Kuna mda wanawake kwa tamaa zao wanafanya watoto wanakosa haki kwa baba zao

Zegota

JF-Expert Member
Jun 5, 2020
274
584
Nilikuwa na mahusiano ya mda mrefu na binti mmoja tangu tukiwa masomoni kiasi kwamba mpaka ndugu na wazazi wa pande zote wakayafahamu mahusiano yetu.

Tuliendelea kuwa pamoja hata wakati ambapo tulikuwa tumemaliza masomo yetu ya elimu ya juu. Tuliishi wote nikiwa nimepanga baada ya kupata kidogo sapoti ya wazazi nikawa napambana na maisha ya kitaa nikijua Niko mtu ambae ni mwenza sahihi kwangu.

Huyu binti alipatq ujauzito na vipimo vilithibitisha hivo, akaomba kurudi kwao nikamruhusu. Nikabaki mjini napambana ninachopata namtumia kumsapoti kutunza mimba, alivojifungua ikabidi kama miezi minne hivi Mimi na binamu yangu tukasifiri kwenda kuona mtoto, tulipofika kimuonekano yule mtoto najiona Mimi kabisa kwa ule mfanano lakini baada ya maongezi ya mda mrefu na kutoa zawadi tulizopeleka, Binti akiwa na macho makavu kabisa tukiwa wa3, Mimi, yeye na binamu akinambia "nashukuru kwa sapoti Yako kwa kipindi chote ambacho tuko wote, lakini niombe samahani kukuambia kuwa huyu mtoto sio wako" na kadi nikapewa likionesha baba yake sio Mimi. Hapa naambiwa maneno haya Niko kwao tena nikiwa na binamu yangu

Sikuwa na jinsi zaidi ya kujikaza kiume kama vile hakuna kitu kilichotokea, baadae tukaaga tukaondoka, tulivyorudi nikawaeleza wazazi yote yaliyotokea wakanipa ushauri wao na maisha mapya yakaendelea.

Baada ya Miaka 3 kupita, maisha yangu yamebadilika kwa kiasi kubwa sana tofauti na mwanzo ambavyo nilikuwa Sina kazi, napokea simu kutoka kwa huyu binti wiki iliyopita, Akisema " Yule mtoto ni wangu na yeye ananipa taarifa tu nijue tu Ile ni damu yangu suala la kumhudumia yeye Hana shida nalo nikiamua nihudumie nisipoamua niache na kwamba kipindi kile alisema vile kwa kuwa sikuwa na uwezo wa kumhudumia hivyo kulikuwa na mtu ampa sapoti ya kutosha"

Ukimwangalia mtoto ni Mimi kabisa Wala siwezi kukataa hilo, kwa Sasa huyu nadhani kibosile wake aliyekuwa anampa jeuri hayuko nae tena anataka kurudisha mpira kwangu.

Pamoja kwamba alidai hahitaji sapoti kwangu amekuwa msumbufu sana mpaka kwa ndugu
 
Nilikuwa na mahusiano ya mda mrefu na binti mmoja tangu tukiwa masomoni kiasi kwamba mpaka ndugu na wazazi wa pande zote wakayafahamu mahusiano yetu.

Tuliendelea kuwa pamoja hata wakati ambapo tulikuwa tumemaliza masomo yetu ya elimu ya juu. Tuliishi wote nikiwa nimepanga baada ya kupata kidogo sapoti ya wazazi nikawa napambana na maisha ya kitaa nikijua Niko mtu ambae ni mwenza sahihi kwangu.

Huyu binti alipatq ujauzito na vipimo vilithibitisha hivo, akaomba kurudi kwao nikamruhusu. Nikabaki mjini napambana ninachopata namtumia kumsapoti kutunza mimba, alivojifungua ikabidi kama miezi minne hivi Mimi na binamu yangu tukasifiri kwenda kuona mtoto, tulipofika kimuonekano yule mtoto najiona Mimi kabisa kwa ule mfanano lakini baada ya maongezi ya mda mrefu na kutoa zawadi tulizopeleka, Binti akiwa na macho makavu kabisa tukiwa wa3, Mimi, yeye na binamu akinambia "nashukuru kwa sapoti Yako kwa kipindi chote ambacho tuko wote, lakini niombe samahani kukuambia kuwa huyu mtoto sio wako" na kadi nikapewa likionesha baba yake sio Mimi. Hapa naambiwa maneno haya Niko kwao tena nikiwa na binamu yangu

Sikuwa na jinsi zaidi ya kujikaza kiume kama vile hakuna kitu kilichotokea, baadae tukaaga tukaondoka, tulivyorudi nikawaeleza wazazi yote yaliyotokea wakanipa ushauri wao na maisha mapya yakaendelea.

Baada ya Miaka 3 kupita, maisha yangu yamebadilika kwa kiasi kubwa sana tofauti na mwanzo ambavyo nilikuwa Sina kazi, napokea simu kutoka kwa huyu binti wiki iliyopita, Akisema " Yule mtoto ni wangu na yeye ananipa taarifa tu nijue tu Ile ni damu yangu suala la kumhudumia yeye Hana shida nalo nikiamua nihudumie nisipoamua niache na kwamba kipindi kile alisema vile kwa kuwa sikuwa na uwezo wa kumhudumia hivyo kulikuwa na mtu ampa sapoti ya kutosha"

Ukimwangalia mtoto ni Mimi kabisa Wala siwezi kukataa hilo, kwa Sasa huyu nadhani kibosile wake aliyekuwa anampa jeuri hayuko nae tena anataka kurudisha mpira kwangu.

Pamoja kwamba alidai hahitaji sapoti kwangu amekuwa msumbufu sana mpaka kwa ndugu
Ashakutaarifu ni mtoto wako na anachohitaji ni wewe kujua tu kwamba uyo ni mwanao sasa anataka nini kingine mpaka kufikia hatua ya kusumbua ndugu? Hapa utapigwa kwa mchezo wao ule wa kutaka child support we nenda kamchukue mtoto wako uishi nae, kama bado hustler mtulize dogo kwa bibi ake kwanza
 
Kama una hakika mtoto ni wako fanya kila jitihada awe chini ya himaya yako moja kwa moja.
Usimuadhibu malaika wa Mungu kwa upumbavu na umalaya wa mama yake.

Wapo watakaosema ni vibaya kumtenganisha mtoto na mama yake lakini kitendo cha huyo mama kumbadilishia mtoto mababa kwa kigezo cha uwezo wa kiuchumi kushamtoa sifa zote za kuwa mama bora.

Ni swala la wakati atatokea mwenye uwezo zaidi yako utanyang'anywa tena mtoto.
 
Mimi nilibeba Mwanangu akiwa na miaka miwili baada ya kuletewa mapicha picha.

Mpaka alipojirudi ndio nikamrudisha ila Cha ajabu dogo aligoma kubaki kwa mama yake.

Nikatimua nae baadae ka mama yake kaka jileta kwangu kenyewe sijui nimekuja kumuona mtoto.

Nikakapiga mimba nyingine ndio ngebe ziliisha.
 
Back
Top Bottom