Kuna haja ya kuboresha taaluma ya ualimu ili kukuza sekta ya elimu Tanzania

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
613
1,776
Ualimu na Mvuto kwa Vijana.jpg

Mwalimu ana jukumu muhimu katika kuunda haiba ya vijana na kuwatayarisha kuwa raia wazalendo na wanaowajibika. Kando na kazi za kufundisha darasani, mwalimu pia anatarajiwa kuchukua nafasi ya mshauri, kiongozi na mlezi kwa wanafunzi. Lakini pamoja na umuhimu huo, bado kuna mtazamo hasi dhidi walimu katika jamii.

Ualimu hauchukuliwi kama taaluma inayoheshimika. Kwa siku hizi ni nadra kuona kijana yeyote akitazama ualimu kama chaguo lake la kwanza la taaluma. Hii ni kwakuwa kuna changamoto mbalimbali zinazosababisha taaluma ya ualimu kutoheshimika na wengi nchini Tanzania.

Kwanza, ni kwa sababu ya mishahara midogo ukilinganisha na taaluma nyingine kama vile sheria na udaktari. Aidha, malalamiko ya walimu kuhusu mazingira duni ya kufundishia na kujifunzia, uhaba wa vitendea kazi na ukubwa wa madarasa hayawavutii wengi kuingia katika taaluma hiyo. Hata hivyo, vijana wanaojiunga na taaluma hii ni kwa sababu hawana njia mbadala.

Sababu nyingine ni kwamba vijana wanaona taaluma ya ualimu kama ni kwa ajili ya wale ambao hawakufanya vizuri katika mitihani ya kitaifa.

Hivyo, inaweza kuwa elimu ni sehemu muhimu ya ajenda ya maendeleo ya serikali ya Tanzania, lakini haijawavutia vijana kujiunga na taaluma ya ualimu kwa moyo mmoja kwasababu kila mara inaonekana hasi ikilinganishwa na taaluma nyingine.

Tufanye nini?

Tuboreshe vipato
Ili kuwavutia vijana kwenye taaluma ya ualimu, kuwe na mishahara inayoendana na maisha ya sasa. Serikali inapaswa pia kuunda sera bora za taaluma hii na kutoa motisha kwa kazi za ziada. Hii isiwe tu kwa shule za umma; shule za binafsi pia zina jukumu la kufanya kazi ya ualimu kuvutia. Baadhi ya shule za binafsi pia zinashutumiwa kutotoa mikataba kwa walimu hata baada ya miaka kadhaa. Hili linapaswa kurekebishwa ili kuongeza hamu ya vijana kufundisha.

Mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia
Baadhi ya majengo ya shule yana paa zinazovuja, madarasa yenye vumbi, madawati na meza mbovu au kutokuwepo kabisa na vifaa vya kufundishia. Njia rahisi ya kufanya taaluma ya ualimu ivutie vijana ni kujenga majengo mazuri, ofisi na madarasa kwa waelimishaji. Hii itasababisha kuwa na mazingira rafiki kwa wote – wanafunzi na walimu.

Mazingira ya mwanadamu yanaweza kuathiri sana uzalishaji. Ili kuwafanya walimu kuzingatia majukumu yao na wanafunzi kujifunza vizuri, lazima mazingira yawe ya kuvutia. Shule nyingi za binafsi zinaonekana kuzingatia sana kipengele hiki, ila serikali bado inahitaji nguvu kubwa kuboresha mazingira pamoja viwango vya ufundishaji katika shule za umma.

Teknolojia katika sekta ya elimu
Vijana wa karne ya 21 wanaweza kufanya kazi vizuri katika sehemu za kazi ambazo zinahimiza matumizi ya teknolojia na ubunifu. Mbinu za kizamani za ufundishaji sasa haziendani na wakati tuliomo. Matumizi ya teknolojia yanaweza kuwavutia vijana wengi kwani pia unawapatia fursa ya kukua na maendeleo ya kiteknolojia lakini pia kunaweza kuwasaidia kupunguza mzigo wa kazi. Shule nyingi za umma zina changamoto ya umeme, hivyo ni wakati sasa wa serikali kuona umuhimu wa kuzifanya shule zetu kuwa za kisasa na zinazotoa fursa ya vijana kupata elimu inayoendana na teknolojia ya sasa.

