Unaona Simba wapo sahihi kwa hili au umeandika ili ujaze page tuKumekuwapo na sakata siku mbili hizi kati ya msemaji wa Simba, Haji Manara na mtangazaji wa Wasafi FM, Maulid Kitenge.
Hii ni baada ya Kitenge kupost kwenye page zake kwamba kuna ugomvi kati ya Morrison na kocha wake Gomes, na ndio maana Morrison aliachwa Dar safari ya Khartoum, madai ambayo Manara aliyakanusha na kumuonya Kitenge aache uzushi.
Leo katika kipindi cha michezo asubuhi, amehojiwa CEO wa Simba, akakanusha kuwapo ugomvi huo na akadai ni waandishi tu wanaotafuta followers kwenye pages zao ndio wanazusha hilo. Pia akahojiwa kocha Gomes kama ana ugomvi na kwa nini alimuacha Dar, akasema taarifa hizo si za kweli na Morrison ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa ambaye atawasaidia sana Simba, na akasema alimuacha Dar kwa sababu za matatizo ya kifamilia.
Pamoja na ufafanuzi huo wa CEO na kocha mwenyewe, lakini bado Kitenge akawa anamlazimisha Zingizi aongelee ugomvi ili kuhalalisha habari yake ya mitandaoni, na wakati wakizungumza hayo, wachambuzi wengine wa soka akina Musa, Ambangile nk waliamua kupiga kimya kuwaachia Kitenge na Zingizi wakifarijiana kuwa CEO na kocha wamekanusha tu ila kuna habari wao wanazo, hadi ikafikia hatua ya Ambangile kuvunja ukimya na kuanzisha habari nyingine mpya.
Kitendo cha wachambuzi wenye akili zao kuamua kukalia kimya ushawishi wa Kitenge ili wasiwaamini CEO na Gomes kimenifanya nipate picha kuwa huenda waliona watajiondolea heshima kujadili kitu ambacho kimeshakanushwa, tena mmoja wa wakanushaji nihuyo huyo Gomes anayehusishwa na ugomvi!
Hongera Musa Kawambwa, George Ambangile na wachambuzi wote mliokuwapo studio kwa kumuachia Kitenge alibebe zigo lake, wala asiwasumbue, mpeni makavu!