Kuna maswali yafaa tujiulize kwa bajeti ya serikali ya 2017/18

Noel Shao

Member
Jan 19, 2017
89
185
BAJETI HII HAITA MUACHA MTU SALAMA.

Na Noel Shao

Kuna maswali yafaa tujiulize kwa bajeti ya serikali ya 2017/18.

1. Uelewa wa bajeti yenyewe kwa wasomi walio wengi umekuwa shida. Kwa mfano spika wa Bunge Job ndugai alisema “Kwa kweli hii haijawahi kutokea, ni kwa miaka mingi hatujawahi kuona bajeti nzuri kama hii.”
Kama spika wa Bunge anaweza sema hivi, halafu anashindwa ainisha, Chambua, oanisha mambo, unajiuliza kwa wale wasio enda shule itakuwa Je?

Mara nyingi utekelezaji wa bajeti huwa ni kama abradakaraba tu. Huwa hazitekelezeki zaidi ya shangwe kwenye maandishi na taaluma kuingiliwa na siasa. Yamkini yupo sahihi ila kaifananisha bajeti hii na ya miaka ipi hadi iwe bora kuwahi kutokea.? Hapa utagundua kuwa tatizo la wengi katika CCM ni kumbukumbu ndogo na ushabiki wa Chama.

Kadhalika, Kinacho msumbua spika nadhani ni uspika 2020. Ndugai hivi karibuni ameshindwa jitathimini kama anasema kwa niaba ya 'kiti' yaani wananchi au chama chake na matazamio ya madaraka.

2. Kitendo cha serikali kufuta Road License. Kwa lugha nyepesi ni kuwa serikali imefanya Biashara moja kubwa mno. Serikali imeamua kutumia lugha kufuta badala ya 'kuhamisha '. Tozo za road licenses zimehamishiwa kwenye mafuta na siyo zimefutwa.
Hii maana yake nini:-
a) Walala hoi, na wavuja jasho wote watashiriki kikombe hichi cha kulipa kodi. Mafuta yanapo ongezeka kila kitu hupanda bei, na ikumbukwe wananchi wengi vjijini bado ni watumiaji wa mafuta ya taa, pia auli zitapanda, kile kitendo cha kufuta kodi katika usafiri wa mazao, gharama zake utalipia kwenye mafuta.

Dhana ya 'serikali ya wanyonge' katika bajeti hii tumeuziwa maneno. Vitendo ni kuwa wanyonge hao watawasaidia mabwenyenye katika kulipa kodi.

b). Serikali hapa haijacheza na vichwa vya wavuja jasho pekee, bali hata wabunge. Nilishangaa kuona wabunge wanapiga meza kushangilia kile kilicho itwa "kufuta" wakasahau kuwa huu pia ulikuwa mtego na mchezo wa kucheza na lugha . Kwa sasa ni kuwa lile zoezi la baadhi wa wabunge, Mawaziri kukwepa kulipa kodi, katika hili hawana namna. Lazima mashangingi yao watayaweka mafuta. Sasa watakwepa vipi hapo.

Labda kukwepa huu mtego, kwa kuwa nao ni wajuvi wa kucheza na lugha waanzishe Petrol station zao "VIP " kama bima zao za afya. Au wawe na vitambulisho wakienda sheli waonyeshe.

3. Kitendo cha serikali kuu kuamua kukusanya ushuru hadi ule ulio kuwa unakusanywa na halimashauri mfano ushuru wa mabango kimenipa shaka mbili, moja, halimashauri wao wataingiza mapato kupitia nini? Au watabaki wanakusanya ushuru wa taka??? Pili, kitendo hichi kina wingu kisiasa.

Mwisho, Bunge letu linatia shaka kuliko matumaini. Halina meno, limekuwa kibogoyo kumumunya maneno ya serikali. Halina changamoto kwa serikali, katika mazingira kama haya huwa sioni uhalali wa kuwepo kwake. Kama wanashindwa kuipa changamoto serikali kwenye masuala kma haya, uhai bunge uko wapi??

