Kuna matatizo gani hospitali za M'nyamala na Temeke?

Mar 6, 2010
74
0
Hakika hii nchi ndio maana inazidi kulaanika siku hadi siku.

Kwa walioangalia kwenye ITV taarifa ya habari imesikitisha saana kuona wagonjwa wakiwa kwenye ambulance wakisubiria wengine wazidiwe ndipo wapelekwe muhimbili.

Mh meya wa kinondoni SALUM LONDA akiwa na wenzake waliamua kuwatoke gafla bila taarifa hospital ya mwananyamala na kukuta wagonjwa wamelala kwenye ambulance ati wakisubiri ijae wapelekwe MUHIMBILI...jamani kweli hawa watu wanamjua MUNGU kweli..

Je ingekuwa ndugu yako anaumwa kweli wewe DK MKUU DK SULEIMAN ulietetea ati ni kutokana na kufanya ECONOMY ya Mafuta ya Gari...???kweli wewe baba Mamamako ameletwa hapo amezidiwa anatakiwa kwenda muhimbili nyie si wa kwanza kulazimisha dereva amwahimishe muhimbili iweje wengine mnawafanya kama Samaki wa MUSOMA jamani...gari aiondoki mpaka ijae ndio safari ya kupeleka samaki inaanza..sasa binadamu hawana aibu wala haya kabisa jamani...Huyu dk bila haya wala aibu ya kuzaliwa alijitetea kwamba Awakuwa na mafuta ya gari ya kutosha so wana minimize kwenda mara kwa mara kwa kusubiri wengine wajae wanaoitajika kwenda hospital.....

Hivi wewe waziri wa afya hawa watu wana akili??na kama kweli wanayosema mafuta machache wewe na wizara yako mna akili kweli??mnawaambia wasubirishe watu wanaoitajika opereshen kwenye ambulance;;;shame tanzania gov...,.

Watanzania tunaitaji kubadilika kudai haki zetu hata kwa damu
 
Mwanamke mmja aitwaye jane...amefariki jana kwenye hospital ya Temeke
baada ya kukosa damu kisa pesa,habari zaidi ambazo clouds imeweza kuweka wazi swala hili kupitia mh kibonde akisoma yaliomo magazetini ....
hali halisi ilikuwa hivi..mgonjwa aliletwa na ndugu yake ..alipofika akaa kama nusu saa kabla ya ma nurse kuanza kumshugulikia ..walipoona amezidiwa wakasema mgonjwa wenu anaitaji damu...anaeweza umtolea aje.....mmoja wao akajitolea wakaenda akatolewa damu..mgonjwa akapelekewa kama ni kweli..nasema hivi baada ya dk 20 nurse alirudi tena kusema mgonjwa anaitaji damu zaidi..hapo ikafika stage nurse akasema kama una 10,000 tukusaidie fasta kupata damu..yule ndugu akasema ana 5000 akaomba wamwekee rest anaenda mtu kuichukua kwenye atm..yule dada akawaacha gafla akwapita wakamuita jamani anaendeleaje...aakajibu mi nimemaliza kazi anakuja mwingine mtasema nae...hapo alikuwa anadai hela na kungangania mgonjwa hali si nzuri..alipofika nurse mwingine akumwaambia kama kuna mgonjwa hali mbaaya anaitaji damu...wakaaka kama saa tano..kuelekea sita usiku yaani sita kasorobo yule dada MUNGU akampenda zaidi akatutoka...hakika ni aibu kwa waziri mhusika David.amekuwa akifumbia sana matatizo haya akishirikiana na mganga mkuu dada mmoja DK ASHA na hivyo kuona kifo kwa watu wasiowahusu ni kawaida...nakumbuka majuzi tu hospital hii hii mtu mmoja amekufa kwa uzembe...hii hii jamani mtoto amekatwa mkono kwa makosa...HUYU HUYU DK ASHA AKADAI NAOMBENI NIFWATILIE MARA AKAJITOKEZA NA KUDAI AMEAMUA KUWA MWENYEKT WA WATAKAOFWATILIA HILI..MPAKA LEO HII WALE MA NURSE WANAENDELEA KUTINGISHA MAISHA YA WATU...SASA HILI SIJAELEWA DK MWAKYUSA MNA DILI NA HUYU MAMA ..???AMA??MAANA KUNA WENGINE KWELI WATU WANAPOKUFA NDIPO NAFASI ZAO ZA KAZI ZINASIMAMA...KAMA SIO KWA NINI WATU WANAKUFA WEWE UNAKAA KIMYA MNAFANYA WATANZANIA KAMA WENDAWAZIMU??LINI MTAACHA KUUA WATU JAMANI TEEMEKE...

RAIS KIKWETE TUNAOMBA UINGILIE KATI TUMECHOKA NA TEMEKE/MWANYAM,ALA//KAMA KULINDANA MMESHALINDANA VYA KUTOSHA JAMANI INATOSHA ANGALIEN ROHO ZA WATU!!!!
 
HAYA WALE WA MHIMBILI.....MHIMBILI! Inachekesha lakini pia inasononesha sana! Ambulance ni kwa ajili ya emergency! Upendo wa watu unazidi kupoa! Kama huwezi ku-sympasize na Mama mjamzito kwa mfano anayehitaji msaada wa haraka! Vipi kuhusu mtoto mdogo yule wa miaka 5 anayesumbuliwa na asthma! Jiweke kwenye nafasi yao either wewe mwenyewe au mtoto wako, au mke wako! Najua utafanya kila liwezekanalo kuokoa maisha yao But why not to your neighbour?
 
haya wale wa mhimbili.....mhimbili!

wenye haraka zao!!!

mungu atusamehe kwa kweli;hawa ma dk wa siku hizi hawana utu wala ubinadamu utasema wamezaliwa
sudan
 
wanasubiriana kama daladala, ambulance ni kwa ajili ya emergency, so kama wanasubirina si wapande daladala
 
Safi sana hii hali. Kama sikosei, Dar ni moja ya mkoa wenye wabunge wote wa CCM.

Hongera sana Mwananyamala. Nyie endeleeni tu kusubiri hadi ijae. Kama walipanda tshirt za njano na kijana/Pilau na Khanga za sura ya mtu, acha wakione.

Sasa hawa watu utawasaidia vipi kama waliuza wenyewe utu wao na kibaya zaidi, watauza tena mwaka huu na hao CCM wenyewe bila woga wanasema 70% ni wafuata upepo.
 
kweli ubinadamu kazi ndugu yangu
hali hii yapaswa kulaaniwa kwa nguvu zote
huyu dr naamini hafai kukalia nafasi aliyonayo
hafai hata kuitumikia jamii kwa namna yoyote ile
amulikwe kwa ukaribu na aadhibiwe ipasavyo
avuliwe hadhi ya udaktari wa wilaya
miiko ya taaluma hiyo izingatiwe
 
Back
Top Bottom