Kuna kila dalili za nchi kumeingia vitani bila kujiandaa..al shabaab

Ryaro wa Ryaro

JF-Expert Member
Oct 4, 2010
2,659
1,422
Katika kali ya kawaida huwezi kuamini kwa nini Tanzania inataka kujiingiza kwenye vita isiyokuwa na macho. Nimefuatilia kwa ukaribu kabisa na kuona kwamba tunajitafutia matatizo makubwa kwa kile kinachoonekana kama kuutokomeza Uhalamia wa Kisomalia ( Al-shaaba). Nimesikia matamko ya vingozi wetu kwenye international arena ( fora) na kinachoonekana sasa ni Al-shabaab. kwa nini tuingie kwenye vita na hawa mahalamia wakati tunajua kuwa ni ngumu. Tujiulize kwanza khali ya maisha ya watanzania kwa sasa Kiuchumi tupo taabani kabisa na kwa nini sasa tujikite kwenye vita isiyo na macho. Tuwaache Majilani waendelee na hiyo vita lakini matokeo yake ni wazi kuwa HAKUNA ushindi pale i.e tuangalie NATO na Afganistan na na tutaona ni nini majilani zetu watakivuna toka kwa Ma piracy wa Kisomalia..
Tujikite kutatua matatizo yetu kwanza na tuwe makini kwa hili maana viongozi wetu wa kisiasa wanataka kutupeleka ndiko siko.
 
which is better? Kuwaacha alshabab waendelee kutamba au kupunguza angalau nguvu zao? Kuwaacha hawa jamaa bila action ni kuongeza ukubwa wa tatizo
 
Tujihami nao hawa jamaa.tujiandae kupambana nao.We cant be a friend of devil.they will not spare us kwa kujifanya ni marafiki zao rather,watatafuta namna ya kujiimarisha zaidi.we should join the international arena to fight terrorism at any cost.
 
Kenya walikuwa na mtazamo huo huowa kutowashambulia Al shabaab kwa miaka zaidi ya ishirini iliyopita na kwa muda wote walikuwa wakitoa misaada kwa wakimbizi. Hilo halikusaidia kuwafanya wasishambuliwe na magaidi wa kisomali na zaidi ya yote Al shabaab walijikita zaidi Kenya kiuchumi hata kuliko Somalia na sasa wanaathiri vivutio vyao vya utalii na uchumi wa Kenya. Ukweli ni kuwa kukaa kimya na kutokuchukua hatua yoyote hakutawazuia Al shabaab kuteka meli au kushambulia. Sana sana unawapa muda na uwezo wa kuenga mitandao ya kigaidi. Mimi nadhani tungeanza harakati za "kiinteligensia" kufuatilia nyendo za Al shabaab nchini ili tuwashughulikie mapema kabla hawajajiimarisha na kuelekeza mashambulizi yao dhidi ya uchumi wetu.
 
Kuna habari nyingi sana kwamba viongozi kadhaa kwene serikali yetu wamekuwa wakitaka kuwatumia hawa jamaa (Al-Shabaab) kuwanyonga wapigania haki wa nchii na taarifa zilishapelekwa kwa wana-usalama ambao hawakuchukua hatua tulizoziona, labda walichukua hatua za siri kama ambavyo walitaka kuwatumia kwa siri. Nahisi anachoongea JK ni kuidhihirishia jumuiya ya Kimataifa kwamba anapinga ubazazi wa Al-Shabaab, lakini huku nyuma ya pazia kama kawaida yake atakuwa anawasiliana nao na kuwaambia "msijali mimi napiga mdomo tu kuridhisha wapiga kelele"

