Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 36,283
- 43,718
Tangu Taliban kutwaa mamlaka ya kuitawala nchi ya Afghanistan wiki hii memes za kusherehesha utawala huo muovu, katili na wa kijuha zimekuwa nyingi na zimetrend kila kona ya mitandao.
Hawa wabongo wanaotengeneza memes na kusambaza video za Taliban wanaelewa utawala wa Taliban unamaanisha nini kwa raia wengi wa Taliban hasa wanawake na watoto wa kike wanaotaka kuishi maisha ya kawaida kama binadamu wengine waliostaarabika duniani?
Wanafahamu itakuwa lazima wanaume wote kufuga ndevu, wenye michepuko na wanaoishi bila kuona watapigwa mawe mpaka kufa, wezi watakuwa wanakatwa mikono, wanawake hawatashiriki katika uongozi tena, ni lazima wavae hijab au niqab, lazima watoke na mwanaume wakienda kutembea, pombe haitanyweka tena hadharani lakini biashara ya dawa za kulevya za heroine zitashamiri kwa sababu Taliban ni wakulima wazuri wa mihadarati ya opium!
Ni aibu na ujuha kusherekea na kusherehesha utawala katili wa Taliban. Ni bahati mbaya sana kuwa na taifa lenye majuha wengi wanaochukuliwa na upepo wa kila aina matukio yanayotrend bila kuwa na maarifa.
Hawa wabongo wanaotengeneza memes na kusambaza video za Taliban wanaelewa utawala wa Taliban unamaanisha nini kwa raia wengi wa Taliban hasa wanawake na watoto wa kike wanaotaka kuishi maisha ya kawaida kama binadamu wengine waliostaarabika duniani?
Wanafahamu itakuwa lazima wanaume wote kufuga ndevu, wenye michepuko na wanaoishi bila kuona watapigwa mawe mpaka kufa, wezi watakuwa wanakatwa mikono, wanawake hawatashiriki katika uongozi tena, ni lazima wavae hijab au niqab, lazima watoke na mwanaume wakienda kutembea, pombe haitanyweka tena hadharani lakini biashara ya dawa za kulevya za heroine zitashamiri kwa sababu Taliban ni wakulima wazuri wa mihadarati ya opium!
Ni aibu na ujuha kusherekea na kusherehesha utawala katili wa Taliban. Ni bahati mbaya sana kuwa na taifa lenye majuha wengi wanaochukuliwa na upepo wa kila aina matukio yanayotrend bila kuwa na maarifa.