Kuna movie inayotisha zaidi ya 'The Conjuring'?

Na ndo nilivyofanya mkuu ila nilivyomaliza nilitamani kujuta
Maana mkojo ulikuwa umenibana ila nikifikiria toilet kulivyo Giza saa nane usiku nahisi Kama nitakumbana na valak huko
Ukitaka upate msisimko wa horror movie cheki usiku na taa uzime ndo utapata ile feeling yenyewe.
Huwa nafanyaga hivyo na demu wangu, hofu humtanda kama mwizi aluefumaniwa na mali ya wizi
 
Habari zenu wadau wapenda movies hasa zile za kutisha.

Hivi juzi Kati hapa nilicheki movie inayoitwa 'the conjuring', nilicheki sehemu ya Kwanza na ya pili.

Hii ni baada ya kupata habari zake humu JF kwamba inatisha Sana na kilichonivutia zaidi kutaka kuzicheki hizi movies Ni kwasababu they are based on true story!

Hivyo nikawa curious kujua Nini kilijiri coz ninachoamini Ni kwamba wenzetu wa dunia ya Kwanza Mambo ya uchawi na ushirikina hayapo Sana Kama sisi waafrika.

Mazee hizi movie zinatisha aisee hasa ile sehemu ya pili inayohusisha ule mzimu unaoitwa 'valak' (hii sehemu ya pili nilivyomaliza kuangalia nikawa naogopa hata kwenda toilet kukojoa maana ilikuwa saa nane usiku afu Giza kinoma the conjuring sio mchezo mazee)

Nimevutiwa Sana na jinsi directors wanavyopangilia matukio na kufanya usisimke na kuogopa pia, na hata story yake inasisimua Sana kwani mwisho wameweka Picha za wahusika halisi Kama Ed & Lorraine Warren halisi kabisa waliokuwa wanafanya kazi ya kupeleleza matukio yasiyo ya kawaida (paranormal investigators)

Mpaka saivi najiuliza hivi kweli mtu unaweza ukawa na kipawa Kama Cha bi Lorraine Yani 'clairyvoyant'? Lakini kwa mujibu wa story Ni kwamba alikuwa hivyo kweli.

Sio hivyo tu, mwisho wanaonyesha mpaka Picha ya yule mtoto Janet aliyekuwa possessed na ule mzimu akiwa ana elea hewani (levitate) kiukweli ukweli kabisa yaani tukio lenyewe halisi lilivyonaswa kwenye camera achana na ile Picha ya kwenye movie, nilishangaa Sana!

Sasa nilikuwa nauliza wadau wa hizi makitu Kama kuna movie nyingine yoyote inayotisha zaidi ya hizi za the conjuring nipakue fasta nicheki maana siku hizi sijui nimekuwa na akili gani nimejikuta Napenda tu movie za kutisha.

Horror movies ambazo mpaka Sasa nishazicheki Ni hizi hapa chini:
The Conjuring 1&2
The Nun
IT (hii nimecheka chapter 2 tu)
SAW 3D
Final destination1-3
Wrong turn 1, 2, 4 &5

Ila Kati ya hizo zoote hakuna niliyotokea kuielewa Kama the conjuring.

Sasa wadau Nani anajua movie nyingine yoyote inayotisha zaidi ya the conjuring na yenye story ya kusisimua zaidi?

Afu Kuna kipindi nilionaga mdau humu jf anasema the conjuring sehemu ya tatu IPO njiani vipi ishatoka?

Karibuni wazee
Leta clip hapa za hiyo movie tuone
 
NILIWEZA HAYO UTOTONI, SASA HIVI NA BADILI CHANNEL FASTER, SITAKI UJINGA MIMI NA MAZOMBI, MAZOMBI. NAPENDA MOVIE NA SERIES AMBAZO EITHER MAKE ME SAD OR INSPIRE TO FIGHT FOR MY INTENDED GOAL EVEN IF I WILL CRAWL
Sawa mkuu horrors sio type yako
 
Kama unajijua huwezi Bora uachane nazo tu mkuu😀
Maana unaweza hata kuzimia ila kwa sisi wengine ni burudani na Wala sio kujitesa.
Sema jaribu tu mkuu siku Moja ucheki hata SAW 7 hivi utest feeling yake😎
hiyo final destination imenishinda mazombi ndio kabisa hapana siwezi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom