Kuna hizi nafasi za kazi Dubai wakuu. Je, ni za kweli?

NDUKI

JF-Expert Member
Jan 19, 2013
3,423
2,414
Heshima kwenu wakuu.

Nilikuta email kwenye Yahoo ikinijulisha kuwa wanahitajika wafanyakazi Dubai.

Je, ni kweli hizi kazi au ni Blah Blah tu. Kama ni za kweli basi wadau changamkieni fursa.

Screenshot_20200116-171326.png



Sharing is caring. Thanks.
 
Waliniambia kwani mimi ndie nilieanzisha uzi hapa au wewe? Mimi nakusanua maana mimi mjanja sasa wewe leta ujuaji.

Kwa sababu umesema kuna harufu ya kupigwa ndio mana nikakuuliza kwani uliambiwa utume hela...?

Sijauliza kama wewe ni mjanja au mjinga mmoja hizo kauli sijui zimetokea wapi...!
 
Kwa sababu umesema kuna harufu ya kupigwa ndio mana nikakuuliza kwani uliambiwa utume hela...?

Sijauliza kama wewe ni mjanja au mjinga mmoja hizo kauli sijui zimetokea wapi...!
Mkuu kuna utapeli mwingi sana online huku. Juzi hapa kuna mwamba amepost uzi kuwa jamaa yake kapigwa milioni mbili na mtu aliejifanya ni mwanamke yupo South anataka atumiwe nauli waje wale maisha na mshkaji bongo. Jamaa akaingia choo cha kike.

Haya mambo yapo sana. Unaweza kuibiwa kwa tamaa au kukosa umakini. Jiulize kwanza huyo mtu amepata wapi email yako mpaka akutumie tangazo la kazi privately?
 
Mkuu kuna utapeli mwingi sana online huku. Juzi hapa kuna mwamba amepost uzi kuwa jamaa yake kapigwa milioni mbili na mtu aliejifanya ni mwanamke yupo South anataka atumiwe nauli waje wale maisha na mshkaji bongo. Jamaa akaingia choo cha kike.

Haya mambo yapo sana. Unaweza kuibiwa kwa tamaa au kukosa umakini. Jiulize kwanza huyo mtu amepata wapi email yako mpaka akutumie tangazo la kazi privately?

Ndio mana swali langu la mwanzo niliuliza kuwa hawa jamaa walikuomba uwatumie hela...? Kumbe ni mtu aliambiwa na mwanamke atume 2mil nae kwa ujinga wake akatuma, sasa huo si ndio ujinga tunaposema kila siku.

Mtu anakwambiaje umtumie hela halaf ukatuma, huo utakuwa ni ujinga na upopoma wa kiwango cha lami...!
 
Bora umemuokoa wanapigwagwa hawa kjna mwanangu alitumiwa SMS kadhinda 1billion akaambiwa atume dola200 ili apewe pesa zake. Akanifuata nimsaidie jinsi ya kutuma hapo ndio ikawa ponapona yake

Ameniokoa kwani kuna sehemu nimesema nilitaka kutuma pesa, kwa hiyo mwanao akiwa mjinga unaona kila mtu yuko hivyo aisee. Ujinga wa mwanao ni wa mwanao ndugu.
 
Bora umemuokoa wanapigwagwa hawa kjna mwanangu alitumiwa SMS kadhinda 1billion akaambiwa atume dola200 ili apewe pesa zake. Akanifuata nimsaidie jinsi ya kutuma hapo ndio ikawa ponapona yake
Juzi hapa mwenyewe wamenitumia email wakajidai ni LinkedIn wanasema wamenitunuku grant ya USD 500, 000/- wakanitumia na online form nijaze details zangu ili nianze process zakuvuta kibunda nilichotunukiwa. Dah nilicheka mbaya sana 😂😂
 
Wewe unaonekana chukua juu boya ungepigwa mshukuru chaliifrancisco

Watanzania aisee tumepewa utashi ili tuwe tofauti na wanyama, ndege na wadudu kama vile funza, mende n.k

Link ipo hapo kwenye tangazo, sidhani kama ukiingia tu kwenye tangazo utakuwa umeshatapeliwa, inatakiwa ufate process upload CV yako, angalia next step wanataka ufanye nini, itakapofika sehemu ya kuambiwa utume fee yoyote kwani mtu ataingia kwenye wallet yako kuchomoa pesa atume huko, ikifika hapo si unasitisha zoezi.

Lakini mtu hujafanya process yoyote unaanza kupayuka Oooh mwanangu aliambiwa atume hela, mara Oooh nimemuokoa, acha kufikiri kwa kutumia masabuli shughulisha ubongo wako angalau kidogo aisee.

Usipende KUKARIRI na kuwakatisha wengine tamaa kama wee unaona haikufai usikatishe wengine tamaa wenye mioyo ya uthubutu aisee.
 
Hizo kampuni walizoandika unge Google na kuwasiliana nao kama kweli wanatoa ajira


Sent from my iPhone using Tapatalk

Well, sikuwa mmoja mwenye kutarajia kuomba that's why nikasema nishee na wadau sasa mwenye kuhitaji fursa nafkiri itampasa afanye hivyo kiongozi.
 
Well, sikuwa mmoja mwenye kutarajia kuomba that's why nikasema nishee na wadau sasa mwenye kuhitaji fursa nafkiri itampasa afanye hivyo kiongozi.

Nimekuelewa vizuri Mkuu
Nimeona hiyo link ya RicruitArab
Lakini kweli atakaetaka kazi anaweza kujiridhisha kwanza maana matapeli wengi wa Kinigeria


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Nimekuelewa vizuri Mkuu
Nimeona hiyo link ya RicruitArab
Lakini kweli atakaetaka kazi anaweza kujiridhisha kwanza maana matapeli wengi wa Kinigeria


Sent from my iPhone using Tapatalk

Kabisa kiongozi kama unavyosema mtu inabidi ajiridhishe kwanza kama ataona kuna harufu ya utapeli atasitisha maombi as simple as that.

Thanks a lot bro.
 
Back
Top Bottom