Mimi ni Muislamu na Mwenyezi Mungu amenijaalia nimewahi kuhiji pia. Alhamdulillah.
Siku moja nilimuuliza Sheikh, "masharti ya mtu kuwa Muislam ni yapi?" Akaniambia ni kukiri kwa moyo na kutamka kwa ulimi kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa isipokuwa Allah peke yake na Muhammad SAW ni mtume na mjumbe wake.
Sharti jingine ni kufuata yote yaliyoamrishwa na Mwenyewe Subhanahu Wataala na kuyaacha yaliyokatazwa Naye. Subhanallah!
Nikamuuliza, "ni hayo tu?" Akanijibu, Naam, ni hayo tu. Nikamuuliza, "jina je, ni lazima nipewe jina la Kiislamu?" Akaniambia, hakuna jina la Kiislamu. Haya majina tuyatumiayo ni majina ya Kiarabu. Kuna Waarabu wasiokuwa Waislamu wanaitwa majina hayo hayo. Unamkumbuka Tariq Azizi? akaniuliza, nikamwambia ndio namkumbuka. Akaniambia, "hakuwa Muislamu yule.
Sasa nikaanza kutatizwa hivi kwa nini sisi Waafrika tunaacha kutumia majina yetu ya Kiafrika, tunayapenda ya Kiarabu tukiwa ni Waislamu na ya Kizungu tukiwa ni Wakristo. Hii maana yake ni nini?
Kwani Alhaj Kipesile Mwaitobo hawezi kuwa Muislamu au Reverend Kitogo Mazengo hawezi kuwa Mkristo? Mara nyingi ni sisi tu Waafrika. Wagiriki wana majina yao ya kigiriki na Wataliano wanatumia ya kwao ya kitaliano. Kwanini sisi mpaka tuwe George au Abdallah ndio iwe uthibitisho wa imani zetu za kiroho?
Siku moja nilimuuliza Sheikh, "masharti ya mtu kuwa Muislam ni yapi?" Akaniambia ni kukiri kwa moyo na kutamka kwa ulimi kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa isipokuwa Allah peke yake na Muhammad SAW ni mtume na mjumbe wake.
Sharti jingine ni kufuata yote yaliyoamrishwa na Mwenyewe Subhanahu Wataala na kuyaacha yaliyokatazwa Naye. Subhanallah!
Nikamuuliza, "ni hayo tu?" Akanijibu, Naam, ni hayo tu. Nikamuuliza, "jina je, ni lazima nipewe jina la Kiislamu?" Akaniambia, hakuna jina la Kiislamu. Haya majina tuyatumiayo ni majina ya Kiarabu. Kuna Waarabu wasiokuwa Waislamu wanaitwa majina hayo hayo. Unamkumbuka Tariq Azizi? akaniuliza, nikamwambia ndio namkumbuka. Akaniambia, "hakuwa Muislamu yule.
Sasa nikaanza kutatizwa hivi kwa nini sisi Waafrika tunaacha kutumia majina yetu ya Kiafrika, tunayapenda ya Kiarabu tukiwa ni Waislamu na ya Kizungu tukiwa ni Wakristo. Hii maana yake ni nini?
Kwani Alhaj Kipesile Mwaitobo hawezi kuwa Muislamu au Reverend Kitogo Mazengo hawezi kuwa Mkristo? Mara nyingi ni sisi tu Waafrika. Wagiriki wana majina yao ya kigiriki na Wataliano wanatumia ya kwao ya kitaliano. Kwanini sisi mpaka tuwe George au Abdallah ndio iwe uthibitisho wa imani zetu za kiroho?