Kuna Mgongano wa Katiba ya Zanzibar na ya Muungano, ufumbuzi wake tutake tusitake ni katiba mpya!

Ni hatari mno kwa Zanzibar kujitenga sana sana urithi pekee tutakaowaachia wajukuu zetu ni kuhakikisha Zanzibar inakaliwa na watanganyika tu.

Sasa huo Udikteta ulionao ndani ya nafsi yako utakusaidia nini mkuu? Wewe unataka kuwa huru lakini mwenzio umtawale au sivo?
 
View attachment 1767443
Tujadili huku tuliko toka, ndio msingi wa Muungano wetu. Kumefanyika hadaa nyingi kuidhoofisha Zanzibar nje ya Muungano na Ndani ya muungano huu, huu muungano hakuna alie mkubwa wala mdogo, nchi zote ni Equal, hamtaki basi sisi tutaendelea kuhoji uhalali wake na kumetumika sheria zipi za kimataifa mpaka kubadili jina la Muungano wetu , mpaka kumuondoa Rais wa Zanzibar umakamo wa Rais, mpaka kuifuta Tanganyika.
Hadi HII LEO HAKUJA FANYIKA ''CONSTITUTIONAL ASSEMBLY'' yaani Bunge la katiba.
La kwanz ni lile la Kikwete la Katiba ya Warioba ambalo lilikufa kifo cha mende. CCM walilijhodhi na kupindua meza.
 
Kinachotakiwa ni kupigania Tanzania moja na siyo kuwa na kakipande sehemu.

Hilo jambo haliwezekani mkuu, Watanganyika hawataki kutawaliwa na MZanzibari, na Wazanzibari hawataki kutawaliwa na watanganyika. Hiyo moja itapatikanwa vipi?
 
Suluhisho la kudumu ni kuanzisha effective assimilation policy ambayo within 50 years itakuwa imeshafuta uzanzibar na kubaki na Tanzania tu.
Nyerere alichelewa.

Hiyo ilitakiwa pale Mzee Karume aliposema tuwe na nchi moja "wewe rais mimi makamo" palepale Nyerere alitakiwa kuseize moment, sasa yeye akawa na wasiwasi kuwa akikubali idea hiyo ataonekana kaimeza Zanzibar, eti ataonekana mkoloni mpya.
Instead Nyerere akaopt kwenye long game, yaani kuimeza Zanzibar mdogomdogo, Hii plan imefeli baada ya muafaka wa Karume na Seif

Lakini sasa hivi huwezi hata kwa mabomu ya nyuklia kuwafanya Wazanzibar waikane autonomy yao, Never!
 
Kwa sasa inaonekana kama kila kitu kiko shwari katika muungano wetu lakini Ukweli ni kuwa kuna ufa mkubwa sana ambao ni hatari kwa muungano na nchi kiujumla.

Ukweli wenyewe ni kwamba Katiba mbili, yaani ya Muungano na ya Zanzibar (toleo la mwaka 2010)vinakinzana na hivyo kupelekea mkanganyiko ambao hauna afya kwa nchi na hivyo ili kuondoa jambo hili ambalo ni serious lazima mabadiriko katika Katiba ya Zanzibar au ya Muungano lazima yafanywe ili kurekebisha hili tatizo

Vifuatavyo ni vifungu katika katiba ya Zanzibar ambavyo vinapingana waziwazi na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1. Kipengele cha kwanza ni kuhusu Zanzibar kuwa ni nchi

Katiba ya Zanzibar ibara ya 1 imetamka kwa sauti kubwa kuwa ni NCHI na Imeainisha mipaka yake waziwazi

Ibara hiyo inasema hivi:

"1. Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la
Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka
na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar."

Kujitangaza huku kwa Zanzibar kuwa ni nchi haukuwemo kwenye toleo la kwanza la katiba ya mwaka 1984, Je ni kwa nini basi katika mabadiriko ya katiba hiyo toleo la 2010 Wazanzibar wakaamua kuiita Zanzibar kuwa ni nchi?

Wakati wazanzibar wakiutangaza Unchi wao na mipaka yao waziwazi kwenye katiba yao bado Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kutambua uwepo wa nchi moja tu iitwayo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mipaka ya hiyo Tanzania.

2. Ibara ya pili nayo ina contradiction, Katiba ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 imetwaa Madaraka ambayo awali yalikuwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kumpa rais wa Zanzibar. Awali kabisa, katiba ya JMT ilikuwa ikimpa rais wa JMT uwezo wa kuigawa Zanzibar katika mikoa na Wilaya kwa "kushauriana" na Rais wa Zanzibar lakini kwenye katiba ya Zanzibar, nguvu hizo kapewa rais wa Zanzibar kwa kufuata sheria zitakazotungwa na baraza la wawakilishi.

Ibara ya 2A ya Katiba ya Zanzibar toleo la 2010 inasema:

"2A. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Rais
aweza kuigawa Zanzibar katika Mikoa, Wilaya na maeneo mengineyo
kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi"

3. Katiba ya Sasa ya Muungano ibara ya 105(1)(b), Inatambua Muundo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wa Zamani, ambapo kuna cheo cha Waziri kiongozi na siyo muundo wa sasa wenye vyeo vya Makamu wa Kwanza na wa pili wa rais.

Hili siyo jambo dogo, maana ni ajabu uwe na kifungu cha katiba chenye kuelezea cheo ambacho hakipo!!. Kuacha ibara hii iendelee hivihivi kuwemo ndani ya katiba ja JMT wakati tayari Wazanzibar walisharekebisha muundo wa serikali yao maana yake inaweka hata question mark kwenye uhalali wa muundo mpya. Kunahitajika mabadiliko ya katiba ili kuweka jambo hili sawa!

4. Katiba ya Zanzibar ya toleo la 2010 inataka baraza la wawakilishi litunge sheria ya namna Wazanzibar watakavyoshiriki katika majeshi kwa ajili ya ulinzi wa Taifa

Kwanza tunajua kuwa kwa mujibu wa Katiba ya JMT, Suala la Majeshi ya Ulinzi wa Taifa ni suala la Muungano, Kwa muktadha huo, Sheria za Ulinzi wa JMT ni suala la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ninatambua wazi kuwa katiba ya Zanzibar haitumii neno Majeshi kuhusu vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, bali inatumia neno "Idara Maalumu". Wakati huohuo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haitambui Mahali popote kuwa hizo Idara maalumu ni Majeshi ya Ulinzi wa Taifa!
Na Katiba ya nchi, yaani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepiga Marufuku kuanzisha Jeshi la Ulinzi kinyume cha Sheria ya bunge

Sasa swali la Msingi ni je?
(a). Hiyo katiba ya Zanzibar ilipotamka neno Majeshi ilimaanisha Majeshi gani?, kwa nguvu gani ambazo baraza la wawakilishi linazo juu ya majeshi hayo?

(b). Kama Kwa kutamka hilo neno "Majeshi" ilimaanisha idara Maalumu au vikosi Maalumu vya SMZ, Je Kamanda mkuu wa Vikosi hivyo ambaye kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ni rais wa Zanzibar sasa anaweza kuamuru vikosi hivyo kuingia vitani kuilinda Zanzibar?
Maana kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar toleo la 2010 rais wa Zanzibar ana mamlaka ya kuviagiza vikosi ya SMZ (idara maalum) kufanya shughuli(mission) yoyote atakayoona inafaa kwa ajili ya Maslahi ya Taifa (Zanzibar), pigia Msitari maneno SHUGHULI YOYOTE ATAKAYOONA INAFAA!

5. Katiba ya Zanzibar Imepoka Mamlaka ya Amiri Jeshi Mkuu.

Katiba Ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 inatamka Vikosi Maalum ya SMZ kwa kutumia jina (Idara Maalum) na Imetaja Idara hizo kuwa Ni Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) na Jeshi la KMKM (Jeshi la Kuzuia Magendo) ba Idara ya Chuo cha Mafunzo(Magereza).
Na imetamka kwenye Ibara ya 123(1)Kuwa Rais wa Zanzibar atakuwa KAMANDA MKUU WA IDARA HIZO na Anaweza KUFANYA CHOCHOTE, pigia Msitari naneno KUFANYA CHOCHOTE kwa Ajili ya Maslahi ya Zanzibar, Sasa kama huu Siyo Uamiri jeshi mkuu ni nini?

Katiba hiyohiyo ibara ya 123(2) inasema kuwa Rais wa Zanzibar anaweza kuunda Idara nyingine yoyote atakayoona Inafaa na ANAWEZA KUIPA SHUGHULI YOYOTE ATAKAYOONA INAFAA KWA MANUFAA YA TAIFA. Pigia Msitari maneno "Shuguli yoyote", What if shughuli hiyo ikawa ni kupigana vita?
Sasa kama huu siyo uwezo wa Kuunda Majeshi kwa mgongo wa jina "Idara Maalum ni nini?"


6. Rais Wa Zanzibar akila Kiapo cha Kulinda Katiba ya Muungano (wakati wa kuapa kuwa mjumbe wa baraza la Mawaziri) na Akila Kiapo cha Kulinda Katiba ya Zanzibar anakuwa anaapa kufanya vitu vyenye contradiction

Tumeshaona, mahali ambapo katiba hizi mbili, Ya Zanzibar na ya Muungano zinapingana. Sasa ukiwa Rais wa Zanzibar ukaapa kulinda na kutetea vyote viwili, unakuwa unaapa viapo vyenye utata. Je utatekeleza kiapo gani kwanza pindi maslahi ya pande mbili yakikwaruzana?


7. Katiba ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 Imepoka mamlaka ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania kuhusu uwezo wa Mzanzibari kukata rufaa katika mahakama ya Rufaa ya Tanzania kwa makosa yanayohusu uhuru na Haki za binadamu baada ya hukumu kuwa imetolewa na mahakama kuu ya Zanzibar.

Sote tunajua kuwa miongoni mwa mambo ya Muungano ni Mahakama ya Rufaa, hata hivyo katiba ya Zanzibar imemega mamlaka haya ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katiba ya Zanzibar inasema kwenye Ibara ya 24(3) kuwa:

"Rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahkama Kuu katika Shauri lililofunguliwa dhidi ya Masharti ya sura hii ya Katiba yatasikilizwa na Mahkama Kuu mbele ya Majaji watatu bila ya kujumuisha Jaji aliyeamua shauri hilo mara ya kwanza. Majaji hao watatu watateuliwa na Jaji Mkuu na uamuzi wao utakuwa ni wa mwisho na hautokatiwa rufaa kwenye Mahkama ya Rufaa ya Tanzania"


Mwisho Kabisa
Wazanzibar Katika katiba yao toleo la 2010 kuna Mambo wameyawekea Kinga yasibadiishwe kirahisi, Mojawapo ni ZANZIBAR KUWA NCHI, Ukitaka Kubadilisha hili ni lazima Uitishe kura ya Maoni ya Wazanzibar, Sasa Jiulize kama hili itawezekana?
Kwanza Kipengele hiki peke yake Kinaua Ndoto hata ya CCM ya Serikali mbili kuelekea kwenye Serikali Moja

Kwa hiyo Ndugu Zangu, ni lazima tukubaliane, Hatuwezi kuwa na katiba mbili nchini zinazokinzana, Hatuwezi kuwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotambua vyeo ambavyo Havipo, Hatuwezi kuwa na Katiba ya Zanzibar inayompa rais wa "nchi" hiyo uwezo wa kuunda vikosi na akavipa "MISSION YOYOTE" atakayoona Inafaa kwa Masilahi ya sehemu ya Nchi hiyo halafu tusiogope. What If mission hiyo ni kupigana vita dhidi ya "yeyote" anayehatarisha maslahi ya Zanzibar?

Kutokana na Hilo, TUNAHITAJI KATIBA MPYA itakayoondoa Mkanganyiko huu!

