Kuna haja ya kuwa na CWT kwa walimu kwa namna inavyofanya kazi?

DOFFA

JF-Expert Member
Jul 31, 2016
425
233
Chama walimu inakata asilimia fulani kwenye mishahara ya walimu kwa
MADHUMUNI ya:
(a) Kuendeleza na kulinda hadhi ya kazi ya Ualimu pamoja na kusimamia viwango vya juu vya maadili, ufahamu, maarifa na ujuzi.
(b) Kusimamia, kuendeleza na kulinda maslahi ya Walimu na Watendaji, katika Taasisi za Elimu na kuhakikisha kuwa kuna vivutio vya kutosha na mazingira mazuri ya kuwafanya waipende na kuizingatia kazi yao.
(c) Kuhimiza elimu na ujuzi wa Watendaji wanaohudumia Shule, Vyuo na sehemu zote zinazoshughulikia elimu.
(d) Kuwa kitovu cha maandiko ya kuwaendeleza Walimu, Wanachama na Wananchi katika elimu na mafunzo ya kazi ya Ualimu.
(e) Kuwahimiza Walimu kufanya kazi yao vizuri na kuwasisitiza waoneshe mfano bora wa kazi, uadilifu, tabia na mwenendo.
(f) Kuwakutanisha Walimu mara kwa mara ili waweze kujadili maendeleo na matatizo katika taaluma zao na kutafuta mbinu za kuyatatua, kufahamiana na kubadilishana mawazo ili kujenga utamaduni wa kujiendeleza.
(g) Kuhimiza na kuhakikisha kuwa Walimu na Watendaji wanapata huduma zote wanazostahili kiuchumi, kiafya na kijamii.
(h) Kujadili na kushauriana na Waajiri juu ya haki, maslahi na hali nyingine zinazohusiana na mazingira ya ajira ya Ualimu.
(i) Kuishauri serikali juu ya mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo ya elimu nchini.
(j) Kuhakikisha kuwa waajiri wanaohusika wanatambua uwepo wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na kuwaelimisha Walimu kuwa wana uhuru wa kujiunga na Chama hicho na uhuru wa kufanya mgomo pale inapobidi.
7
(k) Kusuluhisha migogoro na kutatua malalamiko mahali pa kazi kati ya Waajiri na Walimu au miongoni mwa Walimu wenyewe.
(l) Kutunga na kusimamia Sera itakayolinda hadhi ya Walimu wanawake kwa kutambua hali na maumbile yao na kuhakikisha kuwa afya zao zinalindwa bila ubaguzi wa ajira, likizo ya uzazi na huduma nyingine anazostahili Mwalimu yeyote.
(m) Kutunga na kusimamia Sera itakayolinda hadhi ya Walimu wenye ulemavu kwa kutambua hali, maumbile na mazingira yao ya kazi .
(n) Kuhakikisha kuwa katika sehemu zote za kazi Walimu hawapati bughudha ya kijinsi na kuweka utaratibu utakaodhibiti wale watakaokiuka.
(o) Kuhakikisha kuwa waajiri na Walimu wanazingatia na kutekeleza sheria na kanuni za nchi zinazohusu kazi, pamoja na mikataba iliyopo kati ya waajiri hao na Walimu au Chama cha Walimu ili mradi sheria hizo zinazingatia HAKI.
(p) Kuwaelimisha wanachama juu ya masuala yote yanayohusiana na ajira zao ikiwa ni pamoja na kuwapa ushauri wa kisheria unapohitajika.
(q) Kuhakikisha kwamba hakuna ubaguzi wa rangi, kabila, dini,
jinsi, ulemavu au hali miongoni mwa wanachama.
(r) Kuwa na uhuru wa kushirikiana na kushauriana na vyama vingine vya wafanyakazi nchini na nje ya nchi.
(s) Kuwekeza katika vitega uchumi vitakavyoboresha ustawi wa wanachama ingawa si Chama cha Kibiashara.
(t) Kutengeneza na kutetea Sera itakayolinda hadhi ya Walimu wenye ulemavu na kuhakikisha kuwa afya zao na vikwazo vinavyoathiri utendaji wao vinaondolewa na kupata huduma nyingine wanazostahili Walimu wenye ulemavu.
 
Malizia sasa mbona umeishia njiani,nilitarajia ungefafanua pia kuhusu pesa unayokatwa kwenye mshahara,pia kiwango cha utetezi katika swala zima la masilahi ya walimu
 
Malizia sasa mbona umeishia njiani,nilitarajia ungefafanua pia kuhusu pesa unayokatwa kwenye mshahara,pia kiwango cha utetezi katika swala zima la masilahi ya walimu
Makato:
B1=Basic 419000
Cwt=8390.