Upande wa pili ni wa hatari sana, kama ni kweli JK anaongea tu kwa kuwa ndio dunia yote inavyosema... basi tuko kwenye hatari kubwa sana. Kwanza tukumbuke kwamba kabla haya hayajaja JK mwenyewe ameipamba sana dhana ya udini na imeshashika kasi vya kutosha, iwapo tu itatokea Al-Shabaab wakaamua kuja Tanzania basi tujue tutakuwa kwenye shida kubwa tena ya muda mrefu sana. Al-Shabaab wanafanya kazi kwa kutafuta wanachama wapya na kuwafunza kila inapowezekana, watapata wanachama wengi na kwa haraka sana hapa kwa sababu zifuatazo;
  • Udini ulioanzishwa na JK umeshashika kasi kiasi kwamba Waislamu wengi wanaweza kushawishika kirahisi sana kushambulia wakristo kwa sasa, hii ni kwasababu Al-Shabaab ni Waislam na hutumia ushawishi mkubwa wa dini kwenye vita yao siku zote.
  • Hali ya Watanzania Kifedha ni ngumu sana kwa sasa, ni rahisi kuwashawishi wote (Waislamu na Wakristo) kuingia Al-Shabaab kwa nguvu ya fedha na kujikuta tukilipuana wenyewe huenda hata Al-Shabaab wakiwa hawapo kwenye nchi hii.
  • Tayari kuna habari nyingi kwamba kuna viongozi walishakuwa na mawasiliano na hawa jamaa, kama ni kweli kuna uwezekano mkubwa hawa hawa viongozi wakatumia nafasi hiyo kuwafanyia kazi wabaya wao ama kuyashambulia makundi ambayo wangependa yaathirike zaidi na hali itakavyokuwa.
  • Al-Shabaab hawajikusanyi mahala ili muwashambulie, wao hujificha kisha hushambulia kwa kuvizia. Usalama wa Taifa wa wakati huo wa Mwl. ungefanya kazi, kwa sasa hakuna Usalama wa Taifa na kuwageuza wananchi watoe taarifa itachukua muda maana tayari polisi wameshawageuka wananchi kwa kuwa waonevu wakubwa kiasi kwamba wananchi wanaweza kufikia kuwaamini Al-Shabaab kuliko hata polisi wetu. Polisi jamii ni usanii usio na mashiko kwa sasa hivi, ni dhana nzuri isiyofanyiwa kazi kwa sasa. Ukitaka kujua katoe taarifa kwamba Mkubwa anaiba uone nini kitatokea.
Hizi ni sababu chache ninazoziona zinaweza kuleta hatari kubwa, tujaribu kutafakari kwa upana wake. Nahisi ni bora vita kabisa kuliko kuwa na watu kama Al-Shabaab maana vita yao haiishi. Angalieni hapo Libya vita ya miezi kadhaa imeisha maana target zilikuwa zinaonekana, hapo Iraq ni miaka na vita haiishi imekuwa kama kidonda kisichopona maana jamaa si taifa fulani na hawana makao maalum, wanatumia popote penye nafasi kujijenga na hushambulia kwa mtindo huo huo. Kuendeleza vita ya Al-Shabaab ni kuendeleza vita isiyoisha, hawa Kenya wenyewe wameshasema kabisa kuwa wako tayari kukaa mezani na kuongea na Al-Shabaab. Kumbukeni Kenya wako uwanjani na wanakiona kinachotokea, sisi hatujui chochote tunaingia tu ushabiki wa kusema mara wapigwe.., wakija tutawapiga.., ooh Kenya songeni mbele.., mara JK sema tu hakuna tatizo na mambo mengine mengi. Hapa tulipo yawezekana tunao Al-Shabaab wengi tu wametulia kila mahali wanasubiri maelekezo, ninyi mnasema oooh uhamiaji watafunga mipaka...wapi??? Hakuna usalama hapa, tuwe makini na maneno yetu kabla hatujafikia kuongelea mambo kama haya.

Huyu jamaa aliyehukumiwa hapa Kenya juzi alifanya kwa shurti yake mwenyewe na ameikubali hukumu yake bila tatizo, mnajua tunao wangapi wa namna hii hapa Tanzania? Mnajua traffic ya watu wetu kwenda na kurudi Somalia, Pakistan, Afghanistan na kwingineko ikoje? Mnajua watanzania wanajifunza nini kwenye makanisa na misikiti yao?
 
Yes, ngoja twende vitani tukaclean weapons,kupunguza uvivu wa askari maake wanasiku nyingi hawajaingia vitani,slaa zetu zina kutu ngoja tukazisafishe kwa hawa ali shabib...
 
Nitapenda kuendelea kusoma , ila kama kweli hao jamaa watakuja TZ kama ambavyo wakati fulani onyo lilitolewa Arusha basi uchumi utalala mara 500 zaidi ya hapa .Uwekezaji utaishia na kama wanadhani utani waendelee waone na hizo mbinu chafu .
 
vita dhidi ya ali-shababu si ngumu kama mnavyofikiria, wakijaribu, tunawakusanya wooote wenye asili asili ya somalia, tunawapakiza kwenye meli tunawapeleka kismayu kwao somalia, twawapa chakula kuwatosha miezi mitatu, twawapa pia mbegu wakalime, hatujali kama huyu ni bashe rage wala kinana, ili lisiwakumbe wawadhibiti hao wasomali wenzao.
 
Back
Top Bottom