Hatuwezi kuendelea Kutegemea GOODWILL YA VIONGOZI kwenye kuudumisha huu Muungano,, Bali tunahitaji Mfumo wa Kikatiba na Kisheria Uliokaa sawa ili hsya mambo yaende vizuri, ili kesho na keshokutwa hata Marais wa Pande hizi mbili wasipotoka Chama Kimoja, Kila Rais ajue mipaka ya Majukumu yake Kikatiba.

KATIBA MPYA HAIEPUKIKI, TUNAWEZA KUJIFICHA KWENYE MCHANGA KAMA MBUNI TUKAJIAMINISHA KUWA KILA KITU KIKO SHWARI LAKINI SIYO KWELI.

TAIFA LINAHITAJI KATIBA MPYA!

Link ya Kupata katiba ya Zanzibar toleo la 2010 ni hii hapa chini:


Katiba hazina mgongano bali kknachopaswa kufanyika Ni UPDATE kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili ku-accomodate maboresho ya liyofanyika kwenye Katiba ya ZNZ ya 2010.
 
Ingekuwa vizuri ukaweka vema hili. Ibara ya pili inasema Zanzibar ni nchi miongoni mwa nchi mbili zinazonda Jamhuri ya Muungano. Hivi ndivyo ilivyo. Hata hivyo ni vema pia kurudi kwenye Articles of Union na the Act of Union kwani hii ndio misingi ya kuwepo kwa JMT. Vinginevyo ni kubabaishana tu.
Kwani Katiba inasemaje kwenye hiyo Act of Union and Article of Union?
 
Katiba hazina mgongano bali kknachopaswa kufanyika Ni UPDATE kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili ku-accomodate maboresho ya liyofanyika kwenye Katiba ya ZNZ ya 2010.

Duh, Sasa wewe ndo umetuchanganya moja kwa moja.

Sasa kama katiba haijawa updated ili kuendana na mabadiliko ya Zanzibar huko si ndo kugongana kwenyewe?
Au unafikiri hiyo Update itafanyika kwa kutype tu upya hizo updates bila kikao cha bunge cha mabadiliko ya katiba kufanyika na kufuata process yote ya mabadiliko ya katiba?.

Ni mpaka mabadiliko hayo yafanywe kupitia upigaji wa kura bungeni na zipatikane theluthi mbili ya Wabunge wa Tanganyika na Theluthi mbili ya wabunge kutoka Zanzibar wapitishe mabadiliko hayo hapo ndipo mkanganyiko huu utaondoka, bila ya hivyo hizi katiba mbili kwa sasa zinapingana
 
Duh, Sasa wewe ndo umetuchanganya moja kwa moja.

Sasa kama katiba haijawa updated ili kuendana na mabadiliko ya Zanzibar huko si ndo kugongana kwenyewe?
Au unafikiri hiyo Update itafanyika kwa kutype tu upya hizo updates bila kikao cha bunge cha mabadiliko ya katiba kufanyika na kufuata process yote ya mabadiliko ya katiba?.

Ni mpaka mabadiliko hayo yafanywe kupitia upigaji wa kura bungeni na zipatikane theluthi mbili ya Wabunge wa Tanganyika na Theluthi mbili ya wabunge kutoka Zanzibar wapitishe mabadiliko hayo hapo ndipo mkanganyiko huu utaondoka, bila ya hivyo hizi katiba mbili kwa sasa zinapingana
Asante Mkuu kwa maboresho. Tuko pamoja

And kwa maneno yako hayo ndipo Rasimu ya Katiba ya Warioba inapokuwa very RELEVANT at this moment in time
 
Unaletaje maendeleo wakati nikiwa na Bidhaa zangu kutoka zanzibar zikija Bara zinatozwa kodi mara ya pili?
Sukari kutoka Zanzibar kuja bara ni marufuku?

-Eti muungano na maendeleo , Serikali ya Zanzibar hairuhusiwi kuomba misaada ya nje kuijenga Zanzibar, na ikimpata mfadhili ,ni mpaka Muungano waridhie ndio apewe msada huo tena kwa mashartiya Kuigawabara % ya huo msaada,?

