Tunaendelea kuwapeni habari zetu za tathmini. Bado timu iko visiwani ikitupatia tathmini mbali mbali za kisiasa na kijamii.
Huko visiwani kuna kijungu chapagwa.
Picha halisi ilioyoko huko ni kuwa baada ya CCM kumteua Dkt Hussein Mwinyi, kwenye jamii kuna fundo la chini chini. Mara HII KAMPENI NI RAHISI MNO KWA WAPINZANI , Tayari huko kuna sauti zinavuma,
"Hatma ya Zanzibar" Hili neno lipigiwe mstari sana, Wenyewe wanasema ulioitwa ukoloni sasa unaelekea kutaka kurasimishwa na kuimaliza Zanzibar
Ujio wa Dkt Mwinyi si tu kwamba ulikataliwa ndani ya CCM kindaki ndaki kwa wenyeji wa Zanzibar, lakini unatafsiriwa ndio unataka kuhitimisha uwepo wa Zanzibar katika ramani.
Watafiti fuatilieni. Zanzibar kuna hofu iliyofichwa na wenyewe wanaambizana. " uchaguzi wa 2020" umebainisha mengi , Ni vita ya CCM asili Zanzibar na CCM kutoka bara. huo ukweli hausemwi.
Katikati ya hilo kuna upinzani wenye nguvu ambao wenyewe unajitosheleza. Mjadala unaendelea kuhusu hatma ya ZANZIBAR na ujio wa Dkt Hussein Mwinyi.
Siasa za Muungano na Maslahi ya Zanzibar yanatajwa sana na kuingizwa nasabu za watu na asili zao.
Hii misemo ipo na kuna tahadhari kubwa inachukuliwa na makundi mbali mnbali ya kisiasa na kijamii.
Kazi ipo kweli kweli. Tunasubiri upepo wa kampeni uanze tuweze kuwajuza zaidi.
Kishada
Huko visiwani kuna kijungu chapagwa.
Picha halisi ilioyoko huko ni kuwa baada ya CCM kumteua Dkt Hussein Mwinyi, kwenye jamii kuna fundo la chini chini. Mara HII KAMPENI NI RAHISI MNO KWA WAPINZANI , Tayari huko kuna sauti zinavuma,
"Hatma ya Zanzibar" Hili neno lipigiwe mstari sana, Wenyewe wanasema ulioitwa ukoloni sasa unaelekea kutaka kurasimishwa na kuimaliza Zanzibar
Ujio wa Dkt Mwinyi si tu kwamba ulikataliwa ndani ya CCM kindaki ndaki kwa wenyeji wa Zanzibar, lakini unatafsiriwa ndio unataka kuhitimisha uwepo wa Zanzibar katika ramani.
Watafiti fuatilieni. Zanzibar kuna hofu iliyofichwa na wenyewe wanaambizana. " uchaguzi wa 2020" umebainisha mengi , Ni vita ya CCM asili Zanzibar na CCM kutoka bara. huo ukweli hausemwi.
Katikati ya hilo kuna upinzani wenye nguvu ambao wenyewe unajitosheleza. Mjadala unaendelea kuhusu hatma ya ZANZIBAR na ujio wa Dkt Hussein Mwinyi.
Siasa za Muungano na Maslahi ya Zanzibar yanatajwa sana na kuingizwa nasabu za watu na asili zao.
Hii misemo ipo na kuna tahadhari kubwa inachukuliwa na makundi mbali mnbali ya kisiasa na kijamii.
Kazi ipo kweli kweli. Tunasubiri upepo wa kampeni uanze tuweze kuwajuza zaidi.
Kishada