Elections 2010 Kuna maana ya Kutangaza Matokeo ya Urais?

Gurtu

JF-Expert Member
May 15, 2010
1,247
342
Nadhani Tanzania kuna upumbavu na upuuzi usioweza kuelezeka. Kuna haja gani ya kumsubiri Mwenyekiti Tume ya Uchaguzi aliyeko Dar es Salaam atangaze matokeo huku watu walikopiga kura hawakutangaziwa? Kama mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ndiye mwenye dhamana ya kutangaza, basi asubiri matokeo yote yafike kwake ili ayatangaze yote kwa pamoja. Sioni maana yoyote kwa mtu aliyepo Dar kutangaza matokeo ya kura wakati najua yeye anatangaza matokeo ambayo ameletewa, huku mimi niliyepiga kura zangu zilihesabiwa kwenye kituo na taarifa zinapatikana kwenye kituo na kwenda hadi kata na mwisho kwenye Jimbo la Uchaguzi.

Katika hili hakuna uwazi wowote zaidi ya kutufanya Watanzania kuwa ni mazezeta. Kitu cha kushangaza ni kuwa baadhi ya maeneo kura za ubunge zinalalamikiwa na hazijatangazwa hadi sasa hivi kwa kuwa wale wagombea wenyewe wanasimamia matokeo yanayotolewa. Ni wazi kwa upande wa Urais mgombea urais hawezi kujua matokeo yanayotolewa kutoka ngazi za chini, na hata akijua kutokana na taarifa toka maeneo husika hayupo pale Tume ya uchaguzi kupinga lolote. Kwa mazingira haya kuna haja ya yale yanayofanywa na Tume?
 
mkuu hili jambo hata mimi limenishangaza sana. kwa kweli tanzania demokrasia bado kabisa. Nasubiri kuona hiyo report ya hao wanaojiita external observer. Nina hamu ya kujua wataandika nini! Maana kuna kila dalili kwamba uchakachuaji ulikuwa ni wa kiasi kikubwa sana.
 
Huu ni wizi, lakini ingawa kwasasa tunaumia tuvumilie maana 2015 tutawashinda kilaini maana wameficha sehemu ambazo wameshindwa kwahiyo hawajui wapi waongeze nguvu. Kwasababu si sehemu zote zenye wabunge wa CCM walimpigia JK:smile-big:
 
Nonononononoooooo hatuwezi kuvumilia wizi mkubwa na wa waziwazi kiasi hiki. Hata dunia itatushangaa. Wazo la kusubiri 2015 tuliondoe kabisa kwenye vichwa vyetu. Ujambazi wa ccm lazima ushughulikiwe mwaka huuhuu kabla ya kuingia 2015. Chadema na wananchi kwa ujumla huu ndiyo mwaka wa kufanya mapinduzi mpaka dunia ihamishie vyombo vya habari hapa. Kwa udi na uvumba lazima kura zihesabiwe upya.

Ole wako jaji makame, mwombe shetani wako usiwe juu ya uso wa dunia hii, wakati nchi itakapokuwa chini ya utawala wa wazalendo. Kichwa chako kitazungushwa mitaani kama embe ili kutoa fundisho kwa wazee wengine wasio na uchungu na hatma ya nchi yao. Siku hiyo, siyo kwamba ipo bali ipo mlangoni inabisha hodi. Watanzania tusidanganyike, 2015 tutafanyiwa ujambazi mwingine halafu tutaendelea kujipa moyo wa kusubiri 2020. Hapana, tusifanye upuuzi huo. Kikwete na mafisadi wake wote wataondoka kwa kelele zetu wanyonge.
 
dar es salaam, slaa ameongoza sana kuwaacha mbali wenzake ila mtashangazwa na moyokeo yake.

Kura za Slaa zimewekwa kwa kikwete, za kikwete kapewa lipumba na za lipumba kapewa slaa. mnaona mchezo huo??
NCHI IPO SHAKANI
 
kikwete na watu wako mafisadi mliokosa huruma na watanzania kwa nini mlituambia tupige kura ndiyo demokrasia, hiyo demokrasia iko wapi si mngeendelea kututawala kiudikteta kama mnavyofanya sasa au mnasubiri mkaaapishe zanzibar halafu mrudi huku mtutangazie upumbavu wenu kuna faida gani ya kupiga kura wakati matokeo mnapanga wenyewe. Next time msitudanganye uchaguzi huru na wa haki my a'''''tuishi tu kama somalia kieleweke.Kibaya zaidi hiyo NEC inayoongozwa na mtu karibu anachungulia kaburi 'yes i said anachungulia kaburi' haisemi hata ni kwa nini hawatangazi matokeo.Ninyi wendawazimu mnacheza kweli na akili za watanzania kwa kutuendesha kama gari lililokosa matairi. TUSILAUMIANE WAJAMENI. TUONANE MTONI TUTAKUSANYIKA MTONI
 
God only can punish JK and his team. Let us continue praying. Please take a look at my avatar!
 
Back
Top Bottom