Kuna haja ya kupitia asilimia za mapato TFF inavinyonya vilabu

mpimamstaafu

JF-Expert Member
Jul 18, 2018
4,445
4,704
Wadau wa soka naamini mmeona mgawanyo wa mapato katika Mechi ya Simba na Yanga. Binafsi naiona TFF inavinyonya Vilabu kwani kuna mapato yanaitwa

1.TFF
2.TPLB
3.GHARAMA ZA MECHI

Binafsi naona mapato ya TFF ndio yangegawanya kwa TPLB na Gharama za Mechi. Tukumbuke TFF imeshindwa kuvipatia vilabu Wadhamini kwa hiyo Vilabu vinajiendesha kwa kutumia hayo Mapato, hakika TFF inavinyonya Vilabu ndio maana Migogoro ya kufukuzana haiishi pale TFF.

Tunaiomba Serikali kama inadhamira ya dhati kuviinua vilabu basi TFF ipunguziwe asilimia ya Mapato. Na kama TFF inataka fedha ibuni vyanzo sio kutegemea Mapato pia TFF kuna Fedha inapata kutoka FIFA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta Uzi nakuunga mkono 100%, Hawa tff na wenzake wanavinyonya vilabu.
 
Watu wanakuza vitambi tu...anyway tukisema sana tutaambiwa tuna wivu wa kike.
 
Wataingiza tu. Afu huko nako kutakuwa na gharama za makomandoo

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
Mkuu, hizo za makomandoo ni za club kwa matakwa yao. Hata za kamati za ufundi humo humo. Ni za wajanja wachache.
 
Tatizo ninaloliona hapa ni kuweka mlolongo wa makato yasiyo na maana yoyote na yanachukua asilimia kubwa. Hata timu ikijenga uwanja Sidhani kama utakuwa mkubwa sana kama ule wa taifa. Mfano uwanja wa chamanzi hata bila makato Hauwezi kupata pesa nyingi kama ukicheza taifa na ukatwe. Uwanja wa azam complex unachukua watazamaji 7000 tu. Kwa simba na yanga ili wajikomboe labda wajenge uwanja wenye kuingiza mashabiki wasiopungua elfu 40.
 
Tatizo ninaloliona hapa ni kuweka mlolongo wa makato yasiyo na maana yoyote na yanachukua asilimia kubwa. Hata timu ikijenga uwanja Sidhani kama utakuwa mkubwa sana kama ule wa taifa. Mfano uwanja wa chamanzi hata bila makato Hauwezi kupata pesa nyingi kama ukicheza taifa na ukatwe. Uwanja wa azam complex unachukua watazamaji 7000 tu. Kwa simba na yanga ili wajikomboe labda wajenge uwanja wenye kuingiza mashabiki wasiopungua elfu 40.
Hata viwanja vya kuanzia watu 20,000 is haba kwa timu zetu hizi . Ukiondoa makato ya dhulma, wanaweza kupata hela za maana. Lakini upuuzi wa TFF, bodi ya ligi, DRFA viondoke. Hata ikibidi kwenda FIFA. Nahisi ni upuuzi wa Bongo tu
 
Azama alikuwa analazimishwa kucheza National Stadium mechi za nyumbani vs Simba na Yanga walishaacha?
 
Back
Top Bottom