambulizi binafsi........Tupe report ya TAKUKURU Iliishia wapi, tueleze je Pro Shao anamalaka yakumuhaishia daktari kwenda rufaa Mbeya ama hospitali nyingine ya rufaa hapa Tz, je Askofu anaweza kuwaziba midomo wafanyakazi wa Wizara ya afya kwa maslahi gani anayowapa ?

I agree! Hata kama kuna matatizo katika utendaji wa KCMC, shambulio kama la kwako ni kosa kisheria linalojulikana kama "slander" au "defamation of character", na linalo potential ya kufuatiliwa kisheria kwa kuwa umezusha tuhuma za uhalifu. Elezea una uthibitisho gani ya kusupport madai yako. Pia, una jibu gani hasa ya yale maswali aliyouliza nguvumali?!?

Unafikiri sentensi kama
"leo hii KCMC imekuwa makao ya mapepo na wachawi ... mafisadi. ... anainajisi KCMC... Waganga wapiga ramli wanacheza na kuweka tunguli, kisa cheo!"
... zinakuongezea credibility ama zinatufanya tutilie mashaka nia zako na uwezo wako wa kusababu? Leta mada yako kiutu-uzima ili tukuamini. JF siyo "KIU" au "Ijumaa"!
 
Tankibovu anawasilisha hoja kwa kusema,

Leo hii KCMC imekuwa makao ya mapepo na wachawi wenye uchu wa madaraka , mafisadi

KCMC imekuwa danguro....viongozi kuzaa na watumishi...hakuna maadili tena.Waliokuwa wakisali kutwa kwa ajili KCMC wameondoka , wamestaafu...msarakambo

4. Viongozi wa Wizara wanapolalamikiwa wakifika KCMC huzibwa midomo kwa pesa..

5. Viongozi wa kanisa nao wametumbukia kwenye mkumbo hupewa fedha nao hukaa kimya.
Karibu sana hapa JF.

Unaweza kuwa una hoja za msingi katika kile unachotaka kukiwasilisha lakini nakuwa na wasiwasi juu ya ama maandishi yako yanayokuwa ya majumuisho (generalized statements) na pengine yanayoweza kuonekana kama kuongeza chumvi hivi. Mfano unaweza kutuhakikishia hapa kuwa :

1. KCMC sasa ni makao makuu ya mapepo na wachawi

2. KCMC imekuwa danguro au unataka kusema kuwa kuna kiongozi au viongozi fulani wachache (na uwataje) wana na tabia za uasherati au yanayofanana na hayo.

3. Viongozi wa Wizara kuzimwa na KCMC kwa pesa

4. Viongozi wa Kanisa nao kuzimwa kwa kupewa pesa


Ebu kuwa specific na bila kujaribu ku-dramatize situations ili ueleweke na kuchukuliwa serious katika kile unachowasilisha; vinginevyo utaitwa mzushi au na wewe kutuhumiwa kuwa unakashifu watu au taasisi mfano umewezaje kujua makao makuu ya mapepo unless unataka kutuambia kuwa nawe ni mwanachama wa makao yake madogo au una utaalamu fulani wa kuyaona makao yote ya mapepo na wachawi na una orodha yake.

Haya pitia tena taarifa yako na uiwasilishe vyema ili binafsi nipate tukusome vyema na kuchangia ipaswavyo.
 
Miaka 30 na iliyopita mtumishi wa Mungu Askofu Stephano Moshi wa KKKT alipata maono...Kilimanjaro Christian Medical Centre kwa kushirikiana na wengine akiwemo Prof Otto Walter hospitali hii mashuhuri na aina yake ikajengwa...ikakua.
Leo hii KCMC imekuwa makao ya mapepo na wachawi wenye uchu wa madaraka , mafisadi. Prof John Shao anainajisi KCMC ili kulinda cheo chake. Waganga wapiga ramli wanacheza na kuweka tunguli, kisa cheo!