-Unasemaje Katiba iliyopo inatosha huku wazanzibari waliokimbizwa na mapinduzi wakitaka kurudi nyumbani hawakubaliwi na Tanganyika hata zanzibar yenyewe inawatamani warejee?

-Suala la Uraia kuwa Moja ni Msiba mkubwa Kwa Znzibar, kwani raia wa Zanzibar si Raia wa Tanganyika, kwa hiyo Tanganyika ndiye anaamua yupi awe raia na yupi asiwe?

TUNAHITAJI KATIBA MPYA ILI TUWE A MUUNDOMPYA WA MUUNGANO.
Hizi ni choko choko tu zenye nia ovu ya kuleta migongano isiyo ya lazima kwenye nchi yetu.Wananchi wa kawaida wala hawana tatizo na mfumo wa muungano wa sasa.Ninyi mlio kwenye payroll ya mabeberu ninyi,ndio mnaotuletea shida.Mnachofanya ni kuwa-instigate Watanzania:Tanganyika na Visiwani,ili waone kwamba serikali zao haziwatendei haki.This is dissent,which if not properly handled could in collaboration with other issues,lead to revolt by the citizenry.Kuweni makini sana.
 
Kwa sasa inaonekana kama kila kitu kiko shwari katika muungano wetu lakini Ukweli ni kuwa kuna ufa mkubwa sana ambao ni hatari kwa muungano na nchi kiujumla.

Ukweli wenyewe ni kwamba Katiba mbili, yaani ya Muungano na ya Zanzibar (toleo la mwaka 2010)vinakinzana na hivyo kupelekea mkanganyiko ambao hauna afya kwa nchi na hivyo ili kuondoa jambo hili ambalo ni serious lazima mabadiriko katika Katiba ya Zanzibar au ya Muungano lazima yafanywe ili kurekebisha hili tatizo

Vifuatavyo ni vifungu katika katiba ya Zanzibar ambavyo vinapingana waziwazi na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1. Kipengele cha kwanza ni kuhusu Zanzibar kuwa ni nchi

Katiba ya Zanzibar ibara ya 1 imetamka kwa sauti kubwa kuwa ni NCHI na Imeainisha mipaka yake waziwazi

Ibara hiyo inasema hivi:

"1. Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la
Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka
na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar."

Kujitangaza huku kwa Zanzibar kuwa ni nchi haukuwemo kwenye toleo la kwanza la katiba ya mwaka 1984, Je ni kwa nini basi katika mabadiriko ya katiba hiyo toleo la 2010 Wazanzibar wakaamua kuiita Zanzibar kuwa ni nchi?

Wakati wazanzibar wakiutangaza Unchi wao na mipaka yao waziwazi kwenye katiba yao bado Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kutambua uwepo wa nchi moja tu iitwayo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mipaka ya hiyo Tanzania.

2. Ibara ya pili nayo ina contradiction, Katiba ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 imetwaa Madaraka ambayo awali yalikuwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kumpa rais wa Zanzibar. Awali kabisa, katiba ya JMT ilikuwa ikimpa rais wa JMT uwezo wa kuigawa Zanzibar katika mikoa na Wilaya kwa "kushauriana" na Rais wa Zanzibar lakini kwenye katiba ya Zanzibar, nguvu hizo kapewa rais wa Zanzibar kwa kufuata sheria zitakazotungwa na baraza la wawakilishi.

Ibara ya 2A ya Katiba ya Zanzibar toleo la 2010 inasema:

"2A. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Rais
aweza kuigawa Zanzibar katika Mikoa, Wilaya na maeneo mengineyo
kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi"

3. Katiba ya Sasa ya Muungano ibara ya 105(1)(b), Inatambua Muundo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wa Zamani, ambapo kuna cheo cha Waziri kiongozi na siyo muundo wa sasa wenye vyeo vya Makamu wa Kwanza na wa pili wa rais.

