Kuna haja ya kuulizana tena kwanini fedha nyingi huingia kwenye matumizi kuliko Miradi ya Maendeleo

Bashir Yakub

Member
May 27, 2013
84
1,561
ANASA ZIMERUDI?

Bashir Yakub.

Ukumbi wa Mlimani City ukitengwa kwa watu 900 gharama ni Tshs 36,000,000/= bila chakula na vinywaji.

Gharama ya dawati moja zuri ni Tshs 80,000/=. Kwa Tshs. 36,000,000/= tunapata dawati 450,000.

Kwa dawati linalokaliwa na wanafunzi wawili jumla ya wanafunzi 225,000 wanakuwa wamepata sehemu nzuri ya kukaa na kupata maarifa.

Unaweza kutafuta mfano mwingine kwa fedha hiyo M.36.

Ikulu ya Magogoni upo ukumbi mkubwa hauna kazi leo. Kadhalika Ikulu ya Chamwino, Dodoma ambako nako wapo wazee, upo ukumbi mkubwa, mpya, na mzuri.

Kabla sijasahau ukumbi wa Serikali wa Mwalim Nyerere Mtaa wa Shaban Robert uliojengwa kwa USD 15 Milioni wenye uwezo wa kukalisha watu zaidi ya 1000, ndani ya ekari 6.2.

Achana na Karimjee na kumbi nyingine nyingi zilizo kila pahala kwenye Maghorofa ya Wizara zilizohamia Dodoma.

Bajeti yetu ya 2020/2021 Trilioni 12.8 ambayo ni asilimia 37 tu ya bajeti yote ndo ilienda kwenye miradi ya maendeleo. Asilimia 63 ya fedha iliyobaki ni MATUMIZI.

Kuna haja ya kuulizana tena kwanini fedha nyingi huingia kwenye matumizi kuliko miradi ya maendeleo.

Kupanga ni kuchagua.
 
Kama unakunywa chai, lunch na chakula cha usiku kwa jumla ya Tsh 10,000 kwa siku, then usipokula mwaka mzima tayari una:

Tsh 10,000*365= Tsh 3,650,000

Kwahiyo ukiacha kula miaka mitano una jenga Mansion🤣

Jamani acheni sekta binafsi ipumue.

Yaani Harmonize, Diamond, Lady Jaydee wakodi Mlimani City halafu serikali ionekane inaharibu pesa.

Unaweza kujifanya bahiri, unabana pesa, halafu walalahoi wanaendelea kuumia, sekta binafsi zinakufa na kupunguza kazi watu wakati pesa wanakula kina Kigwangalla.
 
Ndio zimerudi

Acheni mzunguko wa hela uingie mtaani jamani. Kwani mnapata raha gani watu wakiwa na maisha magumu nyinyi binadamu aisee. Acheni serekali ipeleke hela mitaani
Kweli mkuu zamani fedha enzi za jiwe zilikuwa zinaenda kwa watu wachache wanaofanya biashara ya utumwa na kwenye kampuni zake, mwache mama aongeze mzunguko wa pesa, watu 900 wakipata bahasha ya elfu 50 sio mbaya,wauza chakula nao watapata fedha.

Mikumi tena.
 
Hujui uchumi nyamaza! Huo ndo unaitwa mzunguko wa fedha! Hapo wamiliki wa Diamond Jubilee watalipa wafanyakazi wao posho/mishahara, na hao wafanyakazi watalipa kodi za nyumba zao, maji, umeme, watanunua nguo, kabati, jokofu na mambo mbalimbali.

Unataka nchi ijiendeshe kibahili? Unaona hiyo ndo sifa ya uongozi? Hujui kama hao diamond Jubilee wanalipa kodi na ushuru mbalimbali za serikali?

Hizo fedha zilizokuwa zinatumika kununua wapinzani zilikuwa sio anasa na ubadhirifu?
 
ANASA ZIMERUDI?

Bashir Yakub.

Ukumbi wa Mlimani City ukitengwa kwa watu 900 gharama ni Tshs 36,000,000/= bila chakula na vinywaji.

Gharama ya dawati moja zuri ni Tshs 80,000/=. Kwa Tshs 36,000,000/= tunapata dawati 450,000.

Kwa dawati linalokaliwa na wanafunzi wawili jumla ya wanafunzi 225,000 wanakuwa wamepata sehemu nzuri ya kukaa na kupata maarifa.

Unaweza kutafuta mfano mwingine kwa fedha hiyo M.36.

