Clepatina

JF-Expert Member
Apr 8, 2023
1,268
2,553
Shaloom,

Dada mmoja aliamini kuwa mtu pekee anayestahili kuitoa bikra yake ni mwanaume atakayemuoa. Huu msimamo wa bibie ulifanya apoteze wachumba wengi kwani walipoambiwa hawataonja asali mpaka waingie ndoani walisepa.

Miaka ikaenda, umri wa dada ukazidi kusogea ila bibie hakubadili msimamo wake. Aliendelea kuitunza bikra yake na kuishi maisha ya heshima kama ambvyo binti yeyote mwenye maadili anapaswa kuishi.

Walokole tuna kamsemo ketu kuwa, wakati wa Mungu ndio wakati sahihi na kweli "Wakati wa Mungu ulipofika" bibie akaposwa na kijana aishie huko Marekani. Kilichomvutia kijana kwa bibie ni habari alizozisikia kuwa bibie hajawahi kuguswa na mwanaume yeyote.

Kijana akatuma washenga, akatoa mahari na kufanya taratibu zote ikabakia ndoa tu ambayo ingefungwa baada ya yeye kwenda Marekani na kurudi tena Tanzania.

Basi ikawa rasmi kuwa bibie sasa ni mke mrarajiwa wa mtu aishie Marekani. Viongozi wa kanisa na wazazi wakawa wanamtumia bibie kama mfano wa kuwaasa watoto wa kike kuwa ukijitunza Mungu atakuletea mume bora. Mabinti wakaambiwa si mnaona mwenzenu kajitunza sasa anaolewa na kwenda kuishi Marekani?

Basi bwana siku za mume mtarajiwa kurudi marekani zikakaribia na akaomba aende Dar na mkewe mtarajiwa akamfanyie shopping pamoja na kumuachia mradi wa ujenzi wa jumba lao lililoko Dar ausimamie.

Kwa vile kijana alishafanya taratibu zote wazee wakaona haina shida wakamruhusu binti asafiri na mumewe mtarajiwa kutoka mkoani kwao mpaka Dar.

Kufika Dar wakashukia hotel na huko kijana baada ya kushindwa kumshawishi binti atoe uroda kabla ya ndoa akatumia njia ya kumlewesha na ndipo akafanikiwa kuitoa bikra ya binti kabla ya ndoa.

Dada alilia sana alipozinduka na kujua kikichotokea, ila kijana wa Marekani akafanikiwa kumtuliza dada kwa maneno matamu matamu na ahadi ya kumpenda mpaka kifo kiwatenganishe. Dada akafanyiwa shopping kisha jamaa akakwea pipa akarudi state na bibie akarudi mkoani kwao.

Baada ya week kadhaa dada akagundua ana ujauzito wa mumewe mtarajiwa. Wazee wakajua na kijana wa Marekani akajulishwa na kuombwa kufanya hima aje aoe mkewe na kuondoka nae kabla wambea hawajajua kuwa ile bikra iliyotunzwa kwa miaka mingi ishatolewa kabla ya ndoa.

Kijana wa Marekani akazipokea habari kwa furaha na kuwaahidi wazee kuja ASAP lakini mpaka muda wa mtoto kuzaliwa ukafika ila kijana wa Kimarekani hakutokea.

Baada ya miaka kadhaa ikaja kugundulika kuwa kijana wa Kimarekani alikua ni muhuni tu aliyekuwa na fantansy ya kuchakata bikra na eti hata wakati anatoa ile mahari alikua tayari keshaoa zake huko Marekani na wale washenga aliowatuma walikua ni wahuni wenzie tu wazee wa hovyo, maana wazazi wake wa kweli walipofuatwa walishangaa sababu wao wanajua kijana wao alishaoa siku nyingi tu.

Ikawa asubuhi ikawa jioni dada mrembo aliyeishi kwa maadili akajikuta akichukua kadi yake kwenye chama kubwa la single mothers nchini.