Una mtazamo gani kuhusu bajeti ya 2017 /18

"Noel Shao
[HASHTAG]#mjenziWaTanzaniaMpya[/HASHTAG]
 
Swali la kujiuliza tu wamefuta load licence na kuipeleka katika mafuta swali Je kuna gari linatumia mafuta ya taa

Khoo khoo khoo khoo maana kodi imeongenzwa mpaka kwenye mafuta ya taa
 
BAJETI HII HAITA MUACHA MTU SALAMA.

Na Noel Shao

Kuna maswali yafaa tujiulize kwa bajeti ya serikali ya 2017/18.

1. Uelewa wa bajeti yenyewe kwa wasomi walio wengi umekuwa shida. Kwa mfano spika wa Bunge Job ndugai alisema “Kwa kweli hii haijawahi kutokea, ni kwa miaka mingi hatujawahi kuona bajeti nzuri kama hii.”
Kama spika wa Bunge anaweza sema hivi, halafu anashindwa ainisha, Chambua, oanisha mambo, unajiuliza kwa wale wasio enda shule itakuwa Je?

Mara nyingi utekelezaji wa bajeti huwa ni kama abradakaraba tu. Huwa hazitekelezeki zaidi ya shangwe kwenye maandishi na taaluma kuingiliwa na siasa. Yamkini yupo sahihi ila kaifananisha bajeti hii na ya miaka ipi hadi iwe bora kuwahi kutokea.? Hapa utagundua kuwa tatizo la wengi katika CCM ni kumbukumbu ndogo na ushabiki wa Chama.

Kadhalika, Kinacho msumbua spika nadhani ni uspika 2020. Ndugai hivi karibuni ameshindwa jitathimini kama anasema kwa niaba ya 'kiti' yaani wananchi au chama chake na matazamio ya madaraka.

2. Kitendo cha serikali kufuta Road License. Kwa lugha nyepesi ni kuwa serikali imefanya Biashara moja kubwa mno. Serikali imeamua kutumia lugha kufuta badala ya 'kuhamisha '. Tozo za road licenses zimehamishiwa kwenye mafuta na siyo zimefutwa.
Hii maana yake nini:-
a) Walala hoi, na wavuja jasho wote watashiriki kikombe hichi cha kulipa kodi. Mafuta yanapo ongezeka kila kitu hupanda bei, na ikumbukwe wananchi wengi vjijini bado ni watumiaji wa mafuta ya taa, pia auli zitapanda, kile kitendo cha kufuta kodi katika usafiri wa mazao, gharama zake utalipia kwenye mafuta.

Dhana ya 'serikali ya wanyonge' katika bajeti hii tumeuziwa maneno. Vitendo ni kuwa wanyonge hao watawasaidia mabwenyenye katika kulipa kodi.

b). Serikali hapa haijacheza na vichwa vya wavuja jasho pekee, bali hata wabunge. Nilishangaa kuona wabunge wanapiga meza kushangilia kile kilicho itwa "kufuta" wakasahau kuwa huu pia ulikuwa mtego na mchezo wa kucheza na lugha . Kwa sasa ni kuwa lile zoezi la baadhi wa wabunge, Mawaziri kukwepa kulipa kodi, katika hili hawana namna. Lazima mashangingi yao watayaweka mafuta. Sasa watakwepa vipi hapo.

Labda kukwepa huu mtego, kwa kuwa nao ni wajuvi wa kucheza na lugha waanzishe Petrol station zao "VIP " kama bima zao za afya. Au wawe na vitambulisho wakienda sheli waonyeshe.