Huduma za msingi kwa walimu
Walimu wa shule za umma zilizopo katika maeneo ya vijijini wanakumbana na changamoto za kila aina: maji, umeme, usafiri na huduma nyingine za kijamii. Wengine kuna wakati wanatumia karibu nusu ya mshahara kama nauli ya kwenda ofisi za halmashauri au kufanya manunuzi ya msingi. Haya si mazingira ambayo vijana wengi wa leo wapo tayari kuyaishi. Ni vyema serikali iangalie utaratibu wa kuwawezesha walimu wanaoishi katika maeneo hayo kuishi vizuri kwa kuwapatia makazi, posho maalum, chakula na kuhakikisha wanapata huduma nyingine za msingi.

Ualimu ni kazi ya muhimu, na pengine ya lazima katika jamii. Ili jamii kuyaona na kuyafurahia matunda yake inapaswa kuwa na mikakati endelevu ambayo itawanufaisha walimu na wanafunzi. Serikali ina jukumu, sisi pia tunapaswa kuondokana na dharau tuliyonayo kuhusu taaluma ya ualimu. Kufanya ualimu kuvutia huanza na jinsi tunavyouchukulia na jinsi tunavyoelewa umuhimu wake.

Ikiwa leo ni Oktoba 5, ambayo ni Siku ya Walimu Duniani, nimeona ni vyema tukumbushane mambo machache kwa manufaa ya walimu wetu.
 
Nakuhakikishia haitokuja kutokea hata siku moja walimu wa nchi hii kuja kuheshimiwa chini ya utawala huu wa ccm! Na sababu kubwa ni serikali ya ccm kutanguliza siasa kwenye kila kitu! Yaani kwao siasa ndiyo kipaumbele chao! Kuwakwamua wananchi kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa vitendo; kwao siyo kipaumbele kabisa.

Hebu linganisha tu mshahara wa Profesa wa Chuo Kikuu pale UDSM, UDOM, SUA, nk mwenye PhD! Na Mbunge wa Bunge la Tanganyika anaye takiwa kujua tu kusoma na kuandika! Halafu utakuja kuona masihara ya watawala wetu.

Sishangai kuona kila mtu kwenye jamii kwa sasa anatamani kuwa Mbunge! Hata mimi hapa nilipo natamani ningekuwa Mbunge! Yaani unagonga tu meza, mwisho wa mwezi unalamba milioni 12 kama mshahara na posho!!

Serikali inatakiwa kuboresha mishahara ya wafanyakazi wake wote wakiwemo walimu! Ili iendane na uhalisia.


Haina maana kumlipa daktari/mfanyakazi wa TRA, Bandari, nk mshahara mkubwa! Halafu mwalimu wake aliyemfundisha unamlipa mshahara mbuzi! Hapo lazima kada moja itadharaulika tu. Kila kada ipewe kipaumbele chake Sisemi walingane mishahara!! La hasha!

Ninaongelea kuwepo na uwiano unao karibiana kwenye malipo. Maana kwa sasa kuna gap kubwa sana, kiasi cha kuwafanya baadhi ya walimu werevu kuamua kujiongeza kwa kufanya zaidi shughuli zao binafsi za kujiingizia kipato, kuliko kazi ya kufundisha; ambayo haina maslahi ya kueleweka.
 
View attachment 2377753

Mwalimu ana jukumu muhimu katika kuunda haiba ya vijana na kuwatayarisha kuwa raia wazalendo na wanaowajibika. Kando na kazi za kufundisha darasani...
Tatizo walimu wengi ni waoga kudai haki zao. Na hata wakielekezwa namna ya kudai hawako tayari kwa hofu ya kufungiwa mshahara au kunyimwa fursa nyingine.

Na ndio maana baadhi wanaamua kubadili taaluma au kutafuta shughuli nyingine ya kufanya. Watu waliosomea taaluma ya ualimu wapo wengi sana japo hawafundishi.

Isitoshe hata wakigoma athari za mgomo sio za moja kwa moja kama ilivyo kwa fani nyingine kama udaktari, polisi, bankers nk.
 
