Nadhani Tanzania kuna upumbavu na upuuzi usioweza kuelezeka. Kuna haja gani ya kumsubiri Mwenyekiti Tume ya Uchaguzi aliyeko Dar es Salaam atangaze matokeo huku watu walikopiga kura hawakutangaziwa? Kama mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ndiye mwenye dhamana ya kutangaza, basi asubiri matokeo yote yafike kwake ili ayatangaze yote kwa pamoja. Sioni maana yoyote kwa mtu aliyepo Dar kutangaza matokeo ya kura wakati najua yeye anatangaza matokeo ambayo ameletewa, huku mimi niliyepiga kura zangu zilihesabiwa kwenye kituo na taarifa zinapatikana kwenye kituo na kwenda hadi kata na mwisho kwenye Jimbo la Uchaguzi.
Katika hili hakuna uwazi wowote zaidi ya kutufanya Watanzania kuwa ni mazezeta. Kitu cha kushangaza ni kuwa baadhi ya maeneo kura za ubunge zinalalamikiwa na hazijatangazwa hadi sasa hivi kwa kuwa wale wagombea wenyewe wanasimamia matokeo yanayotolewa. Ni wazi kwa upande wa Urais mgombea urais hawezi kujua matokeo yanayotolewa kutoka ngazi za chini, na hata akijua kutokana na taarifa toka maeneo husika hayupo pale Tume ya uchaguzi kupinga lolote. Kwa mazingira haya kuna haja ya yale yanayofanywa na Tume?
Katika hili hakuna uwazi wowote zaidi ya kutufanya Watanzania kuwa ni mazezeta. Kitu cha kushangaza ni kuwa baadhi ya maeneo kura za ubunge zinalalamikiwa na hazijatangazwa hadi sasa hivi kwa kuwa wale wagombea wenyewe wanasimamia matokeo yanayotolewa. Ni wazi kwa upande wa Urais mgombea urais hawezi kujua matokeo yanayotolewa kutoka ngazi za chini, na hata akijua kutokana na taarifa toka maeneo husika hayupo pale Tume ya uchaguzi kupinga lolote. Kwa mazingira haya kuna haja ya yale yanayofanywa na Tume?