Prof Shao amekuwa kiongozi hapa kwa zaidi ya miaka 10. Mwanzoni alifanya mema sasa hivi amenogewa hataki kuondoka...patamu pesa, wanawake, madaraka.
KCMC imekuwa danguro....viongozi kuzaa na watumishi...hakuna maadili tena. Waliokuwa wakisali kutwa kwa ajili KCMC wameondoka , wamestaafu...msarakambo
1. Prof Shao mwaka 2006 alifukuza kundi la madaktari bingwa waliohoji ukomo wa uongozi wake. Watu hawa wakiwemo Dr Ole, Prof Mlay...walijitolea muda kufundisha chuo cha madaktari na kuiweka KCMC ilipo.
kosa lao ..walihoji uongozi wa Shao kila mmoja ...alisambaratishwa..Mbeya rufaa mradi mabingwa walijikuta wakiwa njiani..

2. Kwa kushirikiana na watiifu wachache amekuwa akijipatia 10% toka kila mradi wa research.

3. TAKUKURU mwaka 2009 walifanya utafiti na kukuta uozo mkubwa katika ulaji wa mishahara ya serikali na forgery ya majina ya watumishi wanaolipwa na serikali. kwa mfano Dr Anna Mushi aliyeondoka siku nyingi KCMC eti hadi 2009 yuko kwenye payroll wengine hata marehemu.

4. Viongozi wa Wizara wanapolalamikiwa wakifika KCMC huzibwa midomo kwa pesa..

5. Viongozi wa kanisa nao wametumbukia kwenye mkumbo hupewa fedha nao hukaa kimya.

6. Wastaafu watumishi wa KCMC karibu wote wanalia na kusaga meno hakuna mfumo wa pensheni zao zimepotea.
7. Mwanae asiyejua kukamilisha sentensi ya kiingereza anapewa cheo cha u head wa IT, jamani muogopeni Mungu.

Prof Shao ni mungu mtu hakuna wa kumgusa si Ask Malasusa wala nani anaendesha KCMC anavyotaka.

Ndugu zangu tuiombee KCMC

Sasa baada ya kashfa ya TAKUKURU 2009...amefukuza madakatari wengine bingwa akiwa na wasiwasi nao...

Hii ndio KCMC ya vitisho, mambo ya giza, ubadhirifu wa pensehni n.k
Kama kweli kweli. Nani anayefaa basi? Jamani. Wajinga ndio waliwao.
 
Nimepata habari zisizo rasmi (msinishambulie) kuwa manesi wa KCMC sasa wako kwenye mgomo tangu jana wamekaa nje. Sijajua ni manesi wa daraja gani, yaani NURSE OFFICERS/ MIDWIVES au NURSE ASSISTANTS/WARD ATTENDANTS.

Tanki bovu inaelekea wewe ni mfanyakazi hapo, tafadhali tujulishe yanayojiri na nini chanzo cha mgomo?
 
Miaka 30 na iliyopita mtumishi wa Mungu Askofu Stephano Moshi wa KKKT alipata maono...Kilimanjaro Christian Medical Centre kwa kushirikiana na wengine akiwemo Prof Otto Walter hospitali hii mashuhuri na aina yake ikajengwa...ikakua.
Leo hii KCMC imekuwa makao ya mapepo na wachawi wenye uchu wa madaraka , mafisadi. Prof John Shao anainajisi KCMC ili kulinda cheo chake. Waganga wapiga ramli wanacheza na kuweka tunguli, kisa cheo!


Prof Shao amekuwa kiongozi hapa kwa zaidi ya miaka 10. Mwanzoni alifanya mema sasa hivi amenogewa hataki kuondoka...patamu pesa, wanawake, madaraka.
KCMC imekuwa danguro....viongozi kuzaa na watumishi...hakuna maadili tena. Waliokuwa wakisali kutwa kwa ajili KCMC wameondoka , wamestaafu...msarakambo
1. Prof Shao mwaka 2006 alifukuza kundi la madaktari bingwa waliohoji ukomo wa uongozi wake. Watu hawa wakiwemo Dr Ole, Prof Mlay...walijitolea muda kufundisha chuo cha madaktari na kuiweka KCMC ilipo.
kosa lao ..walihoji uongozi wa Shao kila mmoja ...alisambaratishwa..Mbeya rufaa mradi mabingwa walijikuta wakiwa njiani..