Nakuhakikishia haitokuja kutokea hata siku moja walimu wa nchi hii kuja kuheshimiwa chini ya utawala huu wa ccm....
Hakika! Kazi zenye manufaa makubwa kwa jamii hazipewi kipaumbele. Wenye dhamana wanadhani ni matumbo na familia zao tu ndizo zenye uhitaji.

Manesi nao wanahaha tu - mazingira ya kazi mabovu na vimishahara punje. Wanahabari hawana mikataba; njaa kila kona. Huwezi kutegemea taifa lenye uwajibikaji kama sauti za Wananchi zinanyongwa kwa mitindo mbalimbali.

Ahsante Tate Mkuu kwa mchango mujarab!
 
Tatizo walimu wengi ni waoga kudai haki zao. Na hata wakielekezwa namna ya kudai hawako tayari kwa hofu ya kufungiwa mshahara au kunyimwa fursa nyingine...
Ni rahisi sana kumnyamazisha mwenye njaa, asiye na kauli. Udhaifu huo unatumiwa ipasavyo na wenye maguvu.
 
Mishahara

Mwalimu ana jukumu muhimu katika kuunda haiba ya vijana na kuwatayarisha kuwa raia wazalendo na wanaowajibika. Kando na kazi za kufundisha darasani, mwalimu pia anatarajiwa kuchukua nafasi ya mshauri, kiongozi na mlezi kwa wanafunzi. Lakini pamoja na umuhimu huo, bado kuna mtazamo hasi dhidi walimu katika jamii.

Ualimu hauchukuliwi kama taaluma inayoheshimika. Kwa siku hizi ni nadra kuona kijana yeyote akitazama ualimu kama chaguo lake la kwanza la taaluma. Hii ni kwakuwa kuna changamoto mbalimbali zinazosababisha taaluma ya ualimu kutoheshimika na wengi nchini Tanzania.

Kwanza, ni kwa sababu ya mishahara midogo ukilinganisha na taaluma nyingine kama vile sheria na udaktari. Aidha, malalamiko ya walimu kuhusu mazingira duni ya kufundishia na kujifunzia, uhaba wa vitendea kazi na ukubwa wa madarasa hayawavutii wengi kuingia katika taaluma hiyo. Hata hivyo, vijana wanaojiunga na taaluma hii ni kwa sababu hawana njia mbadala.

Sababu nyingine ni kwamba vijana wanaona taaluma ya ualimu kama ni kwa ajili ya wale ambao hawakufanya vizuri katika mitihani ya kitaifa.

Hivyo, inaweza kuwa elimu ni sehemu muhimu ya ajenda ya maendeleo ya serikali ya Tanzania, lakini haijawavutia vijana kujiunga na taaluma ya ualimu kwa moyo mmoja kwasababu kila mara inaonekana hasi ikilinganishwa na taaluma nyingine.

Tufanye nini?

Tuboreshe vipato
Ili kuwavutia vijana kwenye taaluma ya ualimu, kuwe na mishahara inayoendana na maisha ya sasa. Serikali inapaswa pia kuunda sera bora za taaluma hii na kutoa motisha kwa kazi za ziada. Hii isiwe tu kwa shule za umma; shule za binafsi pia zina jukumu la kufanya kazi ya ualimu kuvutia. Baadhi ya shule za binafsi pia zinashutumiwa kutotoa mikataba kwa walimu hata baada ya miaka kadhaa. Hili linapaswa kurekebishwa ili kuongeza hamu ya vijana kufundisha.

Mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia
Baadhi ya majengo ya shule yana paa zinazovuja, madarasa yenye vumbi, madawati na meza mbovu au kutokuwepo kabisa na vifaa vya kufundishia. Njia rahisi ya kufanya taaluma ya ualimu ivutie vijana ni kujenga majengo mazuri, ofisi na madarasa kwa waelimishaji. Hii itasababisha kuwa na mazingira rafiki kwa wote – wanafunzi na walimu.

Mazingira ya mwanadamu yanaweza kuathiri sana uzalishaji. Ili kuwafanya walimu kuzingatia majukumu yao na wanafunzi kujifunza vizuri, lazima mazingira yawe ya kuvutia. Shule nyingi za binafsi zinaonekana kuzingatia sana kipengele hiki, ila serikali bado inahitaji nguvu kubwa kuboresha mazingira pamoja viwango vya ufundishaji katika shule za umma.

