Intelligence Justice
JF-Expert Member
- Oct 23, 2020
- 3,036
- 3,479
Wakuu,
Ni dhahiri kabisa kwa sasa mataifa ya Ulaya na Marekani wamekwisha ona udhaifu wa nchi za kiafrika kutosimamiana yenyewe kwa kuteteana au kuonyana pindi inapotokea chi nyingine nje ya bara Afrika linapoanza ukosoaji kwa kutimia sababu halali lakini malengo ni kinyume chake.
1. Hakuna taifa lolote ndani ya Afrika au Umoja wa nchi za |Afrika unakemea upotofu wa taifa jingine au kutetea udhalilishwaji kutoka wa mataifa makubwa yenye nguvu
2. Kila uchaguzi wa kila nchi unapowadia kila nchi husika, inapaswa pawepo chombo maalumu cha usimamizi wa chaguzi hizo ikishiriana na tume ya nchi hiyo kwa masharti yatakayowekwa kwa mujibu wa sheria
3. Kuhakikisha balozi zinazowakilisha nchi zao haziingilii mambo ya ndani ya nchi husika kinyume na majukumu yao yanayowataka kujadiliana na pande tofauti za kisiasa kabla ya kutoa tamko badala ya wanavyofanya kwa sasa. Ni kweli maeneo ya ofisi na makazi ya balozi au mtumishi yeyote mwandamizi wa uwakilishi huo unasimama kama eneo halali la utawala wa nchi hivyo taratibu za kimataifa zinawajibika kufuatwa ipasavyo
4. Mabalozi wengi kutoa nchi za Ulaya na Marekani kwa sasa wanachochea machafuko ya uasi katika nchi za ukaazi sio kwamba wanazipenda sana nchi za kiafrika, lahasha ila ni kwa maslahi ya kiuchumi ya nchi wanazoziwakilisha au makampuni yenye miradi katika nchi hiyo maaana wanawajibika pia kusimamia;
5. Huko Ivory coast, Nigeria, Uganda nk ambapo ni msimu wa kufanya uchaguzi tayari wanaonesha kupendelea vyama pinzani kwa kutoa matamko bila ya kufanya mawasiliano ya kiitifaki kupata maelezo toka upande wa pili na kushauri badala ya kuonesha kwamba kile walichokipata kutoa upande mmoja uko sahihi kinyume na utaratibu wa haki asili (natural justice whereas nobody should be condemned unheard) This is an obvious breach of diplomatic missions;
5. Nchi za kiafrika hazina umoja la sivyo wangekuwa wametoa tamko kuhusiana na tabia ya mataifa ya Ulaya na Marekani kuingilia mambo ya ndani kwa kisingizio ya kutetea demokrasia na haki za binadamu. Hakuna haki isiyokuwa na wajibu kutoka pande mbili;
Kwanini malalamiko ya kisiasa yanapelekwa kwenye balozi na taasisi za kimataifa wakati tuna sheria zetu kisa ni misaada na mikopo wanayotoa?
Hakuna taifa la Ulaya, Marekani linaloipenda Tanzania au kwamba kuna uvunjifu mkubwa sana wa haki za binadamu kuzidi Marekani ambko hadi sasa wameuwawa watu kadhaa tena weusi lakini hakuna hatua za dhati zinazochukuliwa kudhibiti badala yake wana piga kelele dhidi ya mataifa ya kiafrika kwa tamaa zrasirimali zetu na kuweka watu wao wataofanikisha ukwapuaji.
Waafrika amkeni sasa, kukataa haraka sana vinginevyo itatokea wameshaingia Ikulu wenyewe. Mkifanya hivyo heshima itakuwepo, bila hivyo msahau kuonewa kwa mgongo wa misaada, mikopo kwa kisingizio cha demokrasia na haki za binadamu. Doomsdays are speedily coming to overwhelm african sovereignty.
Nawasilisha
Ni dhahiri kabisa kwa sasa mataifa ya Ulaya na Marekani wamekwisha ona udhaifu wa nchi za kiafrika kutosimamiana yenyewe kwa kuteteana au kuonyana pindi inapotokea chi nyingine nje ya bara Afrika linapoanza ukosoaji kwa kutimia sababu halali lakini malengo ni kinyume chake.
1. Hakuna taifa lolote ndani ya Afrika au Umoja wa nchi za |Afrika unakemea upotofu wa taifa jingine au kutetea udhalilishwaji kutoka wa mataifa makubwa yenye nguvu
2. Kila uchaguzi wa kila nchi unapowadia kila nchi husika, inapaswa pawepo chombo maalumu cha usimamizi wa chaguzi hizo ikishiriana na tume ya nchi hiyo kwa masharti yatakayowekwa kwa mujibu wa sheria
3. Kuhakikisha balozi zinazowakilisha nchi zao haziingilii mambo ya ndani ya nchi husika kinyume na majukumu yao yanayowataka kujadiliana na pande tofauti za kisiasa kabla ya kutoa tamko badala ya wanavyofanya kwa sasa. Ni kweli maeneo ya ofisi na makazi ya balozi au mtumishi yeyote mwandamizi wa uwakilishi huo unasimama kama eneo halali la utawala wa nchi hivyo taratibu za kimataifa zinawajibika kufuatwa ipasavyo
4. Mabalozi wengi kutoa nchi za Ulaya na Marekani kwa sasa wanachochea machafuko ya uasi katika nchi za ukaazi sio kwamba wanazipenda sana nchi za kiafrika, lahasha ila ni kwa maslahi ya kiuchumi ya nchi wanazoziwakilisha au makampuni yenye miradi katika nchi hiyo maaana wanawajibika pia kusimamia;
5. Huko Ivory coast, Nigeria, Uganda nk ambapo ni msimu wa kufanya uchaguzi tayari wanaonesha kupendelea vyama pinzani kwa kutoa matamko bila ya kufanya mawasiliano ya kiitifaki kupata maelezo toka upande wa pili na kushauri badala ya kuonesha kwamba kile walichokipata kutoa upande mmoja uko sahihi kinyume na utaratibu wa haki asili (natural justice whereas nobody should be condemned unheard) This is an obvious breach of diplomatic missions;
5. Nchi za kiafrika hazina umoja la sivyo wangekuwa wametoa tamko kuhusiana na tabia ya mataifa ya Ulaya na Marekani kuingilia mambo ya ndani kwa kisingizio ya kutetea demokrasia na haki za binadamu. Hakuna haki isiyokuwa na wajibu kutoka pande mbili;
Kwanini malalamiko ya kisiasa yanapelekwa kwenye balozi na taasisi za kimataifa wakati tuna sheria zetu kisa ni misaada na mikopo wanayotoa?
Hakuna taifa la Ulaya, Marekani linaloipenda Tanzania au kwamba kuna uvunjifu mkubwa sana wa haki za binadamu kuzidi Marekani ambko hadi sasa wameuwawa watu kadhaa tena weusi lakini hakuna hatua za dhati zinazochukuliwa kudhibiti badala yake wana piga kelele dhidi ya mataifa ya kiafrika kwa tamaa zrasirimali zetu na kuweka watu wao wataofanikisha ukwapuaji.
Waafrika amkeni sasa, kukataa haraka sana vinginevyo itatokea wameshaingia Ikulu wenyewe. Mkifanya hivyo heshima itakuwepo, bila hivyo msahau kuonewa kwa mgongo wa misaada, mikopo kwa kisingizio cha demokrasia na haki za binadamu. Doomsdays are speedily coming to overwhelm african sovereignty.
Nawasilisha