Kuna hatari ya ukabila inaienyemelea nchi, Rais Samia inabidi aongoze kwa mkono wa chuma kuepeusha hili

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,806
18,784
Mimi ni muumini mkubwa wa demokrasia na utawala wa sheria, na ndiyo ni moja ya sababu iliyonifanya kuvutiwa na uongozi wa Samia kuliko uliopita

Lakini kuna kipindi demokrasia hutumiwa vibaya na kuigawa nchi kwa udini au ukabila, hapo ndipo nasema demokrasia inabidi iwekwe pembeni

Kumekuwa na dalili za ukabila zinaanza kuchipua nchini, kuna kundi flani linaanza kujinasibu kuwa wao ndio wengi nchini na ndio wanaamua rais awe nani, sijui hili lina ukweli kiasi gani, ila haya ni matumizi mabaya ya demokrasia

Kundi hili linalotaka kutumia vibaya demokrasia ndio hawa hawa waliokuwa wakipiga kelele kuwa demokrasia haina umuhimu Afrika mtu wao alipokuwa akikanyaga katiba na kuua demokrasia, sasa ghafla demokrasia imekua ya muhimu mtu wao anapokuwa hayupo

Mwalimu Nyerere alipochukua nchi kutoka kwa Wakoloni, aliona hatari ya nchi kutumbukia kwenye siasa za kikabila na ikabidi aongoze kama alivyoongoza na tukaipata Tanzania hii

Nchi kama Misri ilikuwa hatarini kumezwa na siasa kali za kidini, kutokana na makundi yaliyokuwa yakitumia vibaya demokrasia, ila kutokana na kuendeshwa kibabe nchi imetulia na ni moja kati ya nchi zilizoendelea sana Africa,

Demokrasia ikitumiwa vibaya ni vurugu
 
Ungekuwa na akili ungeshauri katiba mpya ipatikane haraka ili kuondoa hilo tatizo kama kweli lipo badala ya kushauri na kuhamasisha Udikteta.

Udikteta haujawahi kuwa suluhu ya kudumu ya matatizo ya kisiasa popote duniani, badala yake huongeza maafa, huondoa uhuru na ustaarabu kati ya binadamu.
 
Kuna basi tumepanda lakini Kama halina dereva
Kuna abiria mzee kasema huenda linaendeshwa kwa remote

Abiria wengi hawaelewi Kila mtu anaongea lake
Maombi yanahitajika saana maana safari huenda ikawa ngumu

Hapa katikati Kuna mjeda kafunguka kwamba tunaendeshwa na kondakta kwahiyo tusilaumu

Dua zenu wadau
 
Mkono wa chuma ndiyo umemuondoa Magufuli mwambie ajaribu aone Cha mtema kuni. Kama Karume alijaribu huko Zanzibar akalamba udongo, Nyerere akaponea chupuchupu akaona isiwe kesi akala Kona na kuomba sub Magufuli akataka utemi karma ikafanya yake.
 
Ungekuwa na akili ungeshauri katiba mpya ipatikane haraka ili kuondoa hilo tatizo kama kweli lipo badala ya kushauri na kuhamasisha Udikteta.

Udikteta haujawahi kuwa suluhu ya kudumu ya matatizo ya kisiasa popote duniani, badala yake huongeza maafa, huondoa uhuru na ustaarabu kati ya binadamu.
kabisa anayewambia atatue tatizo yeye mwenyewe teuzi zake zipo kidini na kijinsia
 
Ungekuwa na akili ungeshauri katiba mpya ipatikane haraka ili kuondoa hilo tatizo kama kweli lipo badala ya kushauri na kuhamasisha Udikteta.

Udikteta haujawahi kuwa suluhu ya kudumu ya matatizo ya kisiasa popote duniani, badala yake huongeza maafa, huondoa uhuru na ustaarabu kati ya binadamu.
Nyerere aliongoza kwa udikteta na aliondoa ukabila
Kuna nchi ya Misri pia nimeitolea mfano, hata Rwanda pia

Demokrasia kwa watu wasiokuwa na elimu ni vurugu tupu
 
Kama Nyerere aliondoa ukabila huu wewe unaozungumzia umetoka wapi na umeletwa na nani?

Misri ni taifa la kidekteta tangu kuanzishwa kwake, limekuwa likitawaliwa na madikteta kwa miaka yote mpaka Mohamed Morsi aliposhinda urais katika uchaguzi huru mwaka 2012 kabla hajapinduliwa na jeshi mwaka 2013 na kufia gerezani mwaka 2019.
Nyerere aliongoza kwa udikteta na aliondoa ukabila
Kuna nchi ya Misri pia nimeitolea mfano,
Demokrasia kwa watu wasiokuwa na elimu ni vurugu tupu
 
kundi hili linalotaka kutumia vibaya demokrasia ndio hawa hawa waliokuwa wakipiga kelele kuwa demokrasia haina umuhimu Afrika mtu wao alipokuwa akikanyaga katiba na kuua demokrasia, sasa ghafla demokrasia imekua ya muhimu mtu wao anapokuwa hayupo
Hawa watu ni hatari sana. Tuombe sana asije akatokea rais toka huko tena
 
Wewe unachanganya mifarakano na makundi ya kichama na kuifanya ya kitaifa. Tanzania ni kubwa kuliko chama kimoja na haiwezi kutikiswa na tofauti na migongano ndani ya chama kimoja.
Alikuwa dikteta mshamba yule, Samia akitumia vizuri mamlaka yake tutakuwa na taifa la amani na maendeleo
 
Back
Top Bottom