Teknolojia katika sekta ya elimu
Vijana wa karne ya 21 wanaweza kufanya kazi vizuri katika sehemu za kazi ambazo zinahimiza matumizi ya teknolojia na ubunifu. Mbinu za kizamani za ufundishaji sasa haziendani na wakati tuliomo. Matumizi ya teknolojia yanaweza kuwavutia vijana wengi kwani pia unawapatia fursa ya kukua na maendeleo ya kiteknolojia lakini pia kunaweza kuwasaidia kupunguza mzigo wa kazi. Shule nyingi za umma zina changamoto ya umeme, hivyo ni wakati sasa wa serikali kuona umuhimu wa kuzifanya shule zetu kuwa za kisasa na zinazotoa fursa ya vijana kupata elimu inayoendana na teknolojia ya sasa.

Huduma za msingi kwa walimu
Walimu wa shule za umma zilizopo katika maeneo ya vijijini wanakumbana na changamoto za kila aina: maji, umeme, usafiri na huduma nyingine za kijamii. Wengine kuna wakati wanatumia karibu nusu ya mshahara kama nauli ya kwenda ofisi za halmashauri au kufanya manunuzi ya msingi. Haya si mazingira ambayo vijana wengi wa leo wapo tayari kuyaishi. Ni vyema serikali iangalie utaratibu wa kuwawezesha walimu wanaoishi katika maeneo hayo kuishi vizuri kwa kuwapatia makazi, posho maalum, chakula na kuhakikisha wanapata huduma nyingine za msingi.

Ualimu ni kazi ya muhimu, na pengine ya lazima katika jamii. Ili jamii kuyaona na kuyafurahia matunda yake inapaswa kuwa na mikakati endelevu ambayo itawanufaisha walimu na wanafunzi. Serikali ina jukumu, sisi pia tunapaswa kuondokana na dharau tuliyonayo kuhusu taaluma ya ualimu. Kufanya ualimu kuvutia huanza na jinsi tunavyouchukulia na jinsi tunavyoelewa umuhimu wake.

Ikiwa leo ni Oktoba 5, ambayo ni Siku ya Walimu Duniani, nimeona ni vyema tukumbushane mambo machache kwa manufaa ya walimu wetu.
Mishahara ya walimu sio midogo kama unavyosema hapo kwasababu nasisi walimu tunalipwa kama kada zingine nyingi tu kulingana na viwango vyetu vya elimu na muda tuliokaa kazini. Tusipotoshe watu. Kama ni nyongeza ya mishahara ni watumishi wa kada zote tunahitaji hiyo nyongezaa kwasababu mishahara yetu ni ile ile na utofauti ni mdogo sana mara nyingine.

Pili, walimu tumejenga, tunabadili mboga, tuna usafiri unaoendana na mazingira aliyopo mtu, tunasomesha, na tumefungua biashara nje ya ajira kama tu baadhi ya watumishi wa kada zingine.

Tatu, suala la mazingira ya kufanyia kazi kuwa mazuri au magumu hautuhusu sisi walimu bali linawahusu watoto wenu tunaowafundisha. Wao ndio wanakaa kwenye hayo majengo mabovu na wao ndio wanaokaa chini bila viti.

Nne, huduma za kijamii kama vile maji, umeme na barabara zipo hadi vijijini siku hizi. Mfano mzuri ni huku simiyu.

Tano, unapotosha watu ukisema ualimu haujawahi kuvutia watu kujiunga na ualimu kwasababu kati ya kozi zenye soko zinazokimbiliwa kwasasa ni Ualimu kuanzia wa cheti hadi degree.

Sita, unapotosha watu ukisema ualimu wanaenda wenye marks ndogo kwasababu siku hizi serikali inachukua watu wenye division 1 hadi 3 kwenda kusomea ualimu wa cheti, diploma au degree. Mfano mzuri ni selection za vyuo vya kati za miaka mitatu ya hivi karibuni, watu wenye div 1 na 2 ndio waliochukuliwa kwenda kusomea diploma ya ualimu. Mfano mwingine ni vyuo vikuu, embu nenda pale udsm au udom au must au mzumbe au sua ukajionee mwenyewe watu wanaosomea ualimu wa ngazi ya degree pale wana division One za ngapi. Wakati serikali inachukua watu wenye division 1 hadi 3 kusomea ualimu, kozi zingine kama za afya wanachukuliwa watu wenye division 4 ya 28. Fuatilia.