C1=530000
Cwt 10600.
D1=716000
Cwt 14320.
E1=940000
Cwt 18800.

F1=1235000
Cwt 24700.
 
Kuna CHAMA KINAITWA CHAKAMWATA (CHAMA CHA KUTETEA HAKI NA MASILAHI YA WALIMU TANZANIA) NI CHAMA KIPYA , NI SULUHISHO KWA KERO ZA WALIMU, MAKATO NI 1% YA MSHAHARA ,NA 0.5% YA MAKATO YA MWALIMU ANARUDISHIWA PINDI ANASTAAFU AU KUACHA KAZI. HAPA CHINI NIMEWEKA BAADHI YA TAARIFA KUHUSU CHAMA KIPYA LAKINI BARUA YA USAJILI NITAIWEKA SOON IKIKUBALI.
 

Attachments

  • chakamwata contribution code.pdf
    254.3 KB · Views: 60
  • HISTORIA YA CHAMA CHA KUTETEA HAKI NA MASILAHI YA WALIMU TANZANIA.pdf
    385.3 KB · Views: 280
Kuna CHAMA KINAITWA CHAKAMWATA (CHAMA CHA KUTETEA HAKI NA MASILAHI YA WALIMU TANZANIA) NI CHAMA KIPYA , NI SULUHISHO KWA KERO ZA WALIMU, MAKATO NI 1% YA MSHAHARA ,NA 0.5% YA MAKATO YA MWALIMU ANARUDISHIWA PINDI ANASTAAFU AU KUACHA KAZI.
chama kizuri ktk mapato na marejesho tofauti na hicho CWT. hivi ni lazima mtu kua ktk CWT? na kama sikitaki hiki CWT, nitatumia jia gani kujitoa ili lijiunge na chama kingine?
 
Chama walimu inakata asilimia fulani kwenye mishahara ya walimu kwa
MADHUMUNI ya:
(a) Kuendeleza na kulinda hadhi ya kazi ya Ualimu pamoja na kusimamia viwango vya juu vya maadili, ufahamu, maarifa na ujuzi.
(b) Kusimamia, kuendeleza na kulinda maslahi ya Walimu na Watendaji, katika Taasisi za Elimu na kuhakikisha kuwa kuna vivutio vya kutosha na mazingira mazuri ya kuwafanya waipende na kuizingatia kazi yao.
(c) Kuhimiza elimu na ujuzi wa Watendaji wanaohudumia Shule, Vyuo na sehemu zote zinazoshughulikia elimu.
(d) Kuwa kitovu cha maandiko ya kuwaendeleza Walimu, Wanachama na Wananchi katika elimu na mafunzo ya kazi ya Ualimu.
(e) Kuwahimiza Walimu kufanya kazi yao vizuri na kuwasisitiza waoneshe mfano bora wa kazi, uadilifu, tabia na mwenendo.
(f) Kuwakutanisha Walimu mara kwa mara ili waweze kujadili maendeleo na matatizo katika taaluma zao na kutafuta mbinu za kuyatatua, kufahamiana na kubadilishana mawazo ili kujenga utamaduni wa kujiendeleza.
(g) Kuhimiza na kuhakikisha kuwa Walimu na Watendaji wanapata huduma zote wanazostahili kiuchumi, kiafya na kijamii.
(h) Kujadili na kushauriana na Waajiri juu ya haki, maslahi na hali nyingine zinazohusiana na mazingira ya ajira ya Ualimu.
(i) Kuishauri serikali juu ya mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo ya elimu nchini.
(j) Kuhakikisha kuwa waajiri wanaohusika wanatambua uwepo wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na kuwaelimisha Walimu kuwa wana uhuru wa kujiunga na Chama hicho na uhuru wa kufanya mgomo pale inapobidi.
7
(k) Kusuluhisha migogoro na kutatua malalamiko mahali pa kazi kati ya Waajiri na Walimu au miongoni mwa Walimu wenyewe.
(l) Kutunga na kusimamia Sera itakayolinda hadhi ya Walimu wanawake kwa kutambua hali na maumbile yao na kuhakikisha kuwa afya zao zinalindwa bila ubaguzi wa ajira, likizo ya uzazi na huduma nyingine anazostahili Mwalimu yeyote.
(m) Kutunga na kusimamia Sera itakayolinda hadhi ya Walimu wenye ulemavu kwa kutambua hali, maumbile na mazingira yao ya kazi .
(n) Kuhakikisha kuwa katika sehemu zote za kazi Walimu hawapati bughudha ya kijinsi na kuweka utaratibu utakaodhibiti wale watakaokiuka.
(o) Kuhakikisha kuwa waajiri na Walimu wanazingatia na kutekeleza sheria na kanuni za nchi zinazohusu kazi, pamoja na mikataba iliyopo kati ya waajiri hao na Walimu au Chama cha Walimu ili mradi sheria hizo zinazingatia HAKI.
(p) Kuwaelimisha wanachama juu ya masuala yote yanayohusiana na ajira zao ikiwa ni pamoja na kuwapa ushauri wa kisheria unapohitajika.
(q) Kuhakikisha kwamba hakuna ubaguzi wa rangi, kabila, dini,
jinsi, ulemavu au hali miongoni mwa wanachama.
(r) Kuwa na uhuru wa kushirikiana na kushauriana na vyama vingine vya wafanyakazi nchini na nje ya nchi.
(s) Kuwekeza katika vitega uchumi vitakavyoboresha ustawi wa wanachama ingawa si Chama cha Kibiashara.
(t) Kutengeneza na kutetea Sera itakayolinda hadhi ya Walimu wenye ulemavu na kuhakikisha kuwa afya zao na vikwazo vinavyoathiri utendaji wao vinaondolewa na kupata huduma nyingine wanazostahili Walimu wenye ulemavu.
hakuna haja, kwani kazi hizo zote walizoorodhesha, zilizo nyingi hawazifani; na hata zile chache wanazojaribu kuzifanya, nazo ni kwa kulipua.
 