Hili siyo jambo dogo, maana ni ajabu uwe na kifungu cha katiba chenye kuelezea cheo ambacho hakipo!!. Kuacha ibara hii iendelee hivihivi kuwemo ndani ya katiba ja JMT wakati tayari Wazanzibar walisharekebisha muundo wa serikali yao maana yake inaweka hata question mark kwenye uhalali wa muundo mpya. Kunahitajika mabadiliko ya katiba ili kuweka jambo hili sawa!

4. Katiba ya Zanzibar ya toleo la 2010 inataka baraza la wawakilishi litunge sheria ya namna Wazanzibar watakavyoshiriki katika majeshi kwa ajili ya ulinzi wa Taifa

Kwanza tunajua kuwa kwa mujibu wa Katiba ya JMT, Suala la Majeshi ya Ulinzi wa Taifa ni suala la Muungano, Kwa muktadha huo, Sheria za Ulinzi wa JMT ni suala la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ninatambua wazi kuwa katiba ya Zanzibar haitumii neno Majeshi kuhusu vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, bali inatumia neno "Idara Maalumu". Wakati huohuo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haitambui Mahali popote kuwa hizo Idara maalumu ni Majeshi ya Ulinzi wa Taifa!
Na Katiba ya nchi, yaani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepiga Marufuku kuanzisha Jeshi la Ulinzi kinyume cha Sheria ya bunge

Sasa swali la Msingi ni je?
(a). Hiyo katiba ya Zanzibar ilipotamka neno Majeshi ilimaanisha Majeshi gani?, kwa nguvu gani ambazo baraza la wawakilishi linazo juu ya majeshi hayo?

(b). Kama Kwa kutamka hilo neno "Majeshi" ilimaanisha idara Maalumu au vikosi Maalumu vya SMZ, Je Kamanda mkuu wa Vikosi hivyo ambaye kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ni rais wa Zanzibar sasa anaweza kuamuru vikosi hivyo kuingia vitani kuilinda Zanzibar?
Maana kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar toleo la 2010 rais wa Zanzibar ana mamlaka ya kuviagiza vikosi ya SMZ (idara maalum) kufanya shughuli(mission) yoyote atakayoona inafaa kwa ajili ya Maslahi ya Taifa (Zanzibar), pigia Msitari maneno SHUGHULI YOYOTE ATAKAYOONA INAFAA!

5. Katiba ya Zanzibar Imepoka Mamlaka ya Amiri Jeshi Mkuu.

Katiba Ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 inatamka Vikosi Maalum ya SMZ kwa kutumia jina (Idara Maalum) na Imetaja Idara hizo kuwa Ni Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) na Jeshi la KMKM (Jeshi la Kuzuia Magendo) ba Idara ya Chuo cha Mafunzo(Magereza).
Na imetamka kwenye Ibara ya 123(1)Kuwa Rais wa Zanzibar atakuwa KAMANDA MKUU WA IDARA HIZO na Anaweza KUFANYA CHOCHOTE, pigia Msitari naneno KUFANYA CHOCHOTE kwa Ajili ya Maslahi ya Zanzibar, Sasa kama huu Siyo Uamiri jeshi mkuu ni nini?

Katiba hiyohiyo ibara ya 123(2) inasema kuwa Rais wa Zanzibar anaweza kuunda Idara nyingine yoyote atakayoona Inafaa na ANAWEZA KUIPA SHUGHULI YOYOTE ATAKAYOONA INAFAA KWA MANUFAA YA TAIFA. Pigia Msitari maneno "Shuguli yoyote", What if shughuli hiyo ikawa ni kupigana vita?
Sasa kama huu siyo uwezo wa Kuunda Majeshi kwa mgongo wa jina "Idara Maalum ni nini?"


