Money Stunna
JF-Expert Member
- Aug 9, 2011
- 13,054
- 6,281
kwani nlazima achome huko?
Mkuu utalatibu unaotumika ni kuchomwa nyuma,wewe unapendea kuchomwa mbele?au sehemu gani ya mwili wako ukichomwa hautajisikia maumivu?Umeshawahi kuchomwa nyuma mara ngapi?kwani nlazima achome huko?
Huo ugonjwa ninao hata mimi, yaani hata hapo nimesisimka mwili mzima, nakumbuka nikiwa kidato cha 2 niliandikiwa 5 ila niliishia 3 baada ya kuona nimepata nafuu nikasepa kwani hizo 3 nilipelekwa na ulinzi mkali ila nyingine wakaamini nitamaliza bt nikaishia kutia tiki mwenyewe,.......Loooh! Mungu atusaidie Waoga wa Sindano
Wewe hakika utakua ni mwoga wa VITU vyenye NCHA KALI...
Mimi naogopa sindano, yaani tangu kuanza kuifunga, kuweka dawa na hata kuchomwa....yaani hapo napata wakati mgumu sana, ktk jambo linalonifanya mtoto ni kuandikiwa sindano, ukubwani i.e nimeshaoa nilishawahi kwenda hosp doctor akaniandikia sindano nilimshawishi hadi akabadili tiba nikapewa vidonge ambavyo gharama ni kama mara 3 au 4 ya sindano ila mimi nilipata amani kutoka rohoni.....Chezea sindano wewe looooooooooooooooh!
Kinachowaogopesha watu kwenye sindano ni zile mbwembwe za maandalizi. Tena enzi zetu wakati tunachangia sindano za kuchemsha ndo ilikuwa balaa. Utakuta zimejaa tele kwenye beseni la maji ya moto. Mara nesi anachukua limkasi, anakorogakoroga halafu anaibuka na moja, anavuta maji ya moto halafu anayatoa kwa presha ya sindano. Akimaliza hapo anavuta dawa kwa mbwembwe, mara anaigongagonga sindano huku imeangalia hewani....yaani ikifika hatua hiyo utakuta dogo ashalala mbele.
Mie pia hii kitu huwa naigopa sana na niliweza kukata zaidi ya miaka 10 bila kupiga sindano though ukipambana na ugonjwa unaohitaji sindano inakuwa no way na ndio maana kuna kipindi kulikuwa na ugonjwa wa uti wa mgongo ilibidi tu nichomwe lakini kama chanjo ingekuwa ni ya vidonge ningegoma
kweli mkuu umenenakinachowaogopesha watu kwenye sindano ni zile mbwembwe za maandalizi. Tena enzi zetu wakati tunachangia sindano za kuchemsha ndo ilikuwa balaa. Utakuta zimejaa tele kwenye beseni la maji ya moto. Mara nesi anachukua limkasi, anakorogakoroga halafu anaibuka na moja, anavuta maji ya moto halafu anayatoa kwa presha ya sindano. Akimaliza hapo anavuta dawa kwa mbwembwe, mara anaigongagonga sindano huku imeangalia hewani....yaani ikifika hatua hiyo utakuta dogo ashalala mbele.
Hujambo lakini bibie.kweli mkuu umenena
Naona hapa tiba imekua kubwa kuliko mgonjwa.Ha! ha! ha!