Kuna haja kwa Sahara media(Mhe Diallo/Star tv) kumrejesha Babu mkombe wa FUTUHI

The Intelligent

JF-Expert Member
Dec 27, 2013
2,459
818
Wakuu kwa wale watazamaji wa kipindi cha futuhi kinachorushwa kila Alhamis star tv, hawawezi kumsahau John Mlinga a.k.a Babu mkombe hasa kwa ububunifu wake ktk kufurahisha watazamaji.

Naomba isieleweke kama nampigia debe huyo jamaa, ila wengi wetu ni mashahidi, kipindi cha FUTUHI kwa sasa kimepoa sana/hakina radha, hii nayo inapunguza watazamaji vilevile kuwanyima watazamaji kile wanachotaka.

Wachekeshaji wa sasa wa futuhi ni magumashi tu, na hii imepelekea kupungua kwa watazamaji wa star tv.
 
Hivi kumbe vikundi vya vichekesho vinamilikiwa na wenye vituo vya TV? Si kwamba wachekeshaji wameunda vikundi vyao na kuomba wenye tv wawape airtime? Kama dhana ya pili ni sahihi basi huyo babu awaombe futuhi wenzake wamrejeshe kundini.
 
Hivi kumbe vikundi vya vichekesho vinamilikiwa na wenye vituo vya TV? Si kwamba wachekeshaji wameunda vikundi vyao na kuomba wenye tv wawape airtime? Kama dhana ya pili ni sahihi basi huyo babu awaombe futuhi wenzake wamrejeshe kundini.

Si unaambiwa alienda kupiga show tabora bila kibali cha boss ndio maana akatimuliwa! hapo ni mkataba tu na huruhusiwi kufanya sanaa nje ya mkataba.
 
Dah, ila sekta ya sanaa ina manyanyaso!

Kwa Tanzania ni karibu sekta zote, halafu star media hawajali watazamaji wao, ndio maana wanawafukuza wachekeshaji bila kujali namna watazamaji watavyojisikia, kuondoka kwa mkombe ni pigo kwa futuhi, kwa kweli watu wengi sasa wamepunguza kutazama hiyo televisheni.
 
Last edited by a moderator:
tatizo msaaniiii kama lilivyo jina akishaona anapata shavu kichwa hichoooo
 
Unajua uchekeshaji ni kipaji sio kusomea kama maigizo na babu bukombe ana kipaji na yule aliyekuwa anaigiza kama mtangazaji wamalize tofauti zao waungane. Waangalie Kenya na Uganda sasa hivi wachekeshaji wanachekesha watu ukumbini na kupata hela za kutosha
 
Hapo me naona brother k tuu ndo anafiti wengine wote ni ovyo.......afu mbona okechi pekee ndiye aliyebaki katika wakongwe wa futuhi!! Au yeye ndo anawapiga majungu wenzake??
 
Back
Top Bottom