Miss Kyalla
Senior Member
- May 13, 2019
- 168
- 135
Kuna kitu hapa wanaume au kina baba hawatakiwi kukichukulia poa, nilelewa na kukulia kwenye familia ya wazazi wote wawili lkn mama ndio alikuwa kila kitu pale home namshukuru Mungu na mzee yeye alikuwaga na mambo yake mwenyewe mwenyewe yani hakuwa friendly na sisi,so tulikuwa hivyoo. Sasa ile hali huwa inaniathiri sana kwanzia nimeanza kujielewa nikiona rafiki zangu baba kaninunulia hiki, nilisafiri na baba, yan wao baba babaa nilikuwa naona wivu sanaa, saivi nimekuwa binti mkubwa tuu bado rafiki zangu tukikaa utaskia ntamwomba baba anisaport, nitaongea na baba, kwenye masend off baba zao wanawapa mazawadi makubwa makubwa yaani wao baba, baba na wao, mimi sasa, nimesota na maisha weee baba wakumwomba anisaidie tatizo langu hakuna saivi katangulia mbele za haki bado kuna mambo yanatokea nazidi kumisi uwepo wake, jamani huwa naumia sana kukosa mapenzi haya ya mzazi mmoja natamani nipate Mume anidekeze haswa niiskie raha ya hawa viumbe wa kiume huku duniani maana mpaka saivi bado sijaiona zaidi ya kunikaba siku moja kunipora kuumizwa yani huwaga nawaangaliaga tuu kaka zangu na haswa pacha wangu niliemfanya ndio babangu ndio wananifanyaga niwawazie positive hawa wanaume.
Sasa basi wewe baba au baba mtarajiwa jitahidi kuwapenda wanao na kuwapa mapenzi kadri uwezavyoo usikae mbali na watoto hata kama hauna kitu hii kitu inaathiri sana kisaikolojia.
Lakin namshukuru Mungu kwa maisha na Kumwombea mama yangu maisha marefu zaidi dunianii
Sasa basi wewe baba au baba mtarajiwa jitahidi kuwapenda wanao na kuwapa mapenzi kadri uwezavyoo usikae mbali na watoto hata kama hauna kitu hii kitu inaathiri sana kisaikolojia.
Lakin namshukuru Mungu kwa maisha na Kumwombea mama yangu maisha marefu zaidi dunianii