6. Rais Wa Zanzibar akila Kiapo cha Kulinda Katiba ya Muungano (wakati wa kuapa kuwa mjumbe wa baraza la Mawaziri) na Akila Kiapo cha Kulinda Katiba ya Zanzibar anakuwa anaapa kufanya vitu vyenye contradiction

Tumeshaona, mahali ambapo katiba hizi mbili, Ya Zanzibar na ya Muungano zinapingana. Sasa ukiwa Rais wa Zanzibar ukaapa kulinda na kutetea vyote viwili, unakuwa unaapa viapo vyenye utata. Je utatekeleza kiapo gani kwanza pindi maslahi ya pande mbili yakikwaruzana?


7. Katiba ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 Imepoka mamlaka ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania kuhusu uwezo wa Mzanzibari kukata rufaa katika mahakama ya Rufaa ya Tanzania kwa makosa yanayohusu uhuru na Haki za binadamu baada ya hukumu kuwa imetolewa na mahakama kuu ya Zanzibar.

Sote tunajua kuwa miongoni mwa mambo ya Muungano ni Mahakama ya Rufaa, hata hivyo katiba ya Zanzibar imemega mamlaka haya ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katiba ya Zanzibar inasema kwenye Ibara ya 24(3) kuwa:

"Rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahkama Kuu katika Shauri lililofunguliwa dhidi ya Masharti ya sura hii ya Katiba yatasikilizwa na Mahkama Kuu mbele ya Majaji watatu bila ya kujumuisha Jaji aliyeamua shauri hilo mara ya kwanza. Majaji hao watatu watateuliwa na Jaji Mkuu na uamuzi wao utakuwa ni wa mwisho na hautokatiwa rufaa kwenye Mahkama ya Rufaa ya Tanzania"


Mwisho Kabisa
Wazanzibar Katika katiba yao toleo la 2010 kuna Mambo wameyawekea Kinga yasibadiishwe kirahisi, Mojawapo ni ZANZIBAR KUWA NCHI, Ukitaka Kubadilisha hili ni lazima Uitishe kura ya Maoni ya Wazanzibar, Sasa Jiulize kama hili itawezekana?
Kwanza Kipengele hiki peke yake Kinaua Ndoto hata ya CCM ya Serikali mbili kuelekea kwenye Serikali Moja

Kwa hiyo Ndugu Zangu, ni lazima tukubaliane, Hatuwezi kuwa na katiba mbili nchini zinazokinzana, Hatuwezi kuwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotambua vyeo ambavyo Havipo, Hatuwezi kuwa na Katiba ya Zanzibar inayompa rais wa "nchi" hiyo uwezo wa kuunda vikosi na akavipa "MISSION YOYOTE" atakayoona Inafaa kwa Masilahi ya sehemu ya Nchi hiyo halafu tusiogope. What If mission hiyo ni kupigana vita dhidi ya "yeyote" anayehatarisha maslahi ya Zanzibar?

Kutokana na Hilo, TUNAHITAJI KATIBA MPYA itakayoondoa Mkanganyiko huu!

Hatuwezi kuendelea Kutegemea GOODWILL YA VIONGOZI kwenye kuudumisha huu Muungano,, Bali tunahitaji Mfumo wa Kikatiba na Kisheria Uliokaa sawa ili hsya mambo yaende vizuri, ili kesho na keshokutwa hata Marais wa Pande hizi mbili wasipotoka Chama Kimoja, Kila Rais ajue mipaka ya Majukumu yake Kikatiba.

KATIBA MPYA HAIEPUKIKI, TUNAWEZA KUJIFICHA KWENYE MCHANGA KAMA MBUNI TUKAJIAMINISHA KUWA KILA KITU KIKO SHWARI LAKINI SIYO KWELI.

TAIFA LINAHITAJI KATIBA MPYA!

Link ya Kupata katiba ya Zanzibar toleo la 2010 ni hii hapa chini:


Mkuu umenifumbua macho sasa nimeamini hatuna muungano Bali tunamgongano
 
Kwa sasa Zanzibar inaendeshwa na aina ya serikali ambayo muundo wake hautambuliki katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katiba ya Zanzibar inapubgana na katiba ya JMT

Tunahitaji katiba mpya yenye kuondoa mtanzuko huu!
 
Back
Top Bottom