Saba, sio kweli kuwa watu waliosoma au wanaosoma ualimu wamekosa namna nyingine kwasababu watu husoma kitu chenye soko. Sio kila mtu anapenda mambo ya kukaa miaka 10 bila ajira huku akipigika mtaani eti kisa anataka kuitwa engineer au lawyer wakati maisha ya watumishi ni yale yale.

Nane, acheni kudanganyana kuwa eti waliosoma ualimu wametoka familia duni halafu nyie mliosoma kozi zingine mmetoka familia za kishua wakati tulisoma wote shule za kata na hali ya umaskini wa familia zenu tunaujua. Mtu aliyetoka familia ya kishua hawezi kulilia ajira za serikali au kukaa anapigwa na njaa miaka 10 eti akisaka ajira. Ukweli ni kwamba asilimia 98 ya watu wanaotegemea ajira hapa tanzania wametoka familia duni na maskini ukiwemo wewe hapo. Punguzeni kujiona wa kishua wakati wote mnategemea mshahara wa kati ya laki 5 hadi milioni 4.
 
Ni rahisi sana kumnyamazisha mwenye njaa, asiye na kauli. Udhaifu huo unatumiwa ipasavyo na wenye maguvu.
Kwahiyo wewe unataka walimu wapindue serikali kwasababu zipi za msingi wakati watumishi tunalipwa kulingana na uwezo wa serikali yetu? Kwa taarifa yako mishahara ya walimu haina tofauti na mishahaara ya kada zingine nyingi hapa tz. Pia changamoto ni zile zile kwenye kada zote na ndio maana ukiend akwenye mahakama nyingi unakuta majengo chakavu kama tu kwenye shule au taasisi nyingi za serikali.
 
Wal
Nakuhakikishia haitokuja kutokea hata siku moja walimu wa nchi hii kuja kuheshimiwa chini ya utawala huu wa ccm! Na sababu kubwa ni serikali ya ccm kutanguliza siasa kwenye kila kitu! Yaani kwao siasa ndiyo kipaumbele chao! Kuwakwamua wananchi kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa vitendo; kwao siyo kipaumbele kabisa.

Hebu linganisha tu mshahara wa Profesa wa Chuo Kikuu pale UDSM, UDOM, SUA, nk mwenye PhD! Na Mbunge wa Bunge la Tanganyika anaye takiwa kujua tu kusoma na kuandika! Halafu utakuja kuona masihara ya watawala wetu.

Sishangai kuona kila mtu kwenye jamii kwa sasa anatamani kuwa Mbunge! Hata mimi hapa nilipo natamani ningekuwa Mbunge! Yaani unagonga tu meza, mwisho wa mwezi unalamba milioni 12 kama mshahara na posho!!

Serikali inatakiwa kuboresha mishahara ya wafanyakazi wake wote wakiwemo walimu! Ili iendane na uhalisia.


Haina maana kumlipa daktari/mfanyakazi wa TRA, Bandari, nk mshahara mkubwa! Halafu mwalimu wake aliyemfundisha unamlipa mshahara mbuzi! Hapo lazima kada moja itadharaulika tu. Kila kada ipewe kipaumbele chake Sisemi walingane mishahara!! La hasha!

Ninaongelea kuwepo na uwiano unao karibiana kwenye malipo. Maana kwa sasa kuna gap kubwa sana, kiasi cha kuwafanya baadhi ya walimu werevu kuamua kujiongeza kwa kufanya zaidi shughuli zao binafsi za kujiingizia kipato, kuliko kazi ya kufundisha; ambayo haina maslahi ya kueleweka.
Walimu tunaheshimika na watu wote wanaojitambua ila wale wote ambao hawajitambui na waliofeli shule ndio hawaheshimu walimu.
 
Hakika! Kazi zenye manufaa makubwa kwa jamii hazipewi kipaumbele. Wenye dhamana wanadhani ni matumbo na familia zao tu ndizo zenye uhitaji.

Manesi nao wanahaha tu - mazingira ya kazi mabovu na vimishahara punje. Wanahabari hawana mikataba; njaa kila kona. Huwezi kutegemea taifa lenye uwajibikaji kama sauti za Wananchi zinanyongwa kwa mitindo mbalimbali.