Chama ambacho wanaume wa Kitanzania huwaona wanachama wote wa chama hicho ni wanawake wasiofaa sio kuoa tu bali hata kwa mahusiano ya kudumu, bali kwa kuwagonga na kukimbia haraka uwezavyo kuokoa maisha yako.

Kabla sijajiunga JF nilikua nawaona single mother ni wanawake kama wanawake wengine. Wako wanaojitambua, wako empty sets. Wako wanaojiheshimu, wako micharuko. Wako wapole na wanyenyekevu wako vichomi pia. Inshort tabia zote za wanawake single mothers utazipata hata kwa wanawake wasio single mothers.

U single mother sio laana ambayo automatically inamfanya mwanamke awe na tabia za hovyo kama hakua hivyo mwanzo na wala kutokuwa single mother sio baraka/neema/kinga ya kumfanya mwanamke awe wa maadili/bora.

Mwanamke yeyote single mother or not, tabia zake zinatokana na malezi au mtazamo wake katika maisha.

Mimi sio single mother ila as long as mim ni mwanamke kama ilivyokuwa kwa bibie mtunza bikra, hata mimi iko siku naweza kuangukia kwa bazazi nikalielewa tukadanganyana danganyana pale at the end of the day bila kujua imekuwa kuwaje nikajikuta na mimi nachukua kadi kwenye chama kubwa la single mothers.

Ikitokea nimekua single mother sitapenda kuongelewa kwa namna single mother wanaongelewa hapa JF.

Hapa JF single mother wanaongelewa kama jamii ya watu wenye laana wanaopaswa kutengwa kama walivyotengwa wale wakoma wa kwenye biblia.

Hapa JF wanaume mnawaongelea single mothers kama viumbe wasio na akili wala maadili, lakini naomba niwaambie hawa single mothers ni nyie mmewatengeneza na tena ni kundi la wanawake wenye akili kubwa na ndio maana wanaweza kulea na kusomesha watoto wao ambao baadhi yenu mmewakataa na kuona ni bora hela yako ununulie msambwanda wa barmaid kuliko kununua daftari za mwanao.

Sio ajabu yule kijana wa Marekani nae yuko hapa JF akiandika nyuzi za kuwaongelea single mother kama walaaniwa kumbe yeye ndio mlaaniwa.

Naombeni wanaume wa JF mtoe hiyo lebel mliyowapachika single mothers, sio sawa duniani wala mbinguni sababu hamjui mwanamke amepitia mitihani gani mpaka kuishia kuwa single mother.

Naomba viongozi wa JamiiForums muliangalie hili. Kuna single mother anaweza kujiua akifikiria aliyopitia na kulinganisha namma jamii inavyomhukumu. Sio sawa jamii kusema watu wote wa kundi fulani wana tabia fulani kwani hiyo sio kweli na sio sawa.

Iweje mwanamke aliyeishi maisha yake yote kwa kujitunza na kujiheshimu halafu badae jamii imuone takataka kisa tu analea mtoto/watoto wake bila baba?

NB: Wanawake wa JF njooni tuwaeleweshe wanaume wetu kwa heshima na upendo kuwa kunyanyapaa single mothers sio sawa. Maana kama leo sio single mother kesho unaweza ukajikuta single mother au binti yako akawa single mother. Utapenda anyanyapaliwe?

Hata wewe mwanaume unayenyanyapaa single mothers leo huwezi jua iko siku wanaume wenzio watamdanganya aishie kuwa single mother. Utapenda jamii imnyanyapae?
 
1684567494938.png
 
Huwa sipendagi kuchangia mada za single mothers, maana zinahusu hisia sana.

Sio kwamba sinaga vya kuongelea, la hasha, nachagua tu kuwa msomaji.

Ninachoweza sema, wanaoponda single mothers huwa wanasababu zao, na pia single mothers wanaoponda wanaume, nao wanasababu zao. Na sometime pande zote mbili huwa na sababu zenye mashiko.