Ikulu ya Magogoni upo ukumbi mkubwa hauna kazi leo. Kadhalika Ikulu ya Chamwino, Dodoma ambako nako wapo wazee, upo ukumbi mkubwa,mpya, na mzuri.

Kabla sijasahau ukumbi wa Serikali wa Mwalim Nyerere Mtaa wa Shaban Robert uliojengwa kwa USD 15 Milioni wenye uwezo wa kukalisha watu zaidi ya 1000, ndani ya ekari 6.2.

Achana na Karimjee na kumbi nyingine nyingi zilizo kila pahala kwenye Maghorofa ya Wizara zilizohamia Dodoma.

Bajeti yetu ya 2020/2021 Trilioni 12.8 ambayo ni asilimia 37 tu ya bajeti yote ndo ilienda kwenye miradi ya maendeleo. Asilimia 63 ya fedha iliyobaki ni MATUMIZI.

Kuna haja ya kuulizana tena kwanini fedha nyingi huingia kwenye matumizi kuliko miradi ya maendeleo.

Kupanga ni kuchagua.
Mkuu usiwe kama vilaza wa CCM ni 450 tu
 
Hujui uchumi nyamaza! Huo ndo unaitwa mzunguko wa fedha! Hapo wamiliki wa Diamond Jubilee watalipa wafanyakazi wao posho/mishahara, na hao wafanyakazi watalipa kodi za nyumba zao, maji, umeme, watanunua nguo, kabati, jokofu na mambo mbalimbali.

Unataka nchi ijiendeshe kibahili? Unaona hiyo ndo sifa ya uongozi? Hujui kama hao diamond Jubilee wanalipa kodi na ushuru mbalimbali za serikali?

Hizo fedha zilizokuwa zinatumika kununua wapinzani zilikuwa sio anasa na ubadhirifu?
Bila mzunguko wa fedha watu wanakufa njaa.
 
Hujui uchumi nyamaza! Huo ndo unaitwa mzunguko wa fedha! Hapo wamiliki wa Diamond Jubilee watalipa wafanyakazi wao posho/mishahara, na hao wafanyakazi watalipa kodi za nyumba zao, maji, umeme, watanunua nguo, kabati, jokofu na mambo mbalimbali.

Unataka nchi ijiendeshe kibahili? Unaona hiyo ndo sifa ya uongozi? Hujui kama hao diamond Jubilee wanalipa kodi na ushuru mbalimbali za serikali?

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
Yafaa wenye uelewa wa enzi ya mwaka 47, waeleweshwe taratibu kwani wakiharakishwa kuelewa wanaonewa bure. Juhudi ya utoaji elimu iimarishwe kwa kuanza na wanajukwaa waliopo humu.
 
Tatizo watanzania asilimia 88.5% ni wapigaji.
Hapo yapo makundi yote
Wanasiasa wa pande zote
Watumishi kada zote
Viongozi wa kidini
Na raia wengine

Haya makundi yote ni wapigaji hata wale wanaolilia maendeleo na kila aina ya ukosoaji na usifiaji wote wapigaji au wana milengo ya upigaji.

Sio Tanzania pekee huu ni ugonjwa sugu barani Afrika kwa ujumla,

Ni vigumu sana kupiga hatua kama kila mtu atakua na ubinafsi uliopitiliza wakuona tumbo lake na familia yake ndio wanapaswa kunufaika na wizi/upigaji wake.
 
Kikao kufanyika Mlimani City... Hapana kwa Kweli, sikubaliani nao!

Kufanyika Ikulu... Hapana vile vile

Mwalimu Nyerere Conference... Kama wangetumia bure kwavile tu ni wa serikali basi huo ungekuwa ni uzuzu; na kama na wenyewe wangelipia, I bet unaweza kuwa expensive kuliko Mlimani City; na kwahiyo hapana!!

Diamond Jubilee ingawaje napo wanaweza kulipia, hapo pangekuwa ni cheap zaidi!
 
Kikao kufanyika Mlimani City... Hapana kwa Kweli, sikubaliana nao!

Kufanyika Ikulu... Hapana vile vile

Mwalimu Nyerere Conference... Kama wangetumia bure kwavile tu ni wa serikali basi huo ungekuwa ni uzuzu; na kama na wenyewe wanalipia, I bet unaweza kuwa expensive kuliko Mlimani Citi; na kwahiyo hapana!!

Diamond Jubilee ingawaje napo wanaweza kulipia, hapo pangekuwa ni cheap zaidi!
Ushauri wako tafadhali.
 
Back
Top Bottom