Ahsante Tate Mkuu kwa mchango mujarab!
Kiongozi ni wanasiasa pekee ndio wenye mazingira mazuri ya kazi na mishahara mizuri. Watumishi wengine wote wanaganga njaa tu kwa mishahara ya kati ya laki 5 na milioni 4.
 
Tatizo walimu wengi ni waoga kudai haki zao. Na hata wakielekezwa namna ya kudai hawako tayari kwa hofu ya kufungiwa mshahara au kunyimwa fursa nyingine.

Na ndio maana baadhi wanaamua kubadili taaluma au kutafuta shughuli nyingine ya kufanya. Watu waliosomea taaluma ya ualimu wapo wengi sana japo hawafundishi.

Isitoshe hata wakigoma athari za mgomo sio za moja kwa moja kama ilivyo kwa fani nyingine kama udaktari, polisi, bankers nk.
Anza wewe kuwa mstari wa mbele.
Nakuhakikishia haitokuja kutokea hata siku moja walimu wa nchi hii kuja kuheshimiwa chini ya utawala huu wa ccm! Na sababu kubwa ni serikali ya ccm kutanguliza siasa kwenye kila kitu! Yaani kwao siasa ndiyo kipaumbele chao! Kuwakwamua wananchi kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa vitendo; kwao siyo kipaumbele kabisa.

Hebu linganisha tu mshahara wa Profesa wa Chuo Kikuu pale UDSM, UDOM, SUA, nk mwenye PhD! Na Mbunge wa Bunge la Tanganyika anaye takiwa kujua tu kusoma na kuandika! Halafu utakuja kuona masihara ya watawala wetu.

Sishangai kuona kila mtu kwenye jamii kwa sasa anatamani kuwa Mbunge! Hata mimi hapa nilipo natamani ningekuwa Mbunge! Yaani unagonga tu meza, mwisho wa mwezi unalamba milioni 12 kama mshahara na posho!!

Serikali inatakiwa kuboresha mishahara ya wafanyakazi wake wote wakiwemo walimu! Ili iendane na uhalisia.


Haina maana kumlipa daktari/mfanyakazi wa TRA, Bandari, nk mshahara mkubwa! Halafu mwalimu wake aliyemfundisha unamlipa mshahara mbuzi! Hapo lazima kada moja itadharaulika tu. Kila kada ipewe kipaumbele chake Sisemi walingane mishahara!! La hasha!

Ninaongelea kuwepo na uwiano unao karibiana kwenye malipo. Maana kwa sasa kuna gap kubwa sana, kiasi cha kuwafanya baadhi ya walimu werevu kuamua kujiongeza kwa kufanya zaidi shughuli zao binafsi za kujiingizia kipato, kuliko kazi ya kufundisha; ambayo haina maslahi ya kueleweka.
Kiongozi madaktari, watu wa tra, watu wa bandari na wengine wote unaofikiria wewe wapo wenye mishahara ya laki 4 na elfu 92 na wapo wenye mishahara zaidi ya hapo kama tu ilivyo kwenye kada zingine zote. Kuna wenye elimu ya cheti ambao huwa na kiwango cha chini cha mshahara na kuna wenye diploma na degree ambao kiwango chao cha mshahara ni kikubwa kuliko wa cheti na kuna wenye masters ambao huwa na mshahara mkubwa zaidi ya hao wa chini yake.

Hata kwenye ualimu pia ni hivyo hivyo. Kuna walimu wa cheti ambao huanza na kiwango chao, kuna diploma ambao huanza na kiwango kikubwa kuliko wa cheti halafu kuna wenye degree ambao huanza na kiwango kikubwa kuliko wa diploma,n.k

Unachotakiwa kujua ni kwamba hapa tz mishahara ya kada zote haiwezi kukufanya uwe tajiri kama akina mo au bakhresa na ndio maana huwezi kusikia daktari aliyeanzisha kiwanda kwa kutumia mshahara wake ambao huwa kati ya laki 5 na milioni 4. Watumishi wa tra, bandari na madaktari wana mishahara ya kawaida sana. Wenye mishahara mizuri hapa tz ni wanasiasa pekee.
 
Back
Top Bottom