3. Kitendo cha serikali kuu kuamua kukusanya ushuru hadi ule ulio kuwa unakusanywa na halimashauri mfano ushuru wa mabango kimenipa shaka mbili, moja, halimashauri wao wataingiza mapato kupitia nini? Au watabaki wanakusanya ushuru wa taka??? Pili, kitendo hichi kina wingu kisiasa.

Mwisho, Bunge letu linatia shaka kuliko matumaini. Halina meno, limekuwa kibogoyo kumumunya maneno ya serikali. Halina changamoto kwa serikali, katika mazingira kama haya huwa sioni uhalali wa kuwepo kwake. Kama wanashindwa kuipa changamoto serikali kwenye masuala kma haya, uhai bunge uko wapi??

Una mtazamo gani kuhusu bajeti ya 2017 /18

"Noel Shao
[HASHTAG]#mjenziWaTanzaniaMpya[/HASHTAG]
Kodi ya mafuta imekuwa ikiongezeka kwa miaka mingi na road licence ikiwepo sasa imeongezeka kwa ongezeko la kawaida la shs 40, makelele ya nini wakati sasa wananchi wana uhuru wa ama kuilipa ama kutoilipa!Haya mafuta hupanda daily na kushuka sioni mantiki ya makelele haya
 
Tafsiri yake ni kuwa tutalipia Road licence ata sisi tusiomiliki vyombo vya usafiri, kingine km taifa bado tunawategemea wavuta fegi na walevi km mtaji wa kutusaidia kusukuma gurudumu la maendeleo.
Jambo ambalo si sahihi hata kidogo. Tunakosa mbinu mbadala ktk kukusanya kodi
 
Personally, naunga mkono kodi ya Motor Vehicle kuhamishiwa kwenye mafuta kwani kwa muda mrefu hii kodi imekuwa kero hasa kwa muda wote ambao imekuwa ikilipwa as a direct tax kwani imekuwa ikiwaathiri hata ambao magari yao yamekuwa grounded regardless of the time.

Naelewa hii kodi ilikuwepo ktk nchi kadhaa hata za jirani lakini nao waliihamishia kwenye mafuta possibly for similar reasons. Hivyo kilichofanyika hapa siyo ajabu hata kidogo.
 
Kuhusu hiyo kodi kuhamishiwa hadi kwenye mafuta ya taa ni sawa ili kupunguza uchakachuaji Wa mafuta na hilo la serikali kukusanya hadi mabango limekaa kisiasa zaidi ili halnashauri zisiwe na vyanzo vya mapato yao ya ndani
 
Halmashauri zitakusanya rambirambi pia ushuru wa sherehe kama harusi na ngoma ikiwemo tozo kwa Djs na MCs.
 
Upumbavu wa ccm na kufikiria matumbo yao badala ya wananchi ndo chanzo cha matatizo yote tuliyonayo
 
Tafsiri yake ni kuwa tutalipia Road licence ata sisi tusiomiliki vyombo vya usafiri, kingine km taifa bado tunawategemea wavuta fegi na walevi km mtaji wa kutusaidia kusukuma gurudumu la maendeleo.
Na cha kushangaza mwakilishi wetu kitwanga kaondolewa kwenye uwaziri...angetutetea
 
Utasikia wanasema wizara hazijapewa pesa za kutosha wakati bajeti inaonekana zimetwngewa kiasi cha kutosha
 
Kodi ya mafuta imekuwa ikiongezeka kwa miaka mingi na road licence ikiwepo sasa imeongezeka kwa ongezeko la kawaida la shs 40, makelele ya nini wakati sasa wananchi wana uhuru wa ama kuilipa ama kutoilipa!Haya mafuta hupanda daily na kushuka sioni mantiki ya makelele haya

Aisee, una kichwa kigumu kweli kweli kuelewa mantiki....

Ni kweli mafuta hupanda na kushuka bei kila wakati, kila siku.....

Lakini unasahau kuwa hii 40/= iliyoongezwa kwa kila lita ni fixed....