CWT ni jipu.tena zaidi ya jipu.sijawahi kuona manufaa yake zaidi ya wao kujinenepesha kwa michango yetu.Ni wakati muafaka kujiunga na hiki chama kipya.viongozi wa chama kipya tembeleeni mashuleni walimu wapo tayari kujiunga na kuachana na hawa wanaovuna bure jasho letu.
 
Pesa zote hizo bora wangeanzisha ujenzi wa nyumba katika kila shule,ah!tanzania hii!
 
Kama kuna kitu nakichukia hapa duniani basi ni cwt,yaani mambo yetu toka tumeahidiwa mpaka leo kimyaa hao viongozi ndo wameingia mitini kazi kula hela tu.
 
Kuna CHAMA KINAITWA CHAKAMWATA (CHAMA CHA KUTETEA HAKI NA MASILAHI YA WALIMU TANZANIA) NI CHAMA KIPYA , NI SULUHISHO KWA KERO ZA WALIMU, MAKATO NI 1% YA MSHAHARA ,NA 0.5% YA MAKATO YA MWALIMU ANARUDISHIWA PINDI ANASTAAFU AU KUACHA KAZI. HAPA CHINI NIMEWEKA BAADHI YA TAARIFA KUHUSU CHAMA KIPYA LAKINI BARUA YA USAJILI NITAIWEKA SOON IKIKUBALI.
hata hao watakua km Cwt wakishafanikiwa malengo yao!
 
chama kizuri ktk mapato na marejesho tofauti na hicho CWT. hivi ni lazima mtu kua ktk CWT? na kama sikitaki hiki CWT, nitatumia jia gani kujitoa ili lijiunge na chama kingine?
Kwa mujibu wa sheria za utumishi wa Umma, kila mwajiliwa anahaki ya kujaza TUF 6 na kuchagua chama apendacho ( dirisha la wakala), lakini kwa maelezo zaidi niambie uko mkoa/ hamashauri gani ili nikuunganishe na viongozi wa Chama watakufikia na kukupa maelezo zaidi.
 
Mimi nataka kujua kama inawezekana Mwalimu kutojiunga na chama chochote?Mi hata sioni manufaa ya kukatwa hizo kwa upande wangu
 
Mimi nataka kujua kama inawezekana Mwalimu kutojiunga na chama chochote?Mi hata sioni manufaa ya kukatwa hizo kwa upande wangu
ndiyo uwezekano upo, lakini mwishowe utaingizwa kwenye chama usichokipenda sababu, mfano, CWT wao wanaamini kuwa kauli yao yoyote kwa serikali inamanufaa kwa walimu wote, hivyo wanahaki ya kukukata hata bila kujiunga.Tumia haki yako ya kuchagua kuliko kuchaguliwa na Mwajili wako. Karibu CHAKAMWATA
 
ndiyo uwezekano upo, lakini mwishowe utaingizwa kwenye chama usichokipenda sababu, mfano, CWT wao wanaamini kuwa kauli yao yoyote kwa serikali inamanufaa kwa walimu wote, hivyo wanahaki ya kukukata hata bila kujiunga.Tumia haki yako ya kuchagua kuliko kuchaguliwa na Mwajili wako. Karibu CHAKAMWATA
Huu sasa ujinga ila kuliko nikatwe na hilo li CWT bora nikatwe na chama kingine.
 
Back
Top Bottom