Kuna karatasi yako moja muhimu hutaiona!

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,605
696,697
Dunia ya makaratasi.. Ndivyo ninavyoweza kusema. Makaratasi yaitwayo nyaraka ndio yanaiongoza dunia

Makaratasi ya vibali mbalimbali
Makaratasi ya vyeti mbalimbali
Makaratasi ya pesa mbalimbali
Makaratasi ya mikataba mbalimbali
Makaratasi ya hati za kusafiria
Makaratasi ya utambuzi nknk

Tangu kuzaliwa mpaka kufa ni makaratasi ndio yanatuongoza, kuanzia nyumbani, makazini, michezoni, kwenye biashara, sanaa, ubunifu, mahusiano, viwango vya elimu nknk.! Bila makaratasi hutambuliki kwa chochote kile, huaminiki wala hujulikani.

Karatasi ndio zitakutambulisha siku na mahali pa kuzaliwa na mwaka pia
Karatasi ndio zitatambulisha viwango vyako vya elimu
Karatasi ndio zitatambulisha mahusiano yako kisheria
Makaratasi ndio yatatambulisha vitu na mali unazomiliki
Makaratasi ndio yataamua kiwango cha ukwasi ama ufukara wako

Hivyo basi daima sisi ni watu wa makaratasi na tunayatunza kweli kweli. Ni karatasi hiyo hiyo inayotengenezwa kutokana na miti ndio tunaitumia hiyo hiyo kuhimiza watu wasikate miti

Kwenye makabati yetu tunayo makaratasi mengi tu tumeyatunza vema na yakipotea tunapata tabu kweli LAKINI kuna karatasi moja tu linalokuhusu sana wewe pekeyako ambalo hutakaa ulione.. Nalo ni katarasi litakaloandikwa kuthibitisha mwisho wako.

Linaitwa HATI YA KIFO. Hili watabaki nalo utakaowaacha na ndio litakuwa MUHIMU kuliko yale yote uliyoyatunza maisha yako yote.

giphy.gif
 
Na hii karatasi wataitumia kutafuta na kuchukua pesa na mali zako zote.

WTF...
Ni zaidi ya hayo... Kuna vyeti vya vifo licha ya kuandikwa sababu za kifo lakini huongezewa alama maalum ya kimataifa (ICD)International Classification of Disease!] kutambulisha asili ya tatizo kama TB, Polio nknk na vingine hutambulisha kama ugonjwa uliomchukua marehemu ni kizalia au wa kuambukiza
Lakini kwa kesi ya corona sio coded number ni mhuri
pasted-image-0-1.jpg
 
Mkuu, ikitokea umekufa baharini kwa kumezwa na papa au kupotea na ndege kama ile ya malaysia nadhani cheti hiki hakitakuwa issued kwako. Maana kutakuwa hakuna proof ya kifo chako. Hvi ikitokea scenario kama hii huwa inakuwaje? Kwa mfano ukapotea na ndege kama Malaysian airways.
 
Mkuu mbona una tufikirisha mambo ambayo hatujui mwisho wake!!

🙆🙆 Ata kabla ya cheti cha kifo wata ulizana tunamzika saa ngapi🙆

Wengine apo apo mbele ya maiti kama vile kalala!! Kafa kweli?

🙆 wengine mbele ya maiti nani analinda nyumbani na ofisini wasije iba!!

🙆Wingine angalia pochi haina nyaraka za benki zisije potea!!

🙆 wengine mbele ya mke wako
Simu zote na card za banki apewe shangazi akaye nazo kwanza😭

🙆mwingine mjomba kaacha pesa nyingi hakuna haja ya mchango tumzike kwa pesa zake leo Adhuhuri😭

Kwenye maisha tuishi kwa upendo na amani mwisho wa mwanaadamu hakuna kimfacho sio watoto wala mali!
 

Similar Discussions

28 Reactions
Reply
Back
Top Bottom