Ninachoweza kukwambia Clepatina huwezi kuyaelewa maumivu halisi ya single mothers kwa kusoma habari zao humu JF jinsi wanavyo nangwa. Na pia huwezi elewa maumivu ya upande wa pili kwa kuangalia maandiko jinsi wanavyo wananga single mothers
 
Shaloom.

Dada mmoja aliamini kuwa mtu pekee anayestahili kuitoa bikra yake ni mwanaume atakayemuoa.

Huu msimamo wa bibie ulifanya apoteze "wachumba" wengi kwani walipoambiwa hawataonja asali mpaka waingie ndoani walisepa.

Miaka ikaenda,umri wa dada ukazidi kusogea ila bibie hakubadili msimamo wake.Aliendelea kuitunza bikra yake na kuishi maisha ya heshima kama
ambvyo binti yeyote mwenye maadili anapaswa kuishi.

Walokole tuna kamsemo ketu kuwa wakati wa Mungu ndio wakati sahihi na kweli "wakati wa Mungu ulipofika" bibie akaposwa na kijana aishie huko Marekani.

Kilichomvutia kijana kwa bibie ni habari alizozisikia kuwa bibie hajawahi kuguswa na mwanaume yeyote.

Kijana akatuma washenga,akatoa mahari na kufanya taratibu zote ikabakia ndoa tu ambayo ingefungwa baada ya yeye kwenda marekani na kurudi tena Tanzania.

Basi ikawa rasmi kuwa bibie sasa ni mke mrarajiwa wa mtu aishie Marekani.Viongozi wa kanisa na wazazi wakawa wanamtumia bibie kama mfano wa kuwaasa watoto wa kike kuwa ukijitunza Mungu atakuletea mume bora.Mabinti wakaambiwa si mnaona mwenzenu kajitunza sasa anaolewa na kwenda kuishi Marekani?

Basi bwana siku za mume mtarajiwa kurudi marekani zikakaribia na akaomba aende Dar na mkewe mtarajiwa akamfanyie shopping pamoja na kumuachia mradi wa ujenzi wa jumba lao lililoko Dar ausimamie.

Kwa vile kijana alishafanya taratibu zote wazee wakaona haina shida wakamruhusu binti asafiri na mumewe mtarajiwa kutoka mkoani kwao mpaka Dar.

Kufika Dar wakashukia hotel na huko kijana baada ya kushindwa kumshawishi binti atoe uroda kabla ya ndoa akatumia njia ya kumlewesha na ndipo akafanikiwa kuitoa bikra ya binti kabla ya ndoa.

Dada alilia sana alipozinduka na kujua kikichotokea ila kijana wa marekani akafanikiwa kumtuliza dada kwa maneno matamu matamu na ahadi ya kumpenda mpaka kifo kiwatenganishe.

Dada akafanyiwa shopping kisha jamaa akakwea pipa akarudi state na bibie akarudi mkoani kwao.

Baada ya week kadhaa dada akagundua ana ujauzito wa mumewe mtarajiwa.Wazee wakajua na kijana wa marekani akajulishwa na kuombwa kufanya hima aje aoe mkewe na kuondoka nae kabla wambea hawajajua kuwa ile bikra iliyotunzwa kwa miaka mingi ishatolewa kabla ya ndoa.

Kijana wa marekani akazipokea habari kwa furaha na kuwaahidi wazee kuja ASAP lkn mpaka muda wa mtoto kuzaliwa ukafika ila kijana wa kimarekani hakutokea.

Baada ya miaka kadhaa ikaja kugundulika kuwa kijana wa kimarekani alikua ni muhuni tu aliyekua na fantansy ya kuchakata bikra na eti hata wakati anatoa ile mahari eti alikua tayari keshaoa zake huko marekani na eti wale washenga aliowatuma walikua ni wahuni wenzie tu wazee wa hovyo maana wazazi wake wa kweli walipofuatwa walishangaa maana wao wanajua kijana wao alishaoa siku nyingi tu.

Ikawa asubuhi ikawa jioni dada mrembo aliyeishi kwa maadili akajikuta akichukua kadi yake kwenye chama kubwa la single mazas nchini.