Mwezi huu kama lita ya petrol ni Tshs. 2200/= maana yake weka na ya Road Licence 40/= na kwa hiyo itakuwa 2240/=.... kwa kila mtu mwenye gari na asiye na gari !!

Mwezi ujao ikiwa 2150/= kwa lita, maana yake ongeza na ya Road Licence 40/= sawa na 2190/= kwa kila mtu mwenye gari na asiye kuwa nalo !!

Usiye na gari utalipaje hii kodi wakati huna gari ?

Ni rahisi tu, utalipia kwenye huduma zitokanazo na kutumia usafiri wa vyombo vya moto kama magari, Pilipili nk.... i. e nauli za usafiri wa abiria na bidhaa kupanda maradufu......

In return, ni kuwa, bei ya bidhaa itapanda am sema mfumko wa bei...!!!
 
Personally, naunga mkono kodi ya Motor Vehicle kuhamishiwa kwenye mafuta kwani kwa muda mrefu hii kodi imekuwa kero hasa kwa muda wote ambao imekuwa ikilipwa as a direct tax kwani imekuwa ikiwaathiri hata ambao magari yao yamekuwa grounded regardless of the time.

Naelewa hii kodi ilikuwepo ktk nchi kadhaa hata za jirani lakini nao waliihamishia kwenye mafuta possibly for similar reasons. Hivyo kilichofanyika hapa siyo ajabu hata kidogo.

Yes, mimi pia naunga mkono kwa sbb nina gari na natambua adha yake...

Lakini point kubwa hapa ni kuwa, ipunguzwe kiwe si zaidi ya Tshs. 15/=ama 20/= kwa lita badala ya hii 40/= ambayo ni kubwa mno...

Nadhani wabunge kuanzia j3 watakapoanza kujadili, walichukue hili na waone namna ya kulichambua na kulifanyia kazi badala kukata viuno, kucheza na kugonga meza tu bila ku - digest mambo na kutoa ushauri...!!
 
Watu wanatoka mapovu, Mara halmashauri zinakosa mapato yao, kwani Road License zilikuwa zinakusanywa na Halmashauri.
Kingine mapato mengi yaliyokuwa yanaenda katika halmashauri yalikuwa yanakuwa na figisu figisu nyingi. Uku katika halmashauri kuna wizi mwingi

 
B



3. Kitendo cha serikali kuu kuamua kukusanya ushuru hadi ule ulio kuwa unakusanywa na halimashauri mfano ushuru wa mabango kimenipa shaka mbili, moja, halimashauri wao wataingiza mapato kupitia nini? Au watabaki wanakusanya ushuru wa taka??? Pili, kitendo hichi kina wingu kisiasa.

Mwisho, Bunge letu linatia shaka kuliko matumaini. Halina meno, limekuwa kibogoyo kumumunya maneno ya serikali. Halina changamoto kwa serikali, katika mazingira kama haya huwa sioni uhalali wa kuwepo kwake. Kama wanashindwa kuipa changamoto serikali kwenye masuala kma haya, uhai bunge uko wapi??

Una mtazamo gani kuhusu bajeti ya 2017 /18

"Noel Shao
[HASHTAG]#mjenziWaTanzaniaMpya[/HASHTAG]

Ni mwendelezo w akodi za nyumba, kumbukaa silimia 90 ya halmashshuri zenye mapato haya zipo chini ya upinzani, na nyingi ni kwneye majiji. so ni ukomoaji wa madiwani washindwe kufanya miradi binfsi.
 
Watu wanatoka mapovu, Mara halmashauri zinakosa mapato yao, kwani Road License zilikuwa zinakusanywa na Halmashauri.
Kingine mapato mengi yaliyokuwa yanaenda katika halmashauri yalikuwa yanakuwa na figisu figisu nyingi. Uku katika halmashauri kuna wizi mwingi

shule za kata zimeleta vioja!
 
Back
Top Bottom