2. Kwa kushirikiana na watiifu wachache amekuwa akijipatia 10% toka kila mradi wa research.

3. TAKUKURU mwaka 2009 walifanya utafiti na kukuta uozo mkubwa katika ulaji wa mishahara ya serikali na forgery ya majina ya watumishi wanaolipwa na serikali. kwa mfano Dr Anna Mushi aliyeondoka siku nyingi KCMC eti hadi 2009 yuko kwenye payroll wengine hata marehemu.

4. Viongozi wa Wizara wanapolalamikiwa wakifika KCMC huzibwa midomo kwa pesa..

5. Viongozi wa kanisa nao wametumbukia kwenye mkumbo hupewa fedha nao hukaa kimya.

6. Wastaafu watumishi wa KCMC karibu wote wanalia na kusaga meno hakuna mfumo wa pensheni zao zimepotea.
7. Mwanae asiyejua kukamilisha sentensi ya kiingereza anapewa cheo cha u head wa IT, jamani muogopeni Mungu.

Prof Shao ni mungu mtu hakuna wa kumgusa si Ask Malasusa wala nani anaendesha KCMC anavyotaka.

Ndugu zangu tuiombee KCMC

Sasa baada ya kashfa ya TAKUKURU 2009...amefukuza madakatari wengine bingwa akiwa na wasiwasi nao...

Hii ndio KCMC ya vitisho, mambo ya giza, ubadhirifu wa pensehni n.k

Duu,are yuo sure of that?how do you measure uchawi?
 
Duu,are yuo sure of that?how do you measure uchawi?
Nafikiri ametumia uchawi kujua yote ya uchawi hapo...KCMC
icon10.gif
 
no comments!!!! mleta mada angewasilisha malalamiko yake makao makuu ya KKKT kwanza, au Kwa katibu mkuu wizara ya afya na pia kuyarudisha takukuru. These direct attacks are to serious and sensitive.
 
...ni kweli malalamiko juu ya prof shao yapo....ni bora maaskofu wa KKKT wakamuonesha mlango wa kutokea sasa....wawaache good samaritan wafanye kazi....
 
Du nilikuwa sijaiona hii.
Dr. Mtwangambate, G, mbona tulikubaliana pamoja ulipotaka ushauri akiwepo na Dr. Kileo kuwa tuwasiliane kwanza kabla ya kushusha haya mambo mazito bila uchunguzi wa kutosha? Jamii ina habari kamili yaana umeongea yaliyo ya kweli lakini kuna mengi ya uongo kabisa. Na mwishowe utaonekana kuwa ni uzushi kwa kila uliloandika sasa.
Mzee kwa mwendo huu naona hata hapa chuoni (katika masomo yako ya juu) uliyoanza yatakushinda sasa.
 
Du nilikuwa sijaiona hii.
Dr. Mtwangambate, G, mbona tulikubaliana pamoja ulipotaka ushauri akiwepo na Dr. Kileo kuwa tuwasiliane kwanza kabla ya kushusha haya mambo mazito bila uchunguzi wa kutosha? Jamii ina habari kamili yaana umeongea yaliyo ya kweli lakini kuna mengi ya uongo kabisa. Na mwishowe utaonekana kuwa ni uzushi kwa kila uliloandika sasa.
Mzee kwa mwendo huu naona hata hapa chuoni (katika masomo yako ya juu) uliyoanza yatakushinda sasa.

Kwahiyo wewe ndiye Dr Shao na mleta mada Dr Mtwangambate,G?
 
Back
Top Bottom