Chama ambacho wanaume wa kitanzania huwaona wanachama wote wa chama hicho ni wanawake wasiofaa sio kuoa tu bali hata kwa mahusiano ya kudumu bali kwa kuwagonga na kukimbia haraka uwezavyo kuokoa maisha yako.

Kabla sikajiunga JF nilikua nawaona single maza ni wanawake kama wanawake wengine.Wako wanaojitambua wako empty sets.Wako wanaojiheshimu wako micharuko.Wako wapole na wanyenyekevu wako vichomi pia.Inshort tabia zote za wanawake single mazas utazipata hata kwa wanawake wasio single mazas.

U single maza sio laana ambayo automatically inamfanya mwanamke awe na tabia za hovyo kama hakua hivyo mwanzo na wala kutokua single maza sio baraka/neema/kinga ya kumfanya mwanamke awe wa maadili/bora.

Mwanamke yeyote single maza or not tabia zake zinatokana na malezi au mtazamo wake katika maisha.

Mimi sio single maza ila as long as mim ni mwanamke kama ilivyokua kwa bibie mtunza bikra hata mim iko siku naweza kuangukia kwa bazaz nikalielewa tukadanganyana danganyana pale at ze end ov ze dei bila kujua imekua kuaje nikajikuta na mim nachukua kadi kwenye chama kubwa la singo mazeriz.

Ikitokea nimekua single maza sitapenda kuongelewa kwa namna single maza wanaongelewa hapa JF.

Hapa JF single maza wanaongelewa kama jamii ya watu wenye laana wanaopaswa kutengwa kama walivyotengwa wale wakoma wa kwenye biblia.

Hapa JF wanaume mnawaongelea singo maza kama viumbe wasio na akili wala maadili lakini naomba niwaambie hawa single maza ni nyie mmewatengeneza na tena ni kundi la wanawake wenye akili kubwa na ndio maana wanaweza kulea na kusomesha watoto wao ambao baadhi yenu mmewakataa na kuona ni bora hela yako ununulie msambwanda wa barmaid kuliko kununua daftari za mwanao.

Sio ajabu yule kijana wa marekani nae yuko hapa JF akiandika nyuzi za kuwaongelea single maza kama walaaniwa kumbe yeye ndio mlaaniwa.

Naombeni wanaume wa JF mtoe hiyo lebel mliyowapachika singo maza sio sawa duniani wala mbinguni sababu hamjui mwanamke amepitia mitihani gani mpaka kuishia kuwa singo maza.

Naomba viongozi wa Jamii forums muliangalie hili.Kuna singo maza anaweza kujiua akifikiria aliyopitia na kulinganisha namma jamii inavyomhukumu.

Sio sawa jamii kusema watu wote wa kundi fulani wana tabia fulani kwani hiyo sio kweli na sio sawa.

Iweje mwanamke aliyeishi maisha yake yote kwa kujitunza na kujiheshimu halafu badae jamii imuone takataka kisa tu analea mtoto/watoto wake bila baba?
Hivi kinyume cha SINGLE MOTHER ni nini ? Au DOUBLE MOTHER?
 
Huwa sipendagi kuchangia mada za single mothers, maana zinahusu hisia sana.

Sio kwamba sinaga vya kuongelea, la hasha, nachagua tu kuwa msomaji.

Ninachoweza sema, wanaoponda single mothers huwa wanasababu zao, na pia single mothers wanaoponda wanaume, nao wanasababu zao. Na sometime pande zote mbili huwa na sababu zenye mashiko.

Ninachoweza kukwambia Clepatina huwezi kuyaelewa maumivu halisi ya single mothers kwa kusoma habari zao humu JF jinsi wanavyo nangwa. Na pia huwezi elewa maumivu ya upande wa pili kwa kuangalia maandiko jinsi wanavyo wananga single mothers
Thanks.
Kwa kuongelea kitu ambacho hupendi kuongelea.
I appreciate that alot.

Uko sawa kwa uliyoyaandika ila ubaya kabebeshwa zaidi mwanamke.
 